< Êxodo 28 >

1 Depois tu farás chegar a ti teu irmão Aarão, e seus filhos com ele, do meio dos filhos de Israel, para me administrarem o ofício sacerdotal: a saber, Aarão, Nadab e Abihu, Eleazar e Ithamar, os filhos de Aarão.
Umuite Aruni kaka yako na wana wake - Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari - miongoni mwa wana wa Israeli, ili anitumikie katika kazi ya ukuhani.
2 E farás vestidos santos a Aarão teu irmão, para glória e ornamento.
Nawe utamfanyia Aruni ndugu yako mavazi matakatifu, kwa utukufu na kwa uzuri.
3 Falarás também a todos os que são sábios de coração, a quem eu tenho enchido do espírito da sabedoria, que façam vestidos a Aarão para santifica-lo; para que me administre o ofício sacerdotal.
Nawe utawaambia watu wote wenye moyo wa hekima, niliowajaza na roho ya hekima wamfanyie Aruni mavazi ili kumtakasa anitumikie katika kazi ya ukuhani.
4 Estes pois são os vestidos que farão: um peitoral, e um éfode, e um manto, e uma túnica bordada, uma mitra, e um cinto: farão pois santos vestidos a Aarão teu irmão, e a seus filhos, para me administrarem o ofício sacerdotal.
Na mavazi watakayoyafanya ni kifuko cha kifuani, na naivera, na joho, na kanzu ya kazi ya urembo, na kilemba, na mshipi; nao watawafanyia Aruni nduguye, na wanawe, mavazi matakatifu ili anitumikie katika kazi ya ukuhani.
5 E tomarão o ouro, e o azul, e a púrpura, e o carmezim, e o linho fino,
Nao wataitwaa dhahabu, na nguo ya rangi ya samawi, na ya rangi ya zambarau, na ya rangi nyekundu.
6 E farão o éfode de ouro, e de azul, e de púrpura, e de carmezim, e de linho fino torcido, de obra esmerada.
Nao waifanye naivera kwa nyuzi za dhahabu, na za samawi, na za zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa kwa kazi ya mstadi.
7 Terá duas hombreiras, que se unam às suas duas pontas, e assim se unirá.
Lazima itakuwa na vipande viwili vya mabegani, vilivyoungana kwenye ncha zake mbili; ili ipate kuunganywa.
8 E o cinto de obra esmerada do seu éfode, que estará sobre ele, será da sua mesma obra, do mesmo, de ouro, de azul, e de púrpura, e de carmezim, e de linho fino torcido.
Na mshipi wa kazi ya ustadi ulio juu yake, ili kuifunga mahali pake; utakuwa wa kazi kama ile ya naivera, ya vitu vile vile ya nyuzi za dhahabu, na za rangi ya samawi, na ya zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa.
9 E tomarás duas pedras sardônicas, e lavrarás nelas os nomes dos filhos de Israel,
Nawe utatwaa vito viwili vya shohamu, ya rangi ya chani-kiwiti, nawe utachora juu yake majina ya wana wa Israeli;
10 Seis dos seus nomes numa pedra, e os outros seis nomes na outra pedra, segundo as suas gerações;
Majina yao sita katika kito kimoja, na majina sita yaliyosalia katika kile kito cha pili, kwa utaratibu wa kuzaliwa kwao.
11 Conforme à obra do lapidário, como o lavor de sêlos lavrarás estas duas pedras, com os nomes dos filhos de Israel: engastadas ao redor em ouro as farás.
Kwa kazi mtu mwenye kuchora mawe kama vile muhuri ichorwavyo, utavichora hivi vito viwili, sawasawa na majina ya wana wa Israeli, nawe utavitia katika vijalizo vya dhahabu.
12 E porás as duas pedras nas hombreiras do éfode, por pedras de memória para os filhos de Israel: e Aarão levará os seus nomes sobre ambos os seus ombros, para memória diante do Senhor.
Nawe utavitia vile vito viwili juu ya vipande vya mabegani vya hiyo naivera, viwe vito vya ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli. Naye Aruni atayachukua majina yao mbele za Yahweh juu ya mabega yake mawili ili kuwa ukumbusho.
13 Farás também engastes de ouro,
Nawe fanya vijalizo viwili vya dhahabu
14 E duas cadeiazinhas de ouro puro: de igual medida, de obra de fieira as farás: e as cadeiazinhas de fieira porás nos engastes.
na mikufu miwili ya dhahabu safi; utaifanya iwe mfano wa kamba, ya kazi ya kusokotwa; nawe uitie ile mikufu ya kazi ya kusokotwa katika vile vijalizo.
15 Farás também o peitoral do juízo de obra esmerada, conforme à obra do éfode o farás: de ouro, de azul, e de púrpura, e de carmezim, e de linho fino torcido o farás.
