< Deuteronômio 23 >
1 O quebrado de quebradura, e o castrado, não entrará na congregação do Senhor.
Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko la Bwana.
2 Nenhum bastardo entrará na congregação do Senhor: nem ainda a sua décima geração entrará na congregação do Senhor.
Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
3 Nenhum amonita nem moabita entrará na congregação do Senhor: nem ainda a sua décima geração entrará na congregação do Senhor eternamente.
Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
4 Porquanto não sairam com pão e água, a receber-vos no caminho, quando saíeis do Egito; e porquanto alugou contra ti a Balaão, filho de Beor, de Pethor, de Mesopotâmia, para te amaldiçoar.
Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimu ili kuwalaani ninyi.
5 Porém o Senhor teu Deus não quis ouvir Balaão: antes o Senhor teu Deus trocou em benção a maldição; porquanto o Senhor teu Deus te amava.
Hata hivyo, Bwana Mungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababu Bwana Mungu wenu anawapenda.
6 Não lhes procurarás nem paz nem bem em todos os teus dias para sempre.
Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote.
7 Não abominarás o edumeu, pois é teu irmão: nem abominarás o egípcio; pois estrangeiro foste na sua terra.
Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake.
8 Os filhos que lhes nascerem na terceira geração, cada um deles entrará na congregação do Senhor.
Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko la Bwana.
9 Quando o exército sair contra os teus inimigos, então te guardarás de toda a coisa má.
Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi.
10 Quando entre ti houver algum que por algum acidente de noite não estiver limpo, sairá fora do exército; não entrará no meio do exército.
Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko.
11 Porém será que, declinando a tarde, se lavará em água; e, em se pondo o sol, entrará no meio do arraial.
Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini.
12 Também terás um lugar fora do arraial; e ali sairás fora.
Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia.
13 E entre as tuas armas terás uma pá; e será que, quando estiveres assentado fora, então com ela cavarás, e, virando-te, cobrirás aquilo que saiu de ti.
Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho.
14 Porquanto o Senhor teu Deus anda no meio do teu arraial, para te livrar, e entregar os teus inimigos diante de ti: pelo que o teu arraial será santo: para que ele não veja coisa feia em ti, e se torne atráz de ti.
Kwa kuwa Bwana Mungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha.
15 Não entregarás a seu senhor o servo que se acolher a ti de seu senhor;
Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake.
16 Contigo ficará no meio de ti, no lugar que escolher em alguma das tuas portas, onde lhe estiver bem: não o oprimirás.
Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee.
17 Não haverá rameira dentre as filhas de Israel; nem haverá sodomita dentre os filhos de Israel.
Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
18 Não trarás salário de rameira nem preço de cão à casa do Senhor teu Deus por qualquer voto: porque estes ambos são igualmente abominação ao Senhor teu Deus.
Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba ya Bwana Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu Bwana Mungu wako anachukizwa na yote mawili.
19 A teu irmão não emprestarás à usura, nem à usura de dinheiro, nem à usura de comida, nem à usura de qualquer coisa que se empreste à usura.
Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake.
20 Ao estranho emprestarás à usura, porém a teu irmão não emprestarás à usura: para que o Senhor teu Deus te abençoe em tudo no que puseres a tua mão, na terra a qual vais a possuir.
Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwamba Bwana Mungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki.
21 Quando votares algum voto ao Senhor teu Deus, não tardarás em paga-lo; porque o Senhor teu Deus certamente o requererá de ti, e em ti haverá pecado.
Ukiweka nadhiri kwa Bwana Mungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi.
22 Porém, abstendo-te de votar, não haverá pecado em ti
Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia.
23 O que saiu da tua boca guardarás, e o farás; trazendo a oferta voluntária, assim como votaste ao Senhor teu Deus, o que declaraste pela tua boca.
Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele za Bwana Mungu wako kwa kinywa chako mwenyewe.
24 Quando entrares na vinha do teu próximo, comerás uvas conforme ao teu desejo até te fartares, porém não as porás no teu vaso
Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako.
25 Quando entrares na seara do teu próximo, com a tua mão arrancarás as espigas; porém não meterás a foice na seara do teu próximo.
Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.