< Provérbios 11 >

1 Balança enganosa é abominação ao Senhor, mas o peso justo o seu prazer.
Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
2 Vinda a soberba, virá também a afronta; mas com os humildes está a sabedoria.
Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
3 A sinceridade dos sinceros os encaminhará, mas a perversidade dos aleives os destruirá.
Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
4 Não aproveitam as riquezas no dia da indignação, mas a justiça livra da morte.
Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
5 A justiça do sincero endireitará o seu caminho, mas o ímpio pela sua impiedade cairá.
Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
6 A justiça dos virtuosos os livrará, mas na sua perversidade serão apanhados os iníquos.
Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
7 Morrendo o homem ímpio perece a sua expectação, e a esperança dos injustos se perde.
Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
8 O justo é livre da angústia, e o ímpio vem em seu lugar.
Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
9 O hipócrita com a boca destrói ao seu companheiro, mas os justos são livres pelo conhecimento.
Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
10 No bem dos justos exulta a cidade; e, perecendo os ímpios, há júbilo.
Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
11 Pela benção dos sinceros se exalta a cidade, mas pela boca dos ímpios se derriba.
Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
12 O que carece de entendimento despreza a seu companheiro, mas o homem bem entendido cala-se.
Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
13 O que anda praguejando descobre o segredo, mas o fiel de espírito encobre o negócio.
Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
14 Não havendo sábios conselhos, o povo cai, mas na multidão de conselheiros há segurança.
Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
15 Decerto sofrerá severamente aquele que fica por fiador do estranho, mas o que aborrece aos que dão as mãos estará seguro.
Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
16 A mulher aprazível guarda a honra, como os violentos guardam as riquezas.
Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
17 O homem benigno faz bem à sua própria alma, mas o cruel perturba a sua própria carne.
Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
18 O ímpio faz obra falsa, mas para o que semeia justiça haverá galardão fiel.
Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
19 Como a justiça encaminha para a vida, assim o que segue o mal vai para a sua morte.
Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
20 Abominação são ao Senhor os perversos de coração, mas os sinceros de caminho são o seu deleite.
Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
21 Ainda que o mau junte mão à mão, não será inculpável, mas a semente dos justos escapará.
Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
22 Como jóia de ouro na tromba da porca, assim é a mulher formosa, que se aparta da razão.
Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
23 O desejo dos justos tão somente é o bem, mas a esperança dos ímpios é a indignação.
Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
24 Alguns há que espalham, e ainda se lhes acrescenta mais, e outros que reteem mais do que é justo, mas é para a sua perda.
Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
25 A alma abençoante engordará, e o que regar, ele também será regado.
Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
26 Ao que retém o trigo o povo amaldiçoa, mas benção haverá sobre a cabeça do vendedor:
Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
27 O que busca cedo o bem busca favor, porém o que procura o mal a esse lhe sobrevirá.
Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
28 Aquele que confia nas suas riquezas cairá, mas os justos reverdecerão como a rama.
Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
29 O que perturba a sua casa herdará o vento, e o tolo será servo do entendido de coração.
Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
30 O fruto do justo é árvore de vida, e o que ganha almas sábio é.
Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
31 Eis que o justo é recompensado na terra; quanto mais o será o ímpio e o pecador.
Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?

< Provérbios 11 >