< Provérbios 14 >

1 Toda mulher sábia edifica sua casa; porém a tola a derruba com suas mãos.
Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 Aquele que anda corretamente teme ao SENHOR; mas o que se desvia de seus caminhos o despreza.
Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
3 Na boca do tolo está a vara da arrogância, porém os lábios dos sábios os protegem.
Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
4 Não havendo bois, o celeiro fica limpo; mas pela força do boi há uma colheita abundante.
Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
5 A testemunha verdadeira não mentirá, mas a testemunha falsa declara mentiras.
Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
6 O zombador busca sabedoria, mas não [acha] nenhuma; mas o conhecimento é fácil para o prudente.
Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
7 Afasta-te do homem tolo, porque [nele] não encontrarás lábios inteligentes.
Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
8 A sabedoria do prudente é entender seu caminho; mas a loucura dos tolos é engano.
Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
9 Os tolos zombam da culpa, mas entre os corretos está o favor.
Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
10 O coração conhece sua [própria] amargura, e o estranho não pode partilhar sua alegria.
Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
11 A casa dos perversos será destruída, mas a tenda dos corretos florescerá.
Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
12 Há um caminho que [parece] correto para o homem, porém o fim dele são caminhos de morte.
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
13 Até no riso o coração terá dor, e o fim da alegria é a tristeza.
Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
14 Quem se desvia de coração será cheio de seus próprios caminhos, porém o homem de bem [será recompensado] pelos seus.
Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
15 O ingênuo crê em toda palavra, mas o prudente pensa cuidadosamente sobre seus passos.
Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
16 O sábio teme, e se afasta do mal; porém o tolo se precipita e se acha seguro.
Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
17 Quem se ira rapidamente faz loucuras, e o homem de maus pensamentos será odiado.
Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
18 Os ingênuos herdarão a tolice, mas os prudentes serão coroados [com] o conhecimento.
Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
19 Os maus se inclinarão perante a face dos bons, e os perversos diante das portas do justo.
Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
20 O pobre é odiado até pelo seu próximo, porém os amigos dos ricos são muitos.
Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
21 Quem despreza a seu próximo, peca; mas aquele que demonstra misericórdia aos humildes [é] bem-aventurado.
Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
22 Por acaso não andam errados os que tramam o mal? Mas [há] bondade e fidelidade para os que planejam o bem.
Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
23 Em todo trabalho cansativo há proveito, mas o falar dos lábios só [leva] à pobreza.
Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
24 A coroa dos sábios é a sua riqueza; a loucura dos tolos é loucura.
Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
25 A testemunha verdadeira livra almas, mas aquele que declara mentiras é enganador.
Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
26 No temor ao SENHOR [há] forte confiança; e será refúgio para seus filhos.
Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
27 O temor ao SENHOR é manancial de vida, para se desviar dos laços da morte.
Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
28 Na multidão do povo está a honra do rei, mas a falta de gente é a ruína do príncipe.
Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
29 Quem demora para se irar tem muito entendimento, mas aquele de espírito impetuoso exalta a loucura.
Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
30 O coração em paz é vida para o corpo, mas a inveja é [como] podridão nos ossos.
Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
31 Quem oprime ao pobre insulta ao seu Criador; mas aquele que mostra compaixão ao necessitado o honra.
Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
32 Por sua malícia, o perverso é excluído; porém o justo [até] em sua morte mantém a confiança.
Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
33 No coração do prudente repousa a sabedoria; mas ela será conhecida até entre os tolos.
Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
34 A justiça exalta a nação, mas o pecado é a desgraça dos povos.
Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
35 O rei se agrada do seu servo prudente; porém ele mostrará seu furor ao causador de vergonha.
Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.

< Provérbios 14 >