< Salmos 107 >

1 Agradecei ao SENHOR, porque ele é bom; porque sua bondade [dura] para sempre.
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 Digam [isso] os resgatados pelo SENHOR, os quais ele resgatou das mão do adversário.
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 E os que ele ajuntou de todas as terras, do oriente e do ocidente, do norte e do sul.
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Os que andaram sem rumo no deserto, por caminhos solitários; os que não acharam cidade para morarem.
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 Famintos e sedentos, suas almas neles desfaleciam.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 Mas eles clamaram ao SENHOR em suas angústias, e ele os livrou de suas aflições.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 E os levou ao caminho correto, para irem a uma cidade de moradia.
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 Agradeçam ao SENHOR por sua bondade, e suas maravilhas perante os filhos dos homens.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 Porque ele fartou a alma sedenta, e encheu de bem a alma faminta;
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 Os que estavam sentados em trevas e sombra de morte, presos com aflição e ferro,
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 Porque se rebelaram contra os mandamentos de Deus, e rejeitaram o conselho do Altíssimo.
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 Por isso ele abateu seus corações com trabalhos cansativos; eles tropeçaram, e não houve quem os socorresse.
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 Porém eles clamaram ao SENHOR em suas angústias, e ele os livrou de suas aflições.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 Ele os tirou das trevas e da sombra da morte, e quebrou suas correntes de prisão.
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 Agradeçam ao SENHOR pela sua bondade, e suas maravilhas perante os filhos dos homens.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 Porque ele quebrou as portas de bronze, e despedaçou os ferrolhos de ferro.
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Os tolos foram afligidos por causa de seu caminho de transgressões e por suas perversidades.
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 A alma deles perdeu o interesse por todo tipo de comida, e chegaram até às portas da morte.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 Porém eles clamaram ao SENHOR em suas angústias, e ele os livrou de suas aflições.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 Ele enviou sua palavra, e os sarou; e ele os livrou de suas covas.
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 Agradeçam ao SENHOR por sua bondade, e suas maravilhas perante os filhos dos homens.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 E sacrifiquem sacrifícios de gratidão; e anunciai as obras dele com alegria.
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 Os que descem ao mar em navios, trabalhando em muitas águas,
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 Esses veem as obras do SENHOR, e suas maravilhas nas profundezas.
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 [Porque] quando ele fala, ele faz levantar tormentas de vento, que levanta suas ondas.
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 Elas sobem aos céus, [e] descem aos abismos; a alma deles se derrete de angústia.
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 Eles cambaleiam e vacilam como bêbados, e toda a sabedoria deles se acaba.
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 Então eles clamaram ao SENHOR em suas angústias, e ele os tirou de suas aflições.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 Ele fez cessar as tormentas, e as ondas se calaram.
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 Então se alegraram, porque houve calmaria; e ele os levou ao porto que queriam [chegar].
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 Agradeçam ao SENHOR por sua bondade, e suas maravilhas perante os filhos dos homens;
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 E exaltem a ele na assembleia do povo, e o glorifiquem na reunião dos anciãos.
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 Ele torna os rios em deserto, e as saídas de águas em terra seca.
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 A terra frutífera em salgada, pela maldade dos que nela habitam.
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 Ele torna o deserto em lagoa, e a terra seca em nascentes de águas.
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 E faz aos famintos habitarem ali; e eles edificam uma cidade para morarem;
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 E semeiam campos, e plantam vinhas, que produzem fruto valioso.
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 E ele os abençoa, e se multiplicam muito, e o gado dele não diminui.
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 Mas [quando] eles se diminuem e se abatem, por causa da opressão, mal e aflição;
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 Ele derrama desprezo sobre os governantes, e os faz andar sem rumo pelos desertos, sem [terem] caminho.
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 Mas ao necessitado, ele levanta da opressão a um alto retiro, e faz famílias como a rebanhos.
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 Os corretos, ao verem, ficam alegres, e todo perverso se calará.
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 Quem é sábio, que preste atenção a estas coisas, e reflita nas bondades do SENHOR.
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.

< Salmos 107 >