< 1 Crônicas 11 >
1 Então todo o Israel se ajuntou a David em Hebron, dizendo: Eis que somos teus ossos e tua carne.
Israeli yote walimjia Daudi kwa pamoja huko Hebroni wakamwambia, “Sisi ni nyama yako na damu yako.
2 E também já de antes, sendo Saul ainda rei, eras tu o que fazias sair e entrar a Israel: também o Senhor teu Deus te disse: Tu apascentarás o meu povo Israel, e tu serás chefe sobre o meu povo Israel.
Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani, naye Bwana Mungu wako alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
3 Também vieram todos os anciãos de Israel ao rei, a Hebron, e David fez com eles aliança em Hebron, perante o Senhor: e ungiram a David rei sobre Israel, conforme a palavra do Senhor pelo ministério de Samuel.
Wazee wote wa Israeli walipokuwa wamewasili kwa Mfalme Daudi huko Hebroni, alifanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta awe mfalme wa Israeli, sawasawa na Bwana alivyoahidi kupitia kwa Samweli.
4 E partiu David e todo o Israel para Jerusalém, que é Jebus: porque ali estavam os jebuseus, moradores da terra.
Daudi na Waisraeli wote wakaenda Yerusalemu (ndio Yebusi). Nao Wayebusi walioishi humo
5 E disseram os moradores de Jebus a David: Tu não entrarás aqui. Porém David ganhou a fortaleza de Sião, que é a cidade de David.
wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu.” Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
6 Porque disse David: Qualquer que primeiro ferir os jebuseus será chefe e maioral. Então Joab, filho de Zeruia, subiu primeiro a ela; pelo que foi feito chefe.
Daudi alikuwa amesema, “Yeyote aongozaye mashambulizi dhidi ya Wayebusi, atakuwa jemadari mkuu.” Yoabu mwana wa Seruya akawa wa kwanza kukwea, naye akawa mkuu.
7 E David habitou na fortaleza; pelo que se chamou a cidade de David.
Daudi akafanya makao yake kwenye ngome, hivyo ukaitwa Mji wa Daudi.
8 E edificou a cidade ao redor, desde milo até ao circuito: e Joab renovou o resto da cidade.
Akajenga mji pande zote, kuanzia kwenye mito hadi kwenye ukuta kuzunguka, wakati huo huo Yoabu akajenga sehemu zingine zilizobaki za Yerusalemu.
9 E ia-se David cada vez mais aumentando e crescendo; porque o Senhor dos exércitos era com ele.
Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
10 E estes foram os chefes dos varões que David tinha, e que o apoiaram fortemente no seu reino, com todo o Israel, para o fazerem rei, conforme a palavra do Senhor, tocante a Israel.
Hawa ndio waliokuwa wakuu wa mashujaa wa Daudi: wao pamoja na Israeli wote wakauimarisha ufalme wake ili kuenea katika nchi yote, kama Bwana alivyoahidi.
11 E estes foram do número dos varões que David tinha: Jasobeam, hachmonita, o principal dos capitães, o qual, brandindo a sua lança contra trezentos, de uma vez os matou.
Hii ndio orodha ya mashujaa wa Daudi: Yashobeamu, Mhakmoni, alikuwa mkuu wa maafisa; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua katika pambano moja.
12 E, depois dele, Eleazar, filho de Dodó, o ahohita: ele estava entre os três varões.
Aliyefuata alikuwa Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
13 Este esteve com David em Pas-dammim, quando os philisteus ali se ajuntaram à peleja, e o pedaço de campo estava cheio de cevada: e o povo fugiu de diante dos philisteus.
Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pas-Damimu, wakati Wafilisti walikusanyika huko kwa ajili ya vita. Huko ambapo kulikuwa na shamba lililokuwa limejaa shayiri, vikosi vya Israeli vikawakimbia Wafilisti.
14 E puseram-se no meio daquele pedaço, e o defenderam, e feriram os philisteus; e obrou o Senhor um grande livramento.
Lakini Eleazari na Daudi wakasimama imