< Jeremias 46 >

1 A palavra do Senhor, que veio a Jeremias o profeta, contra as nações;
Hili ni neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu mataifa:
2 Acerca do Egito, contra o exército de faraó Necho, rei do Egito, que estava junto ao rio Euphrates em Carchemis; ao qual feriu Nabucodonozor, rei de Babilônia, no ano quarto de Joaquim, filho de Josias, rei de Judá.
Kuhusu Misri: Huu ni ujumbe dhidi ya jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri, lililoshindwa huko Karkemishi kwenye Mto Frati na Nebukadneza mfalme wa Babeli, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda:
3 Preparai o escudo e o pavez, e chegai-vos para a peleja.
“Wekeni tayari ngao zenu, kubwa na ndogo, mtoke kwa ajili ya vita!
4 Selai os cavalos, e montai, cavaleiros, e apresentai-vos com elmos: alimpai as lanças, vesti-vos de couraças.
Fungieni farasi lijamu, pandeni farasi! Shikeni nafasi zenu mkiwa mmevaa chapeo! Isugueni mikuki yenu, vaeni dirii vifuani!
5 Por que razão vejo os medrosos voltando as costas? e os seus heroes são abatidos, e vão fugindo, sem olharem para traz: terror há ao redor, diz o Senhor.
Je, ninaona nini? Wametiwa hofu, wanarudi nyuma, askari wao wameshindwa. Wanakimbia kwa haraka pasipo kutazama nyuma, tena kuna hofu kuu kila upande,” asema Bwana.
6 Não fuja o ligeiro, e não escape o herói: para a banda do norte, junto à borda do rio Euphrates tropeçaram e cairam.
Walio wepesi na wenye mbio hawawezi kukimbia, wala wenye nguvu hawawezi kutoroka. Kaskazini, kando ya Mto Frati, wanajikwaa na kuanguka.
7 Quem é este que vem subindo como a corrente, cujas águas se movem como os rios?
“Ni nani huyu ajiinuaye kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi?
8 O Egito vem subindo como a corrente, e as suas águas se movem como os rios; e disse: Subirei, cobrirei a terra, destruirei a cidade, e os que habitam nela.
Misri hujiinua kama Mto Naili, kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi. Husema, ‘Nitainuka na kufunika dunia, nitaiangamiza miji na watu wake.’
9 Trepai, ó cavalos, e estrondeai, ó carros, e saiam os valentes: como também os ethiopes, e os puteos, que tomam o escudo, e os lydios, que tomam e entezam o arco.
Songeni mbele, enyi farasi! Endesheni kwa ukali, enyi magari ya farasi, Endeleeni mbele, enyi mashujaa: watu wa Kushi na Putu wachukuao ngao, watu wa Ludi wavutao upinde.
10 Porém este dia é do Senhor Jehovah dos exércitos, dia de vingança para se vingar dos seus adversários, e devorará a espada, e fartar-se-á, e embriagar-se-á com o sangue deles, porque o Senhor Jehovah dos exércitos tem um sacrifício na terra do norte, junto ao rio de Euphrates.
Lakini ile siku ni ya Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, siku ya kulipiza kisasi, kisasi juu ya adui zake. Upanga utakula hata utakapotosheka, hadi utakapozima kiu yake kwa damu. Kwa maana Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatoa dhabihu kwenye nchi ya kaskazini, kando ya Mto Frati.
11 Sobe a Gilead, e toma bálsamo, ó virgem filha do Egito: debalde multiplicas remédios, pois já não há cura para ti
“Panda hadi Gileadi ukapate zeri, ee Bikira Binti wa Misri. Lakini umetumia dawa nyingi bila mafanikio; huwezi kupona.
12 As nações ouviram a tua vergonha, e a terra está cheia do teu clamor; porque o valente chorou com o valente e cairam ambos juntamente.
Mataifa yatasikia juu ya aibu yako, kilio chako kitaijaza dunia. Shujaa mmoja atajikwaa juu ya mwingine, nao wataanguka chini pamoja.”
13 A palavra que falou o Senhor a Jeremias, o profeta, acerca da vinda de Nabucodonozor, rei de Babilônia, para ferir a terra do Egito.
Huu ndio ujumbe Bwana aliomwambia nabii Yeremia kuhusu kuja kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ili kuishambulia Misri:
14 Anunciai no Egito, e fazei ouvir isto em Migdol; fazei também ouvi-lo em Noph, e em Tahpanhes: dizei: Apresenta-te, e prepara-te; porque já devorou a espada o que está ao redor de ti.
“Tangaza hili katika Misri, nawe ulihubiri katika Migdoli, hubiri pia katika Memfisi na Tahpanhesi: ‘Shikeni nafasi zenu na mwe tayari, kwa kuwa upanga unawala wale wanaokuzunguka.’
