< 38 >

1 Então o SENHOR respondeu a Jó desde um redemoinho, e disse:
Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
2 Quem é esse que obscurece o conselho com palavras sem conhecimento?
“Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
3 Agora cinge teus lombos como homem; e eu te perguntarei, e tu me explicarás.
Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
4 Onde estavas tu quando eu fundava a terra? Declara- [me], se tens inteligência.
Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
5 Quem determinou suas medidas, se tu o sabes? Ou quem estendeu cordel sobre ela?
Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
6 Sobre o que estão fundadas suas bases? Ou quem pôs sua pedra angular,
Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
7 Quando as estrelas do amanhecer cantavam alegremente juntas, e todos os filhos de Deus jubilavam?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
8 Ou [quem] encerrou o mar com portas, quando transbordou, saindo da madre,
Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
9 Quando eu pus nuvens por sua vestidura, e a escuridão por sua faixa;
wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
10 Quando eu passei sobre ele meu decreto, e [lhe] pus portas e ferrolhos,
Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
11 E disse: Até aqui virás, e não passarás adiante, e aqui será o limite para a soberba de tuas ondas?
na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
12 Desde os teus dias tens dado ordem à madrugada? [Ou] mostraste tu ao amanhecer o seu lugar,
Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
13 Para que tomasse os confins da terra, e os perversos fossem sacudidos dela?
ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
14 E [a terra] se transforma como barro [sob] o selo; [todas as coisas sobre ela] se apresentam como vestidos?
Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
15 E dos perversos é desviada sua luz, e o braço erguido é quebrado.
'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
16 Por acaso chegaste tu às fontes do mar, ou passeaste no mais profundo abismo?
Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
17 Foram reveladas a ti as portas da morte, ou viste as portas da sombra de morte?
Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
18 Entendeste tu as larguras da terra? Declara, se sabes tudo isto.
Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
19 Onde está o caminho [por onde] mora a luz? E quanto às trevas, onde fica o seu lugar?
Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
20 Para que as tragas a seus limites, e conheças os caminhos de sua casa.
Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
21 Certamente tu o sabes, pois já eras nascido, e teus dias são inúmeros!
Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
22 Por acaso entraste tu aos depósitos da neve, e viste os depósitos do granizo,
Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
23 Que eu retenho até o tempo da angústia, até o dia da batalha e da guerra?
vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
24 Onde está o caminho em que a luz se reparte, e o vento oriental se dispersa sobre a terra?
Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
25 Quem repartiu um canal às correntezas de águas, e caminho aos relâmpagos dos trovões,
Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
26 Para chover sobre a terra [onde] havia ninguém, [sobre] o deserto, onde não há gente,
na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
27 Para fartar [a terra] deserta e desolada, e para fazer crescer aos renovos da erva.
kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
28 Por acaso a chuva tem pai? Ou quem gera as gotas do orvalho?
Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
29 De qual ventre procede o gelo? E quem gera a geada do céu?
Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
30 As águas se tornam duras como pedra, e a superfície do abismo se congela.
Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
31 Podes tu atar as cadeias das Plêiades, ou desatar as cordas do Órion?
Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
32 Podes tu trazer as constelações a seu tempo, e guiar a Ursa com seus filhos?
Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
33 Sabes tu as ordenanças dos céus? Ou podes tu dispor do domínio deles sobre a terra?
Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
34 Ou podes levantar tua voz até às nuvens, para que a abundância das águas te cubra?
Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
35 Podes tu mandar relâmpagos, para que saiam, e te digam: Eis-nos aqui?
Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
36 Quem pôs a sabedoria no íntimo? Ou quem deu entendimento à mente?
Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
37 Quem pode enumerar as nuvens com sabedoria? E os odres dos céus, quem pode os despejar?
Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
38 Quando o pó se endurece, e os torrões se apegam uns aos outros?
wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
39 Caçarás tu a presa para o leão? Ou saciarás a fome dos leões jovens,
Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
40 Quando estão agachados nas covas, [ou] estão à espreita no matagal?
wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
41 Quem prepara aos corvos seu alimento, quando seus filhotes clamam a Deus, andando de um lado para o outro por não terem o que comer?
Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?

< 38 >