< Provérbios 21 >

1 [Como] ribeiros de águas é o coração do rei na mão do SENHOR, ele o conduz para onde quer.
Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
2 Todo caminho do homem é correto aos seus [próprios] olhos; mas o SENHOR pesa os corações.
Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
3 Praticar justiça e juízo é mais aceitável ao SENHOR do que sacrifício.
Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
4 Olhos orgulhosos e coração arrogante: a lavoura dos perversos é pecado.
Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
5 Os planos de quem trabalha com empenho somente [levam] à abundância; mas [os de] todo apressado somente à pobreza.
Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
6 Trabalhar [para obter] tesouros com língua mentirosa é algo inútil [e] fácil de se perder; os que [assim fazem] buscam a morte.
Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
7 A violência [praticada] pelos perversos os destruirá, porque se negam a fazer o que é justo.
Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
8 O caminho do homem transgressor [é] problemático; porém a obra do puro é correta.
Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
9 É melhor morar num canto do terraço do que numa casa espaçosa com uma mulher briguenta.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
10 A alma do perverso deseja o mal; seu próximo não lhe agrada em seus olhos.
Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
11 Castigando ao zombador, o ingênuo se torna sábio; e ensinando ao sábio, ele ganha conhecimento.
Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
12 O justo considera prudentemente a casa do perverso; ele transtorna os perversos para a ruína.
Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
13 Quem tapa seu ouvido ao clamor do pobre, ele também clamará, mas não será ouvido.
Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
14 O presente em segredo extingue a ira; e a dádiva no colo [acalma] o forte furor.
Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
15 Alegria para o justo é fazer justiça; mas [isso é] pavor para os que praticam maldade.
Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
16 O homem que se afasta do caminho do entendimento repousará no ajuntamento dos mortos.
Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
17 Quem ama o prazer sofrerá necessidade; aquele que ama o vinho e o azeite nunca enriquecerá.
Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
18 O resgate [em troca] do justo é o perverso; e no lugar do reto [fica] o transgressor.
Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
19 É melhor morar em terra deserta do que com uma mulher briguenta e que se irrita facilmente.
Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
20 [Há] tesouro desejável e azeite na casa do sábio; mas o homem tolo é devorador.
Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
21 Quem segue a justiça e a bondade achará vida, justiça e honra.
Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
22 O sábio passa por cima da cidade dos fortes e derruba a fortaleza em que confiam.
Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
23 Quem guarda sua boca e sua língua guarda sua alma de angústias.
Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
24 “Zombador” é o nome do arrogante e orgulhoso; ele trata [os outros] com uma arrogância irritante.
Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
25 O desejo do preguiçoso o matará, porque suas mãos se recusam a trabalhar;
Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
26 Ele fica desejando suas cobiças o dia todo; mas o justo dá, e não deixa de dar.
Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
27 O sacrifício dos perversos é abominável; quanto mais quando a oferta é feita com má intenção.
Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
28 A testemunha mentirosa perecerá; porém o homem que ouve [a verdade] falará com sucesso.
Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
29 O homem perverso endurece seu rosto, mas o correto confirma o seu caminho.
Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
30 Não há sabedoria, nem entendimento, nem conselho contra o SENHOR.
Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
31 O cavalo é preparado para o dia da batalha, mas a vitória [vem] do SENHOR.
Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.

< Provérbios 21 >