15 Porque foram derribados os teus valentes? não se puderam ter em pé, porque o Senhor os empuxou.
Kwa nini mashujaa wako wamesombwa na kupelekwa mbali? Hawawezi kusimama, kwa maana Bwana atawasukuma awaangushe chini.
16 Multiplicou os que tropeçavam: também cairam uns sobre os outros, e disseram: Levanta-te, e voltemos ao nosso povo, e à terra do nosso nascimento, por causa da espada que oprime.
Watajikwaa mara kwa mara, wataangukiana wao kwa wao. Watasema, ‘Amka, turudi kwa watu wetu na nchi yetu, mbali na upanga wa mtesi.’
17 Clamaram ali: faraó rei do Egito é um estrondo; deixou passar o tempo assinalado.
Huko watatangaza, ‘Farao mfalme wa Misri ni makelele tu, amekosa wasaa wake.’
18 Vivo eu, diz o rei, cujo nome é o Senhor dos exércitos, que assim como está Tabor entre os montes, e como o Carmelo sobre o mar, certamente assim virá.
“Kwa hakika kama niishivyo,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote, “mmoja atakuja ambaye ni kama Tabori miongoni mwa milima, kama Karmeli kando ya bahari.
19 Prepara-te aparelhos para a ida em cativeiro, ó moradora, filha do Egito: porque Noph será tornada em desolação, e será abrazada, até que ninguém mais ai more.
Funga mizigo yako kwenda uhamishoni, wewe ukaaye Misri, kwa kuwa Memfisi utaangamizwa na kuwa magofu pasipo mkazi.
20 Bezerra mui formosa é o Egito: já vem a destruição, ela vem do norte.
“Misri ni mtamba mzuri, lakini kipanga anakuja dhidi yake kutoka kaskazini.
21 Até os seus mercenários no meio dela são como bezerros cevados; porém também eles viraram as costas, fugiram juntos; não estiveram firmes; porque já veio sobre eles o dia da sua ruína e o tempo da sua visitação.
Askari wake waliokodiwa katika safu zake wako kama ndama walionenepeshwa. Wao pia watageuka na kukimbia pamoja, hawataweza kuhimili vita, kwa maana siku ya msiba inakuja juu yao, wakati wao wa kuadhibiwa.
22 A sua voz irá como a da serpente; porque irão com poder do exército, e virão a ela com machados como cortadores de lenha.
Misri atatoa sauti kama ya nyoka anayekimbia kadiri adui anavyowasogelea na majeshi, watakuja dhidi yake wakiwa na mashoka, kama watu wakatao miti.
23 Cortaram o seu bosque, diz o Senhor, ainda que não podem contar-se; porque se multiplicaram mais do que os gafanhotos, não se podem numerar.
Wataufyeka msitu wake,” asema Bwana, “hata kama umesongamana kiasi gani. Ni wengi kuliko nzige, hawawezi kuhesabika.
24 A filha do Egito está envergonhada: foi entregue na mão do povo do norte.
Binti wa Misri ataaibishwa, atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.”
25 Diz o Senhor dos exércitos, o Deus de Israel: Eis que eu visitarei a multidão de No, e a faraó, e ao Egito, e aos seus deuses, e aos seus reis, e até ao mesmo faraó, e aos que confiam nele.
Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asema: “Nakaribia kuleta adhabu juu ya Amoni mungu wa Thebesi, na juu ya Farao, Misri na miungu yake, na wafalme wake, pamoja na wale wanaomtegemea Farao.
26 E os entregarei na mão dos que procuram a sua morte, na mão de Nabucodonozor, rei de Babilônia, e na mão dos seus servos; porém depois será habitada, como nos dias antigos, diz o Senhor.
Nitawatia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wao, yaani Nebukadneza mfalme wa Babeli na maafisa wake. Hatimaye, hata hivyo, Misri itakaliwa kama nyakati zilizopita,” asema Bwana.
27 Não temas pois tu, servo meu Jacob, nem te espantes, ó Israel; porque eis que te livrarei de terras de longe, como também a tua semente da terra do seu cativeiro; e Jacob voltará, e descançará, e sossegará, e não haverá quem o atemorize.
“Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli. Hakika nitakuokoa kutoka nchi za mbali, uzao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na salama, wala hakuna hata mmoja atakayewatia hofu.
28 Tu não temas, servo meu, Jacob, diz o Senhor, porque estou contigo; porque farei consumação de todas as nações entre as quais te lancei; porém de ti não farei consumação, mas castigar-te-ei com medida, e não te darei de todo por inocente
Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, kwa maana mimi niko pamoja nawe,” asema Bwana. “Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambayo miongoni mwake nimekutawanya, sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakurudi, lakini kwa haki tu, wala sitakuacha kabisa bila kukuadhibu.”

< Jeremias 46 >