< 1 Crônicas 22 >
1 Então David disse: “Esta é a casa de Deus Javé, e este é o altar de holocausto para Israel”.
Ndipo Daudi akasema, “Nyumba ya Bwana Mungu itakuwa mahali hapa, pia pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Israeli.”
2 David deu ordens para reunir os estrangeiros que estavam na terra de Israel; e colocou pedreiros para cortar pedras vestidas para construir a casa de Deus.
Kwa hiyo Daudi akatoa amri wakusanyike wageni wote waliokuwa wanaishi Israeli, na kutoka miongoni mwao akaweka waashi ili kuchonga mawe kwa ajili ya kujenga nyumba ya Mungu.
3 David preparou ferro em abundância para os pregos das portas dos portões e para os acoplamentos, e bronze em abundância sem peso,
Daudi akatoa chuma tele ili kutengenezea misumari kwa ajili ya mafungo ya malango ya nyumba na shaba tele isiyopimika.
4 e cedros sem número, para os sidônios e o povo de Tiro trouxe cedros em abundância para David.
Pia akatoa magogo ya mierezi yasiyohesabika, kwa kuwa Wasidoni na Watiro walikuwa wamemletea Daudi idadi kubwa ya mierezi.
5 David disse: “Salomão meu filho é jovem e terno, e a casa que será construída para Iavé deve ser extremamente magnífica, de fama e de glória em todos os países. Por isso, vou me preparar para ela”. Assim, Davi se preparou abundantemente antes de sua morte.
Daudi akasema, “Mwanangu Solomoni bado ni mdogo wa umri na hana uzoefu. Nyumba itakayojengwa kwa ajili ya Bwana inatakiwa iwe yenye uzuri mwingi na sifa na fahari mbele ya mataifa yote. Kwa hiyo nitaifanyia matayarisho.” Daudi akafanya matayarisho makubwa kabla ya kifo chake.
6 Então ele chamou por Salomão seu filho, e ordenou-lhe que construísse uma casa para Iavé, o Deus de Israel.
Kisha akamwita Solomoni mwanawe akamwagiza kujenga nyumba kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli.
7 David disse a Salomão, seu filho: “Quanto a mim, estava em meu coração construir uma casa em nome de Javé, meu Deus.
Daudi akamwambia Solomoni: “Mwanangu, nilikuwa na jambo hili ndani ya moyo wangu kujenga nyumba kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wangu.
8 Mas a palavra de Javé veio a mim, dizendo: 'Vocês derramaram sangue abundantemente e fizeram grandes guerras'. Não construirás uma casa em meu nome, porque derramaste muito sangue sobre a terra à minha vista”.
Lakini neno hili la Bwana likanijia, kusema: ‘Wewe umemwaga damu nyingi na kupigana vita vingi. Wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, kwa sababu umemwaga damu nyingi juu ya nchi machoni pangu.
9 Eis que vos nascerá um filho, que será um homem de paz”. Eu lhe darei descanso de todos os seus inimigos ao redor; pois seu nome será Salomão, e darei paz e sossego a Israel em seus dias.
Lakini utakuwa na mwana ambaye atakuwa mtu wa amani na utulivu nami nitampa utulivu mbele ya adui zake wote pande zote. Jina lake ataitwa Solomoni, nami nitawapa Israeli amani na utulivu wakati wa utawala wake.
10 Ele construirá uma casa em meu nome; e ele será meu filho, e eu serei seu pai; e estabelecerei o trono de seu reino sobre Israel para sempre'.
Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu. Yeye atakuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake. Nami nitakifanya imara kiti chake cha enzi cha utawala wake katika Israeli milele.’
11 Agora, meu filho, que Javé esteja contigo e te faça prosperar, e construa a casa de Javé, teu Deus, como ele falou a teu respeito.
“Sasa, mwanangu, Bwana awe pamoja nawe, nawe uwe na mafanikio upate kuijenga nyumba ya Bwana Mungu wako, kama alivyosema utafanya.
12 Que Javé te dê discrição e compreensão, e te coloque no comando de Israel, para que possas manter a lei de Javé teu Deus”.
Bwana na akupe hekima na ufahamu wakati atakuweka juu ya Israeli, ili uweze kuishika sheria ya Bwana Mungu wako.
13 Então você prosperará, se observar os estatutos e as ordenanças que Javé deu a Moisés a respeito de Israel. Seja forte e corajoso. Não tenham medo e não fiquem consternados.
Ndipo utakapofanikiwa, ikiwa utakuwa na bidii kutii amri na sheria Bwana alizompa Mose kwa ajili ya Israeli. Uwe hodari na ushujaa. Usiogope wala usikate tamaa.
14 Agora, eis que em minha aflição preparei para a casa de Javé cem mil talentos de ouro, um milhão de talentos de prata, bronze e ferro sem peso; pois está em abundância. Eu também preparei madeira e pedra; e você pode acrescentar a eles.
“Nimejitaabisha sana ili kupata mahitaji kwa ajili ya Hekalu la Bwana: talanta 100,000 za dhahabu, talanta 1,000,000 za fedha na kiasi kisichopimika cha shaba na chuma, pia mbao na mawe. Nawe waweza kuviongeza.
15 Também há com vocês trabalhadores em abundância - cortadores e trabalhadores de pedra e madeira, e todos os tipos de homens que são hábeis em todo tipo de trabalho;
Unao wafanyakazi wengi: Wachonga mawe, waashi na maseremala, pamoja na watu walio na ustadi katika kila kazi
16 do ouro, da prata, do bronze e do ferro, não há número. Levantem-se e façam, e que Yahweh esteja com vocês”.
wa kufua dhahabu, fedha, shaba na chuma, mafundi wasiohesabika. Sasa basi anza kazi hii, naye Bwana awe pamoja nawe.”
17 David também ordenou a todos os príncipes de Israel que ajudassem Salomão, seu filho, dizendo:
Kisha Daudi akawaamuru viongozi wote wa Israeli wamsaidie Solomoni mwanawe.
18 “Não é Javé o seu Deus com você? Ele não lhe deu descanso de todos os lados? Pois ele entregou os habitantes da terra nas minhas mãos; e a terra está subjugada diante de Iavé e diante de seu povo.
Akawaambia, “Je, Bwana Mungu wenu si yuko pamoja na ninyi? Pia si amewapa raha pande zote? Kwa maana amewatia wenyeji wa nchi mkononi mwangu, nayo nchi iko chini ya Bwana na watu wake.
19 Agora ponha seu coração e sua alma para seguir Yahweh seu Deus. Levantai-vos, pois, e construí o santuário de Javé Deus, para trazer a arca da aliança de Javé e os vasos sagrados de Deus para a casa que será construída em nome de Javé”.
Sasa itoeni mioyo yenu na nafsi zenu katika kumtafuta Bwana Mungu wenu. Anzeni kujenga Maskani ya Bwana Mungu, ili mweze kulileta Sanduku la Agano la Bwana na vyombo vitakatifu vya Mungu katika Hekalu litakalojengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.”