< João 9 >

1 E, passando Jesus, viu um homem cego de nascença.
Wakati, kama Yesu alipokuwa akipita, alimwona mtu kipofu tangu kuzaliwa kwake.
2 E os seus discípulos lhe perguntaram, dizendo: rabi, quem pecou, este ou seus pais, para que nascesse cego?
Wanafunzi wake wakamwuliza, “Rabi, nani aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi wake, hata azaliwe kipofu?”
3 Jesus respondeu: Nem ele pecou nem seus pais; mas foi para que se manifestem nele as obras de Deus.
Yesu akawajibu, “Siyo huyu mtu wala wazazi wake waliotenda dhambi, bali kazi za Mungu zipate kufunuliwa kupitia kwake.
4 Convém que eu faça as obras daquele que me enviou, enquanto é dia: a noite vem, quando ninguém pode trabalhar.
Tunapaswa kufanya kazi zake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana. Usiku waja wakati ambapo hakuna atakayeweza kufanya kazi.
5 Enquanto estou no mundo, sou a luz do mundo.
Wakati niwapo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”
6 Tendo dito isto, cuspiu na terra, e com o cuspo fez lodo, e untou com o lodo os olhos do cego.
Baada ya Yesu kusema maneno haya, alitema kwenye ardhi, alifanya tope kwa mate, na akampaka yule mtu machoni na lile tope.
7 E disse-lhe: vai, lava-te no tanque de Siloé (que significa o Enviado). Foi pois, e lavou-se, e voltou vendo.
Akamwambia, nenda kaoge katika kisima cha Siloam (Inayotafsiriwa kama 'aliyetumwa').” Kwa hiyo huyo mtu alienda, akanawa, na akarudi, anaona.
8 Então os vizinhos, e aqueles que de antes tinham visto que era cego, diziam: Não é este aquele que estava assentado e mendigava?
Majirani wa yule mtu na wale waliomuona mwanzo kama mwombaji walisema, Je! huyu siye yule mtu aliyekuwa akikaa na kuomba?” wengine walisema, “Ni yeye.”
9 Uns diziam: É este. E outros: Parece-se com ele. ele dizia: Eu sou.
Na wengine walisema, “Hapana, bali anafanana naye.” Lakini alikuwa akisema, “Ni mimi.”
10 Diziam-lhe pois: Como se te abriram os olhos?
Wakamwambia, “Sasa macho yako yalifunguliwaje?”
11 Ele respondeu, e disse: O homem, chamado Jesus, fez lodo, e untou-me os olhos, e disse-me: vai ao tanque de Siloé, e lava-te. E fui, e lavei-me, e vi.
Alijibu, mtu aitwaye Yesu alifanya tope na kupaka macho yangu na kuniambia, 'Nenda Siloam ukanawe.' Kwa hiyo nilienda, na nikanawa, na nikapata kuona tena.”
12 Disseram-lhe pois: Onde está ele? ele disse: Não sei.
Wakamwambia, “Yuko wapi?” Alijibu, “Sijui.”
13 Levaram pois aos fariseus o que de antes era cego.
Wakampeleka yule mtu aliyewahi kuwa kipofu kwa Mafarisayo.
14 E era sábado, quando Jesus fez o lodo e lhe abriu os olhos.
Nayo ilikuwa siku ya Sabato wakati Yesu alipotengeneza tope na kuyafumbua macho yake.
15 Tornaram pois também os fariseus a perguntar-lhe como vira, e ele lhes disse: pôs-me lodo sobre os olhos, lavei-me, e vejo.
Ndipo tena Mafarisayo wakamwuliza alipataje kuona. Aliwaambia, “Aliweka tope katika macho yangu, nikanawa, na sasa naweza kuona.”
16 Por isso alguns dos fariseus diziam: Este homem não é de Deus; pois não guarda o sábado. Diziam outros: Como pode um homem pecador fazer tais sinais? E havia dissensão entre eles.
Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Mtu huyu hajatoka kwa Mungu kwa sababu haishiki Sabato.” Wengine walisema, “Inawezekanaje mtu mwenye dhambi kufanya ishara kama hizo?” Kwa hiyo kukawa na mgawanyiko kati yao.
17 Tornaram pois a dizer ao cego: Tu que dizes daquele que te abriu os olhos? E ele disse: Que é profeta.
Ndipo walipomwuliza yule kipofu tena, “Unasemaje juu yake kwa sababu aliyafungua macho yako?” Kipofu akasema, “Ni nabii.”
18 Os judeus, porém, não creram que ele tivesse sido cego, e que agora visse, enquanto não chamaram os pais do que agora via.
Hata wakati huu Wayahudi hawakumwamini kwamba alikuwa kipofu naye amepata kuona mpaka walipowaita wazazi wake yeye aliyepata kuona.
19 E perguntaram-lhes, dizendo: É este o vosso filho, que vós dizeis ter nascido cego? Como pois vê agora?
Waliwauliza wazazi, Je, huyu ni mtoto wenu mnayesema alizaliwa kipofu? amewezaje sasa kuona?”
20 Seus pais lhes responderam, e disseram: Sabemos que este é nosso filho, e que nasceu cego;
Hivyo wazazi wake wakamjibu, “Tunajua kuwa huyu ni mtoto wetu na kwamba alizaliwa kipofu.
21 Mas como agora vê, não sabemos; ou quem lhe tenha aberto os olhos, não sabemos: tem idade, perguntai-lho a ele mesmo; e ele falará por si mesmo.
