< Salmos 6 >

1 Salmo de Davi para o regente, com instrumentos de cordas, uma harpa de oito cordas: SENHOR, não me repreendas na tua ira; e não me castigues em teu furor.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 Tem misericórdia de mim, SENHOR; porque eu [estou] enfraquecido; cura-me, SENHOR, porque meus ossos estão afligidos.
Unirehemu Bwana, kwa maana nimedhoofika; Ee Bwana, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.
3 Até minha alma está muito aflita; e tu, SENHOR, até quando?
Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?
4 Volta, SENHOR; livra minha alma; salva-me por tua bondade.
Geuka Ee Bwana, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
5 Porque na morte não há lembrança de ti; no Xeol quem te louvará? (Sheol h7585)
Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? (Sheol h7585)
6 Já estou cansado do meu gemido; toda a noite eu inundo a minha cama; com minhas lágrimas molho meu leito.
Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha nafurikisha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha viti vyangu vya fahari kwa machozi.
7 Meus olhos estão desolados de mágoa, [e] têm se envelhecido por causa de todos os meus adversários.
Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
8 Sai para longe de mim, todos vós praticantes de maldade; porque o SENHOR já ouviu a voz do meu choro.
Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
9 O SENHOR tem ouvido a minha súplica; o SENHOR aceitará a minha oração.
Bwana amesikia kilio changu kwa huruma, Bwana amekubali sala yangu.
10 Todos os meus inimigos se envergonharão e ficarão muito perturbados; voltarão para trás, [e] repentinamente se envergonharão.
Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.

< Salmos 6 >