< Provérbios 29 >

1 O homem que age com teimosia, mesmo depois de muitas repreensões, será tão destruído que não terá mais cura.
Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
2 Quando os justos se engrandecem, o povo se alegra; mas quando o perverso domina, o povo geme.
Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
3 O homem que ama a sabedoria alegra a seu pai; mas o companheiro de prostitutas gasta os bens.
Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
4 O rei por meio da justiça firma a terra; mas o amigo de subornos a transtorna.
Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
5 O homem que lisonjeia a seu próximo arma uma rede para seus pés.
Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
6 Na transgressão do homem mau há uma armadilha; mas o justo se alegra e se enche de alegria.
Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
7 O justo considera a causa judicial dos pobres; [mas] o perverso não entende [este] conhecimento.
Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
8 Homens zombadores trazem confusão a cidade; mas os sábios desviam a ira.
Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
9 O homem sábio que disputa no julgamento contra um tolo, mesmo se perturbado ou rindo, não terá descanso.
Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
10 Homens sanguinários odeiam o honesto; mas os corretos procuram o seu bem.
Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
11 O louco mostra todo o seu ímpeto; mas o sábio o mantém sob controle.
Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
12 O governante que dá atenção a palavras mentirosas, todos os seus servos serão perversos.
Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
13 O pobre e o enganador se encontram: o SENHOR ilumina aos olhos de ambos.
Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
14 O rei que julga aos pobres por meio da verdade, seu trono se firmará para sempre.
Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
15 A vara e a repreensão dão sabedoria; mas o rapaz deixado solto envergonha a sua mãe.
Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
16 Quando os perversos se multiplicam, multiplicam-se as transgressões; mas os justos verão sua queda.
Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
17 Castiga a teu filho, e ele te fará descansar, e dará prazeres à tua alma.
Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
18 Não havendo visão profética, o povo fica confuso; porém o que guarda a lei, ele é bem-aventurado.
Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19 O servo não será corrigido por meio de palavras; porque [ainda que] entenda, mesmo assim ele não responderá [corretamente].
Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
20 Viste um homem precipitado em suas palavras? Mais esperança há para um tolo do que para ele.
Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
21 Aquele que mima a seu servo desde a infância, por fim ele quererá ser [seu] filho.
Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
22 O homem que se irrita facilmente levanta brigas; e o furioso multiplica as transgressões.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
23 A arrogância do homem o abaterá; mas o humilde de espírito obterá honra.
Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
24 Aquele que reparte com o ladrão odeia sua [própria] alma; ele ouve maldições e não [o] denuncia.
Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
25 O temor do homem arma ciladas; mas o que confia no senhor ficará em segurança.
Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
26 Muitos buscam a face do governante; mas o julgamento de cada um [vem] do SENHOR.
Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
27 O justos odeiam ao homem perverso; e o injusto odeia aos que andam no caminho correto.
Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.

< Provérbios 29 >