< Isaías 40 >

1 Consolai, consolai o meu povo, diz o vosso Deus.
Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
2 Falai benignamente a Jerusalém, e bradai-lhe que já a sua malícia é acabada, que já a sua iniquidade está expiada e que já recebeu em dobro da mão do Senhor, por todos os seus pecados.
Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
3 Voz do que clama no deserto: aparelhai o caminho do Senhor: endireitai no ermo vereda a nosso Deus.
Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
4 Todo o vale será exaltado, e todo o monte e todo o outeiro serão abatidos: e o torcido se endireitará, e o áspero se aplainará.
Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
5 E a glória do Senhor se manifestará, e toda a carne juntamente verá que a boca do Senhor o disse.
Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
6 Voz que diz: Clama; e disse: Que hei de clamar? Toda a carne é erva e toda a sua benignidade como as flores do campo.
Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
7 Seca-se a erva, e caem as flores, soprando nelas o espírito do Senhor. Na verdade que erva é o povo.
Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
8 Seca-se a erva, e caem as flores, porém a palavra de nosso Deus subsiste eternamente.
Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
9 Ah Sião, anunciadora de boas novas, sobe tu a um monte alto. Ah Jerusalém, anunciadora de boas novas, levanta a tua voz fortemente; levanta-a, não temas, e dize às cidades de Judá: Eis aqui está o vosso Deus.
Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
10 Eis que o Senhor Jehovah virá contra o forte, e o seu braço se assenhoreará dele: eis que o seu galardão vem com ele, e o seu salário diante da sua face.
Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
11 Como pastor apascentará o seu rebanho; entre os seus braços recolherá os cordeirinhos, e os levará no seu seio: as paridas guiará suavemente.
Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
12 Quem mediu com o seu punho as águas, e tomou a medida dos céus aos palmos, e recolheu na maior medida o pó da terra e pesou os montes com peso e os outeiros em balanças?
Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
13 Quem guiou o espírito do Senhor? e que conselheiro o ensinou?
Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
14 Com quem tomou conselho, que lhe desse entendimento, e lhe ensinasse o caminho do juízo? lhe ensinasse sabedoria, e lhe fizesse notório o caminho da ciência?
Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
15 Eis que as nações são consideradas por ele como a gota dum balde, e como o pó miúdo das balanças: eis que lança por ai as ilhas como a pó miúdo.
Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
16 Nem todo o líbano basta para o fogo, nem os seus animais bastam para holocaustos.
Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
17 Todas as nações são como nada perante ele; e as reputa por menos que nada e como uma coisa vã
Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
18 A quem pois fareis semelhante a Deus? ou que semelhança lhe apropriareis?
Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
19 O artífice funde a imagem, e o ourives a cobre de ouro, e cadeias de prata lhe funde.
Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
20 O empobrecido, que já não tem que oferecer, escolhe madeira que não se corrompe: artífice sábio se busca, para aparelhar uma imagem que se não possa mover.
Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
21 Porventura não sabeis? porventura não ouvis? ou desde o princípio se vos não notificou? ou não atentastes para os fundamentos da terra?
Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
22 Ele é o que está assentado sobre o globo da terra, cujos moradores são para ele como gafanhotos: ele é o que estende os céus como cortina, e os desenrola como tenda, para habitar neles:
Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
23 O que torna em nada os príncipes, e faz como em coisa vã os juízes da terra.
Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
24 E nem se plantam, nem se semeiam, nem se arraiga na terra o seu tronco cortado, e neles, soprando, se secaram, e um tufão como pragana os levará.
Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
25 A quem pois me fareis semelhante, que lhe seja semelhante? diz o Santo.
“Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
26 Levantai ao alto os vossos olhos, e vede quem criou estas coisas, quem produz por conta o seu exército, quem a todas chama pelos seus nomes; por causa da grandeza das suas forças, e porquanto é forte em poder, nenhuma delas vem a faltar.
Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
27 Porque pois dizes, ó Jacob, e tu falas, ó Israel: O meu caminho está encoberto ao Senhor, e o meu juízo passa de largo pelo meu Deus?
Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
28 Porventura não sabes, porventura não ouviste que o eterno Deus, o Senhor, o criador dos fins da terra, nem se cança nem se fatiga? não há esquadrinhação do seu entendimento.
Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
29 Dá esforço ao cançado, e multiplica as forças ao que não tem nenhum vigor.
Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
30 Os moços se cançarão e se fatigarão, e os mancebos certamente cairão.
Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
31 Mas os que esperam no Senhor renovarão as forças, subirão com asas como águias: correrão, e não se cançarão; caminharão, e não se fatigarão.
bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.

< Isaías 40 >