< Salmos 107 >

1 Louvai ao Senhor, porque ele é bom, porque a sua benignidade dura para sempre.
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 Digam-no os remidos do Senhor, os que remiu da mão do inimigo,
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 E os que congregou das terras do oriente e do ocidente, do norte e do sul.
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Andaram desgarrados pelo deserto, por caminhos solitários; não acharam cidade para habitarem.
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 Famintos e sedentos, a sua alma neles desfalecia.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 E clamaram ao Senhor na sua angústia, e os livrou das suas necessidades.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 E os levou por caminho direito, para irem a uma cidade de habitação.
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 Louvem ao Senhor pela sua bondade, e pelas suas maravilhas para com os filhos dos homens.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 Pois fartou a alma sedenta, e encheu de bondade a alma faminta.
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 Tal como a que se assenta nas trevas e sombra da morte, presa em aflição e em ferro;
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 Porquanto se rebelaram contra as palavras de Deus, e desprezaram o conselho do altíssimo,
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 Portanto lhes abateu o coração com trabalho; tropeçaram, e não houve quem os ajudasse.
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 Então clamaram ao Senhor na sua angústia, e os livrou das suas necessidades.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 Tirou-os das trevas e sombra da morte; e quebrou as suas prisões.
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 Louvem ao Senhor pela sua bondade, e pelas suas maravilhas para com os filhos dos homens.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 Pois quebrou as portas de bronze; e despedaçou os ferrolhos de ferro.
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Os loucos, por causa da sua transgressão, e por causa das suas iniquidades, são aflitos.
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 A sua alma aborreceu toda a comida, e chegaram até às portas da morte.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 Então clamaram ao Senhor na sua angústia: e ele os livrou das suas necessidades.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 Enviou a sua palavra, e os sarou; e os livrou da sua destruição.
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 Louvem ao Senhor pela sua bondade, e pelas suas maravilhas para com os filhos dos homens.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 E ofereçam os sacrifícios de louvor, e relatem as suas obras com regozijo.
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 Os que descem ao mar em navios, mercando nas grandes águas,
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 Esses veem as obras do Senhor, e as suas maravilhas no profundo.
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 Pois ele manda, e se levanta o vento tempestuoso, que eleva as suas ondas.
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 Sobem aos céus; descem aos abismos, e a sua alma se derrete em angústias.
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 Andam e cambaleam como ébrios, e perderam todo o tino.
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 Então clamam ao Senhor na sua angústia; e ele os livra das suas necessidades.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 Faz cessar a tormenta, e calam-se as suas ondas.
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 Então se alegram, porque se aquietaram; assim os leva ao seu porto desejado.
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 Louvem ao Senhor pela sua bondade, e pelas suas maravilhas para com os filhos dos homens.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 Exaltem-no na congregação do povo, e glorifiquem-no na assembléia dos anciãos.
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 Ele converte os rios em um deserto, e as fontes em terra sedenta:
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 A terra frutífera em estéril, pela maldade dos que nela habitam.
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 Converte o deserto em lagoa, e a terra seca em fontes.
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 E faz habitar ali os famintos, para que edifiquem cidade para habitação;
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 E semeiam os campos e plantam vinhas, que produzem fruto abundante.
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 Também os abençoa, de modo que se multiplicam muito; e o seu gado não diminui.
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 Depois se diminuem e se abatem, pela opressão, aflição e tristeza.
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 Derrama o desprezo sobre os príncipes, e os faz andar desgarrados pelo deserto, onde não há caminho.
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 Porém livra ao necessitado da opressão em um lugar alto, e multiplica as famílias como rebanhos.
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 Os retos o verão, e se alegrarão, e toda a iniquidade tapará a boca.
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 Quem é sábio observará estas coisas, e eles compreenderão as benignidades do Senhor.
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.

< Salmos 107 >