< 1 Timóteo 3 >

1 Esta é uma palavra fiel: Se alguém deseja o episcopado, excelente obra deseja.
Msemo huu ni wa kweli: mtu akitaka kuwa kiongozi katika kanisa, huyo anatamani kazi nzuri.
2 Convém pois que o bispo seja irrepreensível, marido de uma mulher, vigilante, sóbrio, honesto, hospitaleiro, apto para ensinar;
Basi, kiongozi wa kanisa anapaswa awe mtu asiye na lawama; anapaswa awe na mke mmoja tu, awe mwenye kiasi, nidhamu na utaratibu; ni lazima awe mkarimu na anayeweza kufundisha;
3 Não dado ao vinho, não espancador, não cobiçoso de torpe ganância, mas moderado, não contencioso, não avarento;
asiwe mlevi au mtu wa matata, bali awe mpole, apendaye amani; asiwe mtu wa kupenda fedha;
4 Que governe bem a sua própria casa, tendo seus filhos em sujeição, com toda a modéstia;
anapaswa awe mtu awezaye kuongoza vema nyumba yake, na kuwafanya watoto wake wawe watii kwa heshima yote.
5 (Porque, se alguém não sabe governar a sua própria casa, como terá cuidado da igreja de Deus?)
Maana kama mtu hawezi kuongoza vema nyumba yake, atawezaje kulitunza kanisa la Mungu?
6 Não neófito, para que, ensoberbecendo-se, não caia na condenação do diabo.
Mtu ambaye hajakomaa bado katika imani asifanywe kuwa kiongozi katika kanisa, asije akajaa majivuno na kuhukumiwa kama vile Ibilisi alivyohukumiwa.
7 Convém também que tenha bom testemunho dos que estão de fora, para que não caia em afronta, e no laço do diabo.
Anapaswa awe mwenye sifa njema kati ya watu walio nje ya kanisa, ili asije akalaumiwa na kuanguka katika mtego wa Ibilisi.
8 Da mesma sorte os diáconos sejam honestos, não de língua dobre não dados a muito vinho, não cobiçosos de torpe ganância;
Wasaidizi katika kanisa wanapaswa pia kuwa watu wenye tabia njema na wanyofu; wasiwe wanywaji mno wa divai au wenye tamaa ya fedha;
9 Tendo o mistério da fé em uma pura consciência.
wanapaswa kuzingatia kwa dhamiri njema ukweli wa ndani wa imani.
10 E também estes sejam primeiro provados, depois sirvam, se forem irrepreensíveis.
Ni lazima kwanza wathibitishwe, na wakionekana kuwa wanafaa, basi, watoe huduma yao.
11 Da mesma sorte as suas mulheres sejam honestas, não maldizentes, sóbrias e fieis em todas as coisas.
Wake zao wanapaswa pia kuwa na tabia njema, wasiowasengenya watu, wenye kiasi na waaminifu katika mambo yote.
12 Os diáconos sejam maridos de uma mulher, e governem bem a seus filhos e a suas próprias casas.
Msaidizi katika kanisa lazima awe na mke moja tu, na awezaye kuongoza vema watoto wake na nyumba yake.
13 Porque os que servirem bem, adquirirão para si um bom grau, e muita confiança na fé que há em Cristo Jesus.
Maana wasaidizi wanaofanya kazi yao vizuri hujipatia msimamo mzuri, na wanaweza kusema bila hofu juu ya imani yao katika Kristo Yesu.
14 Escrevo-te estas coisas, esperando ir vêr-te bem depressa;
Ninakuandikia barua hii nikiwa na matumaini ya kuja kwako hivi karibuni.
15 Mas, se tardar, para que saibas como convém andar na casa de Deus, que é a igreja de Deus vivo, a coluna e firmeza da verdade.
Lakini kama nikicheleweshwa, basi, barua hii itakufahamisha mwenendo tunaopaswa kuwa nao katika nyumba ya Mungu, ambayo ni kanisa la Mungu aliye hai, na ambalo ni nguzo na msingi wa ukweli.
16 E sem dúvida alguma grande é o mistério da piedade: Deus foi manifestado em carne, foi justificado em espírito, visto dos anjos, pregado aos gentios, crido no mundo, e recebido acima na glória.
Hakuna mashaka yoyote juu ya ukuu wa siri ya dini yetu: Alionekana katika umbo la kibinadamu alithibitishwa na Roho kuwa ni mwadilifu, akaonekana na malaika. Alihubiriwa kati ya mataifa, aliaminiwa popote ulimwenguni, akachukuliwa juu mbinguni katika utukufu.

< 1 Timóteo 3 >