< Salmos 129 >

1 Cântico dos degraus: Diga Israel: Desde minha juventude muitas vezes me afligiram.
Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
2 Desde minha juventude, muitas vezes me afligiram, porém não prevaleceram contra mim.
wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
3 Lavradores lavraram sobre minhas costas, fizeram compridos os seus sulcos.
Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
4 O SENHOR é justo; ele cortou as cordas dos perversos.
Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
5 Sejam envergonhados, e voltem para trás todos os que odeiam a Sião.
Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
6 Sejam como a erva dos telhados, que se seca antes que cresça.
Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7 Com que o ceifeiro não enche sua mão, nem o braço daquele que amarra os molhos.
kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8 Nem também os que passam, dizem: A bênção do SENHOR seja sobre vós; nós vos bendizemos no nome do SENHOR.
Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”

< Salmos 129 >