< Provérbios 12 >

1 Aquele que ama a correção ama o conhecimento; mas aquele que odeia a repreensão é um bruto.
Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
2 O homem de bem ganha o favor do SENHOR; mas ao homem de pensamentos perversos, ele o condenará.
Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
3 O homem não prevalecerá pela perversidade; mas a raiz dos justos não será removida.
Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
4 A mulher virtuosa é a coroa de seu marido; mas a causadora de vergonha é como uma podridão em seus ossos.
Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
5 Os pensamentos dos justos são de bom juízo; [mas] os conselhos dos perversos são enganosos.
Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
6 As palavras dos perversos são para espreitar [o derramamento de] sangue [de inocentes]; mas a boca dos corretos os livrará.
Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
7 Os perversos serão transtornados, e não existirão [mais]; porém a casa dos justos permanecerá.
Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
8 Cada um será elogiado conforme seu entendimento; mas o perverso de coração será desprezado.
Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
9 Melhor é o que estima pouco a si mesmo mas tem quem o sirva, do que aquele que elogia e si mesmo, mas nem sequer tem pão.
Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
10 O justo dá atenção à vida de seus animais; mas [até] as misericórdias dos perversos são cruéis.
Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
11 Aquele que lavra sua terra se saciará de pão; mas o que segue [coisas] inúteis tem falta de juízo.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
12 O perverso deseja armadilhas malignas; porém a raiz dos justos produzirá [seu fruto].
Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
13 O perverso é capturado pela transgressão de seus lábios, mas o justo sairá da angústia.
Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
14 Cada um se sacia do bem pelo fruto de sua [própria] boca; e a recompensa das mãos do homem lhe será entregue de volta.
Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
15 O caminho do tolo é correto aos seus [próprios] olhos; mas aquele que ouve o [bom] conselho é sábio.
Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
16 A ira do tolo é conhecida no mesmo dia, mas o prudente ignora o insulto.
Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
17 Aquele que fala a verdade conta a justiça; porém a testemunha falsa [conta] o engano.
Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
18 Há [alguns] que falam [palavras] como que golpes de espada; porém a língua do sábios é [como] um remédio.
Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
19 O lábio da verdade ficará para sempre, mas a língua da falsidade [dura] por [apenas] um momento.
Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
20 [Há] engano no coração dos que tramam o mal; mas os que aconselham a paz [têm] alegria.
Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
21 Nenhuma adversidade sobrevirá ao justos; mas os perversos se encherão de mal.
Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
22 Os lábios mentirosos são abomináveis ao SENHOR, mas dos que falam a verdade são seu prazer.
Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
23 O homem prudente é discreto em conhecimento; mas o coração dos tolos proclama a loucura.
Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
24 A mão dos que trabalham com empenho dominará, e os preguiçosos se tornarão escravos.
Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
25 A ansiedade no coração do homem o abate; [mas] uma boa palavra o alegra.
Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
26 O justo age cuidadosamente para com seu próximo, mas o caminho dos perversos os faz errar.
Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
27 O preguiçoso não assa aquilo que caçou, mas a riqueza de quem trabalha com empenho [lhe é] preciosa.
Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
28 Na vereda da justiça está a vida; e [no] caminho de seu percurso não há morte.
Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

< Provérbios 12 >