< 30 >

1 Porém agora riem de mim os mais jovens do que eu, cujos pais eu havia desdenhado até de os pôr com os cães de meu rebanho.
“Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
2 De que também me serviria força de suas mãos, nos quais o vigor já pereceu?
Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3 Por causa da pobreza e da fome andavam sós; roem na terra seca, no lugar desolado e deserto em trevas.
Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
4 Que colhiam malvas entre os arbustos, e seu alimento eram as raízes dos zimbros.
Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
5 Do meio [das pessoas] eram expulsos, e gritavam contra eles, como a um ladrão.
Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
6 Habitavam nos barrancos dos ribeiros secos, nos buracos da terra, e nas rochas.
Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
7 Bramavam entre os arbustos, e se ajuntavam debaixo das urtigas.
Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
8 Eram filhos de tolos, filhos sem nome, e expulsos de [sua] terra.
Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
9 Porém agora sirvo-lhes de chacota, e sou para eles um provérbio de escárnio.
“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10 Eles me abominam [e] se afastam de mim; porém não hesitam em cuspir no meu rosto.
Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11 Pois [Deus] desatou minha corda, e me oprimiu; por isso tiraram [de si] todo constrangimento perante meu rosto.
Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
12 À direita os jovens se levantam; empurram meus pés, e preparam contra mim seus caminhos de destruição.
Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13 Destroem meu caminho, e promovem minha miséria, sem necessitarem que alguém os ajude.
Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14 Eles vêm [contra mim] como que por uma brecha larga, [e] revolvem-se entre a desolação.
Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15 Pavores se voltam contra mim; perseguem minha honra como o vento, e como nuvem passou minha prosperidade.
Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
16 Por isso agora minha alma se derrama em mim; dias de aflição têm me tomado.
“Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
17 De noite meus ossos se furam em mim, e meus pulsos não descansam.
Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18 Por grande força [de Deus] minha roupa está estragada; ele me prendeu como a gola de minha roupa.
Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19 Lançou-me na lama, e fiquei semelhante ao pó e à cinza.
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20 Clamo a ti, porém tu não me respondes; eu fico de pé, porém tu ficas [apenas] olhando para mim.
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21 Tu te tornaste cruel para comigo; com a força de tua mão tu me atacas.
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22 Levantas-me sobre o vento, [e] me fazes cavalgar [sobre ele]; e dissolves o meu ser.
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23 Porque eu sei que me levarás à morte; e à casa determinada a todos os viventes.
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24 Porém não se estende a mão para quem está em ruínas, quando clamam em sua opressão?
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
25 Por acaso eu não chorei pelo que estava em dificuldade, [e] minha alma não se angustiou pelo necessitado?
Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
26 Quando eu esperava o bem, então veio o mal; quando eu esperava a luz, veio a escuridão.
Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27 Minhas entranhas fervem, e não se aquietam; dias de aflição me confrontam.
Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28 Ando escurecido, mas não pelo sol; levanto-me na congregação, e clamo por socorro.
Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29 Tornei-me irmão dos chacais, e companheiro dos avestruzes.
Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30 Minha pele se escureceu sobre mim, e meus ossos se inflamam de febre.
Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
31 Por isso minha harpa passou a ser para lamentação, e minha flauta para vozes dos que choram.
Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.

< 30 >