< Jeremias 29 >
1 E estas são as palavras da carta que Jeremias, o profeta, enviou de Jerusalém, ao resto do cativeiro dos anciãos, como também aos sacerdotes, e aos profetas, e a todo o povo que Nabucodonozor havia transportado de Jerusalém a Babilônia;
Haya ndiyo maneno ya ile barua ambayo nabii Yeremia aliituma kutoka Yerusalemu kwenda kwa wazee waliobaki miongoni mwa wale waliohamishwa, na kwa makuhani, manabii na watu wengine wote ambao Nebukadneza alikuwa amewachukua kwenda uhamishoni Babeli kutoka Yerusalemu.
2 Depois que sairam o rei Jechonias, e a rainha, e os eunucos, e os príncipes de Judá e Jerusalém, e os carpinteiros e ferreiros de Jerusalém,
(Hii ilikuwa ni baada ya Mfalme Yekonia na malkia mamaye, maafisa wa mahakama, viongozi wa Yuda na wa Yerusalemu, mafundi na wahunzi kwenda uhamishoni kutoka Yerusalemu.)
3 Pela mão de Elasa, filho de Saphan, e de Gemarias, filho de Hilkias, os quais enviou Zedekias, rei de Judá, a Babilônia, a Nabucodonozor, rei de Babilônia, dizendo:
Barua ilikabidhiwa kwa Elasa mwana wa Shafani, na kwa Gemaria mwana wa Hilkia, ambao Sedekia mfalme wa Yuda aliwatuma kwa Mfalme Nebukadneza huko Babeli. Barua yenyewe ilisema:
4 Assim diz o Senhor dos exércitos, o Deus de Israel, a todos os que foram transportados, os quais fiz transportar de Jerusalém para Babilônia:
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, awaambialo wale wote niliowapeleka kutoka Yerusalemu kwenda uhamishoni Babeli:
5 Edificai casas e habitai nelas; e plantai jardins, e comei o seu fruto.
“Jengeni nyumba na mstarehe, pandeni bustani na mle mazao yake.
6 Tomai mulheres e gerai filhos e filhas, e tomai mulheres para vossos filhos, e dai vossas filhas a maridos, e parirão filhos e filhas; e multiplicai-vos ali, e não vos diminuais.
Oeni wake na mzae wana na binti, waozeni wana wenu wake, nanyi watoeni binti zenu waolewe, ili nao pia wazae wana na binti. Ongezekeni idadi yenu huko, wala msipungue.
7 E procurai a paz da cidade, para onde vos fiz transportar, e orai por ela ao Senhor; porque na sua paz vós tereis paz.
Pia tafuteni amani na mafanikio ya mji ambamo nimewapeleka uhamishoni. Mwombeni Bwana kwa ajili ya mji huo, kwa sababu ukistawi, ninyi pia mtastawi.”
8 Porque assim diz o Senhor dos exércitos, o Deus de Israel: Não vos enganem os vossos profetas que estão no meio de vós, nem os vossos adivinhos, nem deis ouvidos aos vossos sonhos, que vós sonhais:
Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Msikubali manabii na wabashiri walioko miongoni mwenu wawadanganye. Msisikilize ndoto ambazo mmewatia moyo kuota.
9 Porque eles vos profetizam falsamente no meu nome: não os enviei, diz o Senhor.
Wanawatabiria ninyi uongo kwa jina langu. Sikuwatuma,” asema Bwana.
10 Porque assim diz o Senhor: Certamente que em se cumprindo setenta anos em Babilônia, vos visitarei, e continuarei sobre vós a minha boa palavra, tornando-vos a trazer a este lugar.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Miaka sabini itakapotimia kwa ajili ya Babeli, nitakuja kwenu na kutimiza ahadi yangu ya rehema ya kuwarudisha mahali hapa.
11 Porque eu bem sei os pensamentos que eu penso de vós, diz o Senhor; pensamentos de paz, e não de mal, para vos dar o fim que esperais.