Nawe lazima utafanya kifuko cha kifuani cha hukumu, kazi ya fundi stadi; utakifanya kwa kuiandama ile kazi ya hiyo naivera. Fanya nyuzi za dhahabu, na za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na nyekundu, na kitani safi yenye kusokotwa, ndivyo utakavyokifanya.
16 Quadrado e dobrado, será de um palmo o seu comprimento, e de um palmo a sua largura;
Kitakuwa mraba, tena cha kukunjwa; urefu wake utakuwa shibiri moja, na upana wake shibiri moja.
17 E o encherás de pedras de engaste, com quatro ordens de pedras: a ordem de uma sárdia, de um topázio, e de um carbúnculo: esta será a primeira ordem:
Nawe ukijaze viweko vya vito, safu nne za vito; safu moja itakuwa ni akiki, na yakuti ya rangi ya manjano, na baharamani, hivi vitakuwa safu ya kwanza.
18 E a segunda ordem será de uma esmeralda, de uma safira, e de um diamante:
Na safu ya pili itakuwa zumaridi, na yakuti samawi, na almasi.
19 E a terceira ordem será de um jacinto, de uma ágata, e de uma ametista:
Na safu ya tatu itakuwa hiakintho, na akiki nyekundu, na amethisto.
20 E a quarta ordem será de uma turqueza, e de uma sardônica, e de um jaspe; engastadas em ouro serão nos seus engastes.
Na safu ya nne itakuwa ni zabarajadi, na shohamu, na yaspi. Vito hivyo vitakazwa ndani ya dhahabu kwa kujaa mahali pake.
21 E serão aquelas pedras segundo os nomes dos filhos de Israel, doze segundo os seus nomes: serão esculpidas como sêlos, cada uma com o seu nome, para as doze tribos.
Na vile vito vitakuwa sawasawa na majina ya wana wa Israeli, kumi na viwili, sawasawa na majina yao. Mfano wa kuchora kwa muhuri kila kimoja sawasawa na jina lake, vitakuwa vya hizo kabila kumi na mbili.
22 Também farás ao peitoral cadeiazinhas de igual medida da obra de trança de ouro puro.
Nawe lazima utie katika kile kifuko cha kifuani mikufu mfano wa kamba, ya kazi ya kusokotwa, ya dhahabu safi.
23 Também farás ao peitoral dois anéis de ouro, e porás os dois anéis nas extremidades do peitoral.
Nawe utie maduara mawili ya dhahabu katika kile kifuko cha kifuani, na kuzitia hizo pete mbili katika ncha mbili za kifuko cha kifuani.
24 Então meterás as duas cadeiazinhas de fieira de ouro nos dois anéis, nas extremidades do peitoral:
Nawe utie hiyo mikufu miwili ya dhahabu iliyosokotwa katika zile pete mbili zilizo katika ncha za kifuko cha kifuani.
25 E as duas pontas das duas cadeiazinhas de fieira meterás nos dois engastes, e as porás nas hombreiras do éfode, defronte dele.
Na ncha zile nyingine za hiyo mikufu miwili ya kusokotwa utazitia katika vile vijalizo viwili, na kuvitia katika vile vipande vya mabegani vya naivera upande wa mbele.
26 Farás também dois anéis de ouro, e os porás nas duas extremidades do peitoral, na sua borda que estiver junto ao éfode por dentro.
Nawe utafanya viduara vili vya dhahabu, uzitie katika hizo ncha mbili za kifuko cha kifuani, katika ukingo wake.
27 Farás também dois anéis de ouro, que porás nas duas hombreiras do éfode, abaixo, defronte dele, defronte da sua juntura, sobre o cinto da obra esmerada do éfode.
Nawe lazima ufanye viduara vili vya dhahabu, na kuzitia katika vile vipande viwili vya mabegani vya ile naivera chini yake, upande wa mbele, karibu na kifungo chake, juu ya huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi.
28 E ligarão o peitoral com os seus anéis aos anéis do éfode por cima com um cordão de azul, para que esteja sobre o cinto da obra esmerada do éfode; e nunca se separará o peitoral do éfode.
Nao watakikaza kile kileso kwa vile viduara vyake kwenye viduara za naivera kwa ukanda wa rangi ya samawi, ili kwamba kikae pale juu ya ule mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi, ili kwamba kifuko cha kifuani kisiachane na naivera.
29 Assim Aarão levará os nomes dos filhos de Israel no peitoral do juízo sobre o seu coração, quando entrar no santuário, para memória diante do Senhor continuamente.
Na Aruni atayachukua majina ya wana wa Israeli katika kile kifuko cha kifuani cha hukumu juu ya moyo wake kwa kufanya maamuzi, hapo atakapoingia ndani ya mahali patakatifu, kuwa ukumbusho mbele yaYahweh daima.
30 Também porás no peitoral do juízo Urim e Tumim, para que estejam sobre o coração de Aarão, quando entrar diante do Senhor: assim Aarão levará o juízo dos filhos de Israel sobre o seu coração diante do Senhor continuamente.