Jinsi gani sasa anaona, hatujui, na yeye aliyemfumbua macho yake, hatumjui. Mwulizeni yeye. Ni mtu mzima. Anaweza kujieleza mwenyewe.”
22 Seus pais disseram isto, porque temiam os judeus. Porquanto já os judeus tinham resolvido que, se alguém confessasse ser ele o Cristo, fosse expulso da sinagoga.
Wazazi wake walisema mambo haya, kwa sababu waliwaogopa Wayahudi. Kwa vile Wayahudi walikuwa wamekubaliana tayari kuwa, ikiwa yeyote atakiri kuwa Yesu ni Kristo, atatengwa na Sinagogi.
23 Por isso é que seus pais disseram: Tem idade, perguntai-lho a ele mesmo.
Kwa sababu hii, wazazi wake walisema, “Ni mtu mzima, mwulizeni yeye.”
24 Chamaram pois segunda vez o homem que tinha sido cego, e disseram-lhe: Dá glória a Deus; nós sabemos que esse homem é pecador.
Kwa hiyo kwa mara ya pili, walimwita yule mtu aliyewahi kuwa kipofu na kumwambia, “Mpe Mungu utukufu. Tunajua kwamba mtu huyu ni mwenye dhambi.”
25 Respondeu ele pois, e disse: Se é pecador, não sei: uma coisa sei, que, havendo eu sido cego, agora vejo.
Ndipo yule mtu alijibu, “Awe ni mwenye dhambi, mimi sijui. Kitu kimoja ninachokijua: nilikuwa kipofu, na sasa ninaona.”
26 E tornaram a dizer-lhe: Que te fez ele? Como te abriu os olhos?
Ndipo walipomwambia, “Amekufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?”
27 Respondeu-lhes: Já vo-lo disse, e não ouvistes: para que o quereis tornar a ouvir? Quereis vós porventura fazer-vos também seus discípulos?
Alijibu, “Nimekwishawaambia tayari, na nyinyi hamkusikiliza! Kwa nini mnataka kusikia tena? Nanyi hamtaki kuwa wanafunzi wake pia, sivyo?
28 Então o injuriaram, e disseram: discípulo dele sejas tu: nós, porém, somos discípulos de Moisés.
Walimtukana na kusema, “Wewe ni mwanafunzi wake, lakini sisi ni wanafunzi wa Musa.
29 Nós bem sabemos que Deus falou a Moisés, mas este não sabemos de onde é.
Tunajua kwamba Mungu alizungumza na Musa, lakini kwa huyu mtu, hatujui kule atokako.”
30 O homem respondeu, e disse-lhes: nisto pois está a maravilha, que vós não saibais de onde ele é, e me abrisse os olhos;
Yule mtu akajibu na kuwaambia, “Kwa nini, hili ni jambo la kushangaza, kwamba hamjui anakotoka, na bado ameyafumbua macho yangu.
31 Ora nós sabemos que Deus não ouve a pecadores; mas, se alguém é temente a Deus, e faz a sua vontade, a esse ouve.
Tunajua kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini ikiwa mtu yeyote anamwabudu Mungu na hufanya mapenzi yake, Mungu humsikiliza.
32 Desde todos os séculos nunca se ouviu que alguém abrisse os olhos a um que nasceu cego. (aiōn g165)
Tangu kuanza kwa Ulimwengu haijawahi kamwe kusikiwa kwamba yeyote ameyafumbua macho ya mtu aliyezaliwa kipofu. (aiōn g165)
33 Se este não fosse de Deus, nada poderia fazer.
Ikiwa mtu huyu hakutoka kwa Mungu, asingelifanya chochote.”
34 Responderam eles, e disseram-lhe: Tu és nascido todo em pecados, e nos ensinas a nós? E expulsaram-no.
Walijibu na kumwambia, “Ulizaliwa katika dhambi kabisa, na wewe unatufundisha sisi?” Ndipo walipomfukuza kutoka katika sinagogi.
35 Jesus ouviu que o tinham expulsado, e, encontrando-o, disse-lhe: Crês tu no Filho de Deus?
Yesu alisikia kwamba wamemwondoa kwenye sinagogi. Alimpata na kumwambia, “Unamwamini Mwana wa Mtu?”
36 Ele respondeu, e disse: Quem é ele, Senhor, para que nele creia?
Alijibu na kusema, “Ni nani, Bwana, ili nami nipate kumwamini?”
37 E Jesus lhe disse: Tu já o tens visto, e é aquele que fala contigo.
Yesu akamwambia, “Umeshamuona, naye unayezungumza naye ndiye.”
38 Ele disse: Creio, Senhor. E o adorou.
Yule mtu akasema, “Bwana, Naamini.” Ndipo akamsujudia.
39 E disse-lhe Jesus: Eu vim a este mundo para juízo, a fim de que os que não veem vejam, e os que veem sejam cegos.
Yesu akasema, “Kwa hukumu nimekuja katika Ulimwengu huu ili kwamba wale wasioona wapate kuona na wale wanaoona wawe vipofu.”
40 Aqueles dos fariseus, que estavam com ele, ouvindo isto, disseram-lhe: também nós somos cegos?
Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa pamoja naye wakasikia maneno hayo na kumwuliza, “Na sisi pia ni vipofu?”
41 Disse-lhes Jesus: Se fosseis cegos, não terieis pecado; mas agora dizeis: Vemos; por isso o vosso pecado permanece.
Yesu akawaambia, “Kama mngelikuwa vipofu, msingelikuwa na dhambi. Hata hivyo, sasa mnasema, 'Tunaona,' dhambi yenu inakaa.”

< João 9 >