< 31 >

1 Eu fiz um pacto com meus olhos; como, pois, eu olharia com cobiça para a virgem?
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
2 Pois qual é a porção [dada] por Deus acima, e a herança [dada] pelo Todo-Poderoso das alturas?
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
3 Por acaso a calamidade não é para o perverso, e o desastre para os que praticam injustiça?
Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
4 Por acaso ele não vê meus caminhos, e conta todos os meus passos?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
5 Se eu andei com falsidade, e se meu pé se apressou para o engano,
“Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
6 Pese-me ele em balanças justas, e Deus saberá minha integridade.
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
7 Se meus passos se desviaram do caminho, e meu coração seguiu meus olhos, e se algo se apegou às minhas mãos,
kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
8 Que eu semeie, e outro coma; e meus produtos sejam arrancados.
basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
9 Se foi meu coração se deixou seduzir por [alguma] mulher, ou se estive espreitei à porta de meu próximo,
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
10 Que minha mulher moa para outro, e outros se encurvem sobre ela.
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
11 Pois tal seria um crime vergonhoso, e delito [a ser sentenciado por] juízes.
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
12 Pois seria um fogo que consumiria até à perdição, e destruiria toda a minha renda.
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
13 Se desprezei o direito de meu servo ou de minha serva quando eles reclamaram comigo,
“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
14 Que faria eu quando Deus se levantasse? E quando ele investigasse [a causa], o que eu lhe responderia?
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
15 Aquele que me fez no ventre [materno também] não fez a ele? E não nos preparou de um mesmo [modo] na madre?
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
16 Se eu neguei aos pobres o que eles desejavam, ou fiz desfalecer os olhos da viúva;
“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
17 E se comi meu alimento sozinho, e o órfão não comeu dele
kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
18 (Porque desde a minha juventude cresceu comigo como [se eu fosse seu pai], e desde o ventre de minha mãe guiei [a viúva] );
lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
19 Se eu vi alguém morrer por falta de roupa, e o necessitado sem algo que o cobrisse,
kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
20 Se sua cintura não me bendisse, quando ele se esquentava com as peles de meus cordeiros;
ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
21 Se levantei minha mão contra o órfão, quando vi que seria favorecido na corte judicial,
na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
22 Que minha escápula caia do meu ombro, e meu braço se quebre de sua articulação.
basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
23 Porque o castigo de Deus era um assombro para mim, e eu não teria poder contra sua majestade.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
24 Se eu pus no ouro minha esperança, ou disse ao ouro fino: Tu és minha confiança;
“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
25 Se eu me alegrei de que minha riqueza era muita, e de que minha mão havia obtido muito;
kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
26 Se olhei para o sol quando brilhava, e à lua quando estava bela,
kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
27 E meu coração se deixou enganar em segredo, e minha boca beijou minha mão,
hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
28 Isto também seria um delito [a ser sentenciado por] juiz; porque teria negado ao Deus de cima.
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
29 Se eu me alegrei da desgraça daquele que me odiava, e me agradei quando o mal o encontrou,
“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
30 Sendo que nem deixei minha boca pecar, desejando sua morte com maldição,
lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
31 Se a gente da minha casa nunca tivesse dito: Quem não se satisfez da carne dada por ele?
kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
32 O estrangeiro não passava a noite na rua; eu abria minhas portas ao viajante.
Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
33 Se encobri minhas transgressões como as pessoas [fazem], escondendo meu delito em meu seio;
kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
34 Porque eu tinha medo da grande multidão, e o desprezo das famílias me atemorizou; então me calei, e não saí da porta:
kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
35 Quem me dera se alguém me ouvisse! Eis que minha vontade é que o Todo-Poderoso me responda, e meu adversário escrevesse um relato da acusação.
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
36 Certamente eu o carregaria sobre meu ombro, e o poria em mim como uma coroa.
Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
37 Eu lhe diria o número de meus passos, e como um príncipe eu me chegaria a ele.
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
38 Se minha terra clamar contra mim, e seus sulcos juntamente chorarem;
“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
39 Se comi seus frutos sem [pagar] dinheiro, ou fiz expirar a alma de seus donos;
kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
40 Em lugar de trigo que [me] produza cardos, e ervas daninhas no lugar da cevada. [Aqui] terminam as palavras de Jó.
basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.

< 31 >