< 1 Crônicas 6 >
1 Os filhos de Levi foram: Gérson, Coate, e Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
2 Os filhos de Coate: Anrão, Izar, Hebrom e Uziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
3 Os filhos de Anrão: Arão, Moisés, e Miriã. E os filhos de Arão foram: Nadabe, Abiú, Eleazar, e Itamar.
Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
4 E Eleazar gerou a Fineias, Fineias gerou a Abisua;
Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
5 Abisua gerou a Buqui, Buqui gerou a Uzi;
Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
6 Uzi gerou a Zeraías, Zeraías gerou a Meraiote;
Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
7 Meraiote gerou a Amarias, Amarias gerou a Aitube;
Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
8 Aitube gerou a Zadoque, Zadoque gerou a Aimaaz;
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
9 Aimaaz gerou a Azarias, Azarias gerou a Joanã;
Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
10 Joanã gerou a Azarias (este é o que administrou o sacerdócio na casa que Salomão edificou em Jerusalém);
Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
11 Azarias gerou a Amarias, Amarias gerou a Aitube;
Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
12 Aitube gerou a Zadoque, Zadoque gerou a Salum;
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
13 Salum gerou a Hilquias, Hilquias gerou a Azarias;
Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
14 Azarias gerou a Seraías, Seraías, gerou a Jeozadaque.
Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
15 E Jeozadaque foi [levado cativo] quando O SENHOR levou Judá e a Jerusalém como prisioneiros, pela mão de Nabucodonosor.
Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
16 Os filhos de Levi foram: Gérson, Coate, e Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
17 E estes são os nomes dos filhos de Gérson: Libni, e Simei.
Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
18 Os filhos de Coate: Anrão, Izar, Hebrom, e Uziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
19 Os filhos de Merari: Mali, e Musi. Estas são as famílias de Levi, segundo seus pais.
Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
20 De Gérson: seu filho Libni, seu filho Jaate, seu filho Zima.
Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
21 Seu filho Joabe, seu filho Ido, seu filho Zerá, e seu filho Jeaterai.
Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
22 Os filhos de Coate foram: seu filho Aminadabe, seu filho Corá, seu filho Assir,
Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
23 Seu filho Elcana, seu filho Ebiasafe, seu filho Assir,
Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
24 Seu filho Taate, seu filho Uriel, seu filho Uzias, e seu filho Saul.
Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
25 E os filhos Elcana foram: Amasai e Aimote.
Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
26 [Quanto] a Elcana, os filhos de Elcana foram: seu filho Zofai, seu filho Naate,
Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
27 Seu filho Eliabe, seu filho Jeroão, e seu filho Elcana.
Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
28 E os filhos de Samuel foram: o primogênito Vasni, e Abias.
Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
29 Os filhos de Merari: Mali, seu filho Libni, seu filho Simei, seu filho Uzá,
Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
30 Seu filho Simeia, seu filho Hagias, e seu filho Asaías.
Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
31 Estes, pois, são os que Davi constituiu para o ofício da música da casa do Senhor, depois que a arca teve repouso.
Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
32 E eles serviam diante da tenda do tabernáculo da congregação com cânticos, até que Salomão edificou a casa do SENHOR em Jerusalém; e estiveram segundo seu costume em seu serviço.
Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
33 Estes, pois, foram os que ali estavam com seus filhos: dos filhos dos coatitas, Hemã, o cantor, filho de Joel, filho de Samuel,
Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
34 Filho de Elcana, filho de Jeroão, filho de Eliel, filho de Toá,
Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
35 Filho de Zufe, filho de Elcana, filho Maate, filho de Amasai,
Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
36 Filho de Elcana, filho de Joel, filho de Azarias, filho de Sofonias,
Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
37 Filho de Taate, filho de Assir, filho de Ebiasafe, filho de Corá,
Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
38 Filho de Izar, filho de Coate, filho de Levi, filho de Israel.
Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
39 E seu irmão Asafe estava à sua direita; Asafe era, filho de Berequias, filho de Simeia,
Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
40 Filho de Micael, filho de Baaseias, filho de Malquias,
Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
41 Filho de Etni, filho de Zerá, filho de Adaías,
Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
42 Filho de Etã, filho de Zima, filho de Simei;
Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
43 Filho de Jaate, filho de Gérson, filho de Levi.
Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
44 E seus irmãos, os filhos de Merari, estavam à esquerda; [eram eles]: Etã, filho de Quisi, filho de Abdi, filho de Maluque,
Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
45 Filho de Hasabias, filho de Amazias, filho de Hilquias,
Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
46 Filho de Anzi, filho de Bani, filho de Semer,
Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
47 Filho de Mali, filho de Musi, filho de Merari, filho de Levi.
Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
48 E seus irmãos, os Levitas, foram postos para todo o serviço do tabernáculo da casa de Deus.
Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
49 E Arão e seus filhos ofereciam incenso sobre o altar do holocausto e sobre o altar do incenso, para toda a obra do lugar santíssimo, e para fazer expiação sobre Israel, conforme tudo quanto Moisés, servo de Deus, havia mandado.
Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
50 E estes foram os filhos de Arão: seu filho Eleazar, seu filho Fineias, seu filho Abisua,
Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
51 Seu filho Buqui, seu filho Uzi, seu filho Zeraías,
Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
52 Seu filho Meraiote, seu filho Amarias, seu filho Aitube,
Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
53 Seu filho Zadoque, e seu filho Aimaaz.
Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
54 E estas foram suas habitações, conforme seus acampamentos e seus termos, dos filhos de Arão da família dos coatitas, porque eles foram sorteados.
Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
55 Deram-lhes, pois, a Hebrom na terra de Judá, e seus campos ao redor dela.
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
56 Porém o território da cidade e suas aldeias foram dadas a Calebe, filho de Jefoné.
lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 E aos filhos de Arão deram as [seguintes] cidades de refúgio: Hebrom, e Libna com seus campos; Jathir e Estemoa com seus campos;
Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
58 Hilém com seus campos; Debir com seus campos;
Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
59 Asã com seus campos; e a Bete-Semes com seus campos;
Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
60 E da tribo de Benjamim, a Geba com seus campos; Alemete com seus campos; e Anatote com seus campos. Todas as suas cidades, [repartidas] por suas famílias, foram treze cidades.
na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
61 Mas aos filhos de Coate, que restaram da família daquela tribo, [deram] por sorteio dez cidades da meia tribo de Manassés.
Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
62 E aos filhos de Gérson, segundo suas famílias, [deram] treze cidades da tribo de Issacar, da tribo de Aser, da tribo de Naftali, e da tribo de Manassés, em Basã.
Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 E aos filhos de Merari, segundo suas famílias, [deram] por sorteio doze cidades da tribo de Rúben, da tribo de Gade, e da tribo de Zebulom.
Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
64 Assim os filhos de Israel deram aos Levitas estas cidades com seus campos.
Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
65 E deram-lhes por sorteio, da tribo dos filhos de Judá, da tribo dos filhos de Simeão, e da tribo dos filhos de Benjamim, estas cidades, as quais mencionaram por seus nomes.
Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
66 E quanto ao [resto] das famílias dos filhos de Coate deram-lhes cidades com seus termos da tribo de Efraim.
Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
67 E deram-lhes das cidades de refúgio, a Siquém e seus campos nas montanhas de Efraim, e a Gezer com seus campos,
Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
68 A Jocmeão com seus campos, a Bete-Horom com seus campos,
Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
69 A Aijalom com seus campos, e a Gate-Rimom com seus campos;
Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
70 Da meia tribo de Manassés, a Aner com seus campos, e a Bileã com seus campos, para os que restaram da família dos filhos de Coate.
Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
71 Aos filhos de Gérson [deram] da família da meia tribo de Manassés, a Golã em Basã com seus campos e a Astarote com seus campos;
Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
72 E da tribo de Issacar, a Quedes com seus campos, a Daberate com seus campos,
Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
73 A Ramote com seus campos, e a Aném com seus campos;
Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
74 E da tribo de Aser a Masal com seus campos, a Abdom com seus campos,
Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
75 A Hucoque com seus campos, e a Reobe com seus campos.
Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
76 E da tribo de Naftali, a Quedes na Galileia com seus campos, a Hamom com seus campos, e a Quiriataim com seus campos.
Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
77 E aos que restaram dos filhos de Merari, [deram] da tribo de Zebulom, a Rimono com seus campos, e a Tabor com seus campos;
Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
78 E dalém do Jordão de Jericó, ao oriente do Jordão, [deram] da tribo de Rúben, a Bezer no deserto com seus campos; a Jaza com seus campos.
Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
79 A Quedemote com seus campos, e a Mefaate com seus campos;
Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
80 E da tribo de Gade, a Ramote em Gileade com seus campos, a Maanaim com seus campos,
Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
81 A Hesbom com seus campos, e a Jazer com seus campos.
Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.