< Jó 40 >
1 Então o SENHOR respondeu mais a Jó, dizendo:
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 Por acaso quem briga contra o Todo-Poderoso pode ensiná-lo? Quem quer repreender a Deus, responda a isto.
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Então Jó respondeu ao SENHOR, dizendo:
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 Eis que eu sou insignificante; o que eu te responderia? Ponho minha mão sobre minha boca.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 Uma vez falei, porém não responderei; até duas vezes, porém não prosseguirei.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Então o SENHOR respondeu a Jó desde o redemoinho, dizendo:
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Cinge-te agora os teus lombos como homem; eu te perguntarei, e tu me explica.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Por acaso tu anularias o meu juízo? Tu me condenarias, para te justificares?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 Tens tu braço como Deus? Ou podes tu trovejar com [tua] voz como ele?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Orna-te, pois, de excelência e alteza; e veste-te de majestade e glória.
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Espalha os furores de tua ira; olha a todo soberbo, e abate-o.
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Olha a todo soberbo, e humilha-o; e esmaga aos perversos em seu lugar.
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Esconde-os juntamente no pó; ata seus rostos no oculto.
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 E eu também te reconhecerei; pois tua mão direita te terá livrado.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Observa o beemote, ao qual eu fiz contigo; ele come erva come como o boi.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 Eis que sua força está em seus lombos, e seu poder na musculatura de seu ventre.
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 Ele torna sua cauda dura como o cedro, e os nervos de suas coxas são entretecidos.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 Seus ossos são [como] tubos de bronze; seus membros, como barras de ferro.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 Ele é a obra-prima dos caminhos de Deus; aquele que o fez o proveu de sua espada.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 Pois os montes lhe produzem pasto; por isso todos os animais do campo ali se alegram.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 Ele se deita debaixo das árvores sombrias; no esconderijo das canas e da lama.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 As árvores sombrias o cobrem, cada uma com sua sombra; os salgueiros do ribeiro o cercam.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Ainda que o rio se torne violento, ele não se apressa; confia ainda que o Jordão transborde até sua boca.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 Poderiam, por acaso, capturá-lo à vista de seus olhos, [ou] com laços furar suas narinas?
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?