< Salmos 80 >

1 Para o regente, conforme “Susanedute”. Samo de Asafe: Ó Pastor de Israel, inclina teus ouvidos [a mim], tu que pastoreias a José como a ovelhas, que habitas entre os querubins, mostra teu brilho,
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 Perante Efraim, Benjamim e Manassés, desperta o teu poder, e vem para nos salvar.
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 Restaura-nos, Deus, e faz brilhar o teu rosto; e [assim] seremos salvos.
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 Ó SENHOR Deus dos exércitos, até quando ficarás irritado contra a oração de teu povo?
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 Tu os alimentas com pão de lágrimas, e lhes faz beber lágrimas com grande medida.
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 Puseste-nos como a briga de nossos vizinhos, e nossos inimigos zombam [de nós].
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 Restaura-nos, ó Deus dos exércitos, e faz brilhar o teu rosto; e [assim] seremos salvos.
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 Tu transportaste [tua] vinha do Egito, tiraste as nações, e a plantaste.
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 Preparaste [um lugar] para ela, e a fizeste estender suas raízes, e ela encheu a terra.
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 Os montes foram cobertos pela sombra dela, e seus ramos [se tornaram] como o dos mais fortes cedros.
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 Ela espalhou seus ramos até o mar, e seus brotos até o rio.
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 Por que [pois] quebraste seus muros, de modo que os que passam arrancam seus frutos?
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 O porco do campo a destruiu; os animais selvagens a devoraram.
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 Ó Deus dos exércitos, volta, te pedimos; olha desde os céus, e vê, e visita esta vinha;
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 E a videira que tua mão direita plantou; o ramo que fortificaste para ti.
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 [Ela está] queimada pelo fogo, [e] cortada; perecem pela repreensão de tua face.
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 Seja tua mão sobre o homem de tua mão direita, sobre o filho do homem a quem fortificaste para ti.
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 Assim não desviaremos de ti; guarda-nos em vida, e chamaremos o teu nome.
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 SENHOR Deus dos exércitos, restaura-nos; faz brilhar o teu rosto, e [assim] seremos salvos.
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.

< Salmos 80 >