< Salmos 135 >

1 Aleluia! Louvai o nome do SENHOR; louvai [-o] vós, servos do SENHOR,
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 Que prestais serviço na Casa do SENHOR, nos pátios da Casa do nosso Deus.
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Louvai ao SENHOR, porque o SENHOR é bom; cantai louvores ao seu nome, porque é agradável;
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 Porque o SENHOR escolheu para si a Jacó, a Israel como propriedade sua;
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 Porque eu sei que o SENHOR é grande, e nosso Senhor está acima de todos os deuses.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 O SENHOR faz tudo o que quer, nos céus, na terra, nos mares, e [em] todos os abismos.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 Ele faz as nuvens subirem desde os confins da terra, faz os relâmpagos com a chuva; ele produz os ventos de seus tesouros.
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 Ele feriu os primogênitos do Egito, desde os homens até os animais.
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 Ele enviou sinais e prodígios no meio de ti, Egito; contra Faraó, e contra todos os seus servos.
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Ele feriu muitas nações, e matou reis poderosos:
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 Seom, rei dos amorreus, e Ogue, rei de Basã; e todos os reinos de Canaã.
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 E deu a terra deles como herança; como herança a Israel, seu povo.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 Ó SENHOR, teu nome [dura] para sempre; [e] tua memória, SENHOR, de geração em geração.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 Porque o SENHOR julgará a seu povo; e terá compaixão de seus servos.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 Os ídolos das nações [são] prata e ouro; [são] obra de mãos humanas.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 Têm boca, mas não falam; têm olhos, mas não veem.
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 Têm ouvidos, mas não ouvem; não têm respiração em sua boca.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Tornem-se como eles os que os fazem, [e] todos os que confiam neles.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Casa de Israel, bendizei ao SENHOR! Casa de Arão, bendizei ao SENHOR!
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Casa de Levi, bendizei ao SENHOR! Vós que temeis ao SENHOR, bendizei ao SENHOR.
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Bendito seja o SENHOR desde Sião, ele que habita em Jerusalém. Aleluia!
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Salmos 135 >