Nawe utie hizo Urimu na Thumimu katika kile kifuko cha kifuani cha hukumu; nazo zitakuwa juu ya moyo wa Aruni, hapo atakapoingia ndani mbele ya Yahweh na Aruni atachukua hukumu ya hao wana wa Israeli juu ya moyo wake mbele ya Yahweh daima.
31 Também farás o manto do Éfode, todo azul.
Nawe fanya hiyo joho ya naivera ya rangi ya samawi yote.
32 E o colar da cabeça estará no meio dele: este colar terá uma borda da obra tecida ao redor: como colar de saia de malha será nele, para que se não rompa.
Nayo itakuwa na tundu katikati yake kwa kupitisha kichwa; itakuwa na utepe wa kazi ya kusokotwa kuzunguka hilo tundu lake, mfano wa tundu lililo katika kanzu ya chuma, ili lisipasuke.
33 E nas suas bordas farás romãs de azul, e de púrpura, e de carmezim, ao redor das suas bordas; e campainhas de ouro no meio delas ao redor.
Nawe katika pindo zake utatia makomamanga ya rangi ya samawi, na ya rangi ya zambarau, na ya rangi nyekundu, kuzunguka pindo zake kotekote; na njuga za dhahabu kati ya hayo makomamanga pande zote.
34 Uma campainha de ouro, e uma romã, outra campainha de ouro, e outra romã, haverá nas bordas do manto ao redor,
Kengele ya dhahabu na komamanga, kengele ya dhahabu na komamanga, katika pindo za joho kuizunguka pande zote.
35 E estará sobre Aarão quando ministrar, para que se ouça o seu sonido, quando entrar no santuário diante do Senhor, e quando sair, para que não morra.
Nayo itakuwa juu ya Aruni akitumika; na sauti ya hizo kengele itasikilikana hapo aingiapo ndani ya mahali patakatifu mbele ya Yahweh na hapo atokapo nje, ili kwamba asife.
36 Também farás uma lâmina de ouro puro, e nela gravarás à maneira de gravuras de selos: santidade ao Senhor.
Nawe fanya bamba la dhahabu safi na kuchora juu yake, mfano wa machoro ya muhuri, “Mtakatifu kwa Yahweh.”
37 E ata-la-ás com um cordão de azul, de maneira que esteja na mitra; sobre a frente da mitra estará.
Nawe ulitie hilo bamba katika ukanda wa rangi ya samawi, nalo litakuwa katika kile kilemba; litakuwa upande wa mbele wa kile kilemba.
38 E estará sobre a testa de Aarão, para que Aarão leve a iniquidade das coisas santas, que os filhos de Israel santificarem em todas as ofertas de suas coisas santas; e estará continuamente na sua testa, para que tenham aceitação perante o Senhor.
Nalo litakuwa katika kipaji cha uso cha Aruni, na Aruni atauchukua uovu wa vile vitu vitakatifu, watakavyovitakasa hao wana wa Israeli katika vipawa vyao vyote vitakatifu, nalo litakuwa katika kipaji chake cha uso sikuzote, ili kwamba vipate kukubaliwa mbele za Yahweh.
39 Também farás túnica de linho fino: também farás uma mitra de linho fino: mas o cinto farás da obra de bordador.
Na hiyo kanzu utaifuma ya kitani nzuri ya kazi ya urembo, ufanye na kilemba cha nguo ya kitani nzuri, nawe utafanya mshipi wa kazi ya mwenye kutia taraza.
40 Também farás túnicas aos filhos de Aarão, e far-lhes-ás cintos: também lhes farás tiaras, para glória e ornamento.
Kisha utafany kanzu kwa ajili ya wana wa Aruni, nawe wafanyie mishipi, wafanyie na kofia kwa utukufu na uzuri.
41 E vestirás com eles a Aarão teu irmão, e também seus filhos: e os ungirás e consagrarás, e os santificarás, para que me administrem o sacerdócio.
Nawe mvike huyo nduguye Aruni na wanawe nao mavazi hayo; nawe watie mafuta, na kuwaweka kwa kazi takatifu, na kuwatakasa, ili wapate kunitumikia mimi katika kazi ya ukuhani.
42 Faze-lhes também calções de linho, para cobrirem a carne nua: serão dos lombos até às pernas.
Nawe wafanyie suruali za nguo ya kitani, ili kufunika tupu ya miili yao; suruali hizo zitafika tangu kiunoni hata mapajani.
43 E estarão sobre Aarão e sobre seus filhos, quando entrarem na tenda da congregação, ou quando chegarem ao altar para ministrar no santuário, para que não levem iniquidade, e morram; isto será estatuto perpétuo para ele e para a sua semente depois dele.
Aruni na wanawe watazivaa, hapo watakapoingia katika hema ya kukutania, au hapo watakapoikaribia madhabahu ili watumike katika mahali patakatifu; wasije wakachukua uovu, wakafa; hii itakuwa ni amri ya milele kwake yeye, na kwa wazao wake.

< Êxodo 28 >