< Salmos 63 >

1 Salmo de Davi, quando ele estava no deserto de Judá: Deus, tu [és] meu Deus. Eu te busco ao amanhecer; minha alma tem sede de ti, minha carne muito te deseja, em terra seca, cansativa, sem águas.
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 Para que eu te veja em teu santuário, para ver tua força e tua glória.
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 Porque tua bondade [é] melhor que a vida; meus lábios te louvarão.
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 Assim te bendirei em minha vida; por teu nome levantarei minhas mãos.
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 Minha alma será saciada, como que de gorduras e muita comida; e minha boca te louvará com lábios alegres,
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 Quando eu me lembrar de ti em minha cama; nas vigílias da noite meus pensamentos estarão em ti.
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 Porque tu tens sido meu socorro; e à sombra de tuas asas cantarei de alegria.
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 Minha alma está apegada a ti; tua mão direita me sustenta.
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 Porém aqueles que procuram assolar a minha alma irão para as profundezas da terra.
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 Eles serão derrubados pela força da espada; serão repartidos entre raposas.
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 Mas o Rei se alegrará em Deus; todo o que por ele jurar se alegrará, porque a boca dos mentirosos será tapada.
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.

< Salmos 63 >