< Salmos 1 >

1 Bem-aventurado o varão que não anda no conselho dos ímpios, nem está no caminho dos pecadores, nem se assenta no assento dos escarnecedores.
Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 Antes tem o seu prazer na lei do Senhor, e na sua lei medita de dia e de noite.
Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 Pois será como a árvore plantada junto a ribeiros de águas, que dá o seu fruto no seu tempo; as suas folhas não cairão, e tudo quanto fizer prosperará.
Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
4 Não são assim os ímpios: mas são como a moinha que o vento espalha.
Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 Pelo que os ímpios não subsistirão no juízo, nem os pecadores na congregação dos justos.
Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 Porque o Senhor conhece o caminho dos justos; porém o caminho dos ímpios perecerá.
Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.

< Salmos 1 >