Kwa maana ninajua mipango niliyo nayo kwa ajili yenu,” asema Bwana, “ni mipango ya kuwafanikisha na wala si ya kuwadhuru, ni mipango ya kuwapa tumaini katika siku zijazo.
12 Então me invocareis, e ireis, e orareis a mim, e eu vos ouvirei.
Kisha mtaniita, na mtakuja na kuniomba, nami nitawasikiliza.
13 E buscar-me-eis, e me achareis, quando me buscardes com todo o vosso coração.
Mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
14 E serei achado de vós, diz o Senhor, e farei tornar os vossos cativos, e congregar-vos-ei de todas as nações, e de todos os lugares para onde vos lancei, diz o Senhor, e tornarei a trazer-vos ao lugar de onde vos transportei.
Nitaonekana kwenu,” asema Bwana, “nami nitawarudisha watu wenu waliotekwa. Nitawakusanya kutoka mataifa yote na mahali pote nilipokuwa nimewafukuzia, nami nitawarudisha mahali ambapo nilikuwa nimewatoa walipochukuliwa uhamishoni,” asema Bwana.
15 Porque dizeis: O Senhor nos levantou profetas em Babilônia.
Mnaweza mkasema, “Bwana ameinua manabii kwa ajili yetu huku Babeli,”
16 Porque assim diz o Senhor acerca do rei que se assenta no trono de David; e acerca de todo o povo que habita nesta cidade, a saber, de vossos irmãos, que não sairam convosco para o cativeiro;
lakini hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme aketiaye kiti cha enzi cha Daudi, na watu wa kwenu wote wanaobaki katika mji huu, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi uhamishoni.
17 Assim diz o Senhor dos exércitos: Eis que enviarei entre eles a espada, a fome e a peste, e fa-los-ei como a figos podres, que não se podem comer, de maus que são.
Naam, hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Nitatuma upanga, njaa na tauni dhidi yao, nami nitawafanya kuwa kama tini dhaifu zile ambazo ni mbovu sana zisizofaa kuliwa.
18 E persegui-los-ei com a espada, com a fome, e com a peste; dá-los-ei para servirem de comoção a todos os reinos da terra, como também por maldição, e por espanto, e por assobio, e por opróbrio entre toda sas nações para onde os lançar;
Nitawafukuza kwa upanga, kwa njaa na kwa tauni, nami nitawafanya kitu cha kuchukiza sana kwa falme zote za dunia, na kuwa kitu cha laana na cha kuogofya, cha dharau na kukemewa, miongoni mwa mataifa yote nitakakowafukuzia.
19 Porquanto não deram ouvidos às minhas palavras, diz o Senhor, enviando-lhes eu os meus servos, os profetas, madrugando e enviando; porém vós não escutastes, diz o Senhor.
Kwa kuwa hawakuyasikiliza maneno yangu,” asema Bwana, “maneno ambayo niliwatumia tena na tena kupitia watumishi wangu manabii. Wala ninyi watu wa uhamisho hamkusikiliza pia,” asema Bwana.
20 Vós, pois, ouvi a palavra do Senhor, todos os do cativeiro que enviei de Jerusalém a Babilônia.
Kwa hiyo, sikieni neno la Bwana, enyi nyote mlio uhamishoni, niliowapeleka Babeli kutoka Yerusalemu.
21 Assim diz o Senhor dos exércitos, o Deus de Israel, acerca de Ahab, filho de Colaias, e de Zedekias, filho de Maaseias, que vos profetizam falsamente no meu nome: Eis que os entregarei na mão de Nabucodonozor, rei de Babilônia, e ele os ferirá diante dos vossos olhos.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu Ahabu mwana wa Kolaya, na Sedekia mwana wa Maaseya, wanaowatabiria uongo kwa jina langu: “Nitawatia mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atawaua mbele ya macho yenu hasa.
22 E tomarão deles uma maldição todos os transportados de Judá, que estão em Babilônia, dizendo: O Senhor te faça como Zedekias, e como Ahab, os quais o rei de Babilônia assou no fogo
Kwa ajili yao, watu wote wa uhamisho kutoka Yuda walioko Babeli watatumia laana hii: ‘Bwana na akutendee kama Sedekia na Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwachoma kwa moto.’
23 Porquanto fizeram loucura em Israel, e cometeram adultério com as mulheres de seus companheiros, e falaram uma palavra no meu nome falsamente, que não lhes mandei, e eu o sei e sou testemunha disso, diz o Senhor.
Kwa kuwa wamefanya mambo maovu kabisa katika Israeli, wamezini na wake za majirani zao, tena kwa Jina langu wamesema uongo, mambo ambayo sikuwaambia kuyafanya. Nami nayajua haya, na ni shahidi wa jambo hilo,” asema Bwana.
24 E a Shemaias, o nehelamita, falarás, dizendo:
Mwambie Shemaya Mnehelami,
25 Assim diz o Senhor dos exércitos, o Deus de Israel, dizendo: Porquanto tu enviaste no teu nome cartas a todo o povo que está em Jerusalém, como também a Sofonias, filho de Maaseias, o sacerdote, e a todos os sacerdotes, dizendo:
“Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ulituma barua kwa jina lako mwenyewe kwa watu wote wa Yerusalemu, kwa Sefania mwana wa kuhani Maaseya na kwa makuhani wengine wote. Ulimwambia Sefania,
26 O Senhor te pôs por sacerdote em lugar de Joiada, o sacerdote, para que sejais encarregados da casa do Senhor sobre todo o homem furioso, e que profetiza, para o lançares na prisão e no tronco.
‘Bwana amekuweka wewe uwe kuhani badala ya Yehoyada ili uwe msimamizi wa nyumba ya Bwana. Unapaswa kufunga kwa mikatale na mnyororo wa shingoni mwendawazimu yeyote anayejifanya nabii.
27 Agora, pois, porque não repreendeste a Jeremias, o anathotita, que profetiza vos?
Kwa nini basi hukumkemea Yeremia Mwanathothi, aliyejifanya kama nabii miongoni mwenu?
28 Porque por isso nos mandou a nós a Babilônia, dizendo: Ainda o cativeiro muito há de durar; edificai casas, e habitai nelas; e plantai jardins, e comei o seu fruto.
Ametutumia ujumbe huu huku Babeli: Mtakuwako huko muda mrefu. Kwa hiyo jengeni nyumba mkakae; pandeni mashamba na mle mazao yake.’”
29 E lera Sofonias, o sacerdote, esta carta aos ouvidos de Jeremias, o profeta.
Kuhani Sefania, hata hivyo, akamsomea nabii Yeremia ile barua.
30 E veio a palavra do Senhor a Jeremias, dizendo:
Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
31 Manda a todos os do cativeiro, dizendo: Assim diz o Senhor acerca de Semaias, o nehelamita: Porquanto Semaias vos profetizou, e eu não o enviei, e vos fez confiar em mentiras,
“Tuma ujumbe huu kwa watu wote walio uhamishoni: ‘Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu Shemaya Mnehelami: Kwa sababu Shemaya amewatabiria ninyi, hata ingawa sikumtuma, naye amewafanya kuamini uongo,
32 Portanto assim diz o Senhor: Eis que visitarei a Semaias, o nehelamita, e a sua semente: ele não terá ninguém que habite entre este povo, e não verá o bem que hei de fazer ao meu povo, diz o Senhor, porquanto falou rebelião contra o Senhor.
hili ndilo Bwana asemalo: Hakika nitamwadhibu Shemaya Mnehelami pamoja na uzao wake. Hapatakuwa na yeyote atakayebaki miongoni mwa watu hawa, wala hataona mema nitakayowatendea watu wangu, asema Bwana, kwa sababu ametangaza uasi dhidi yangu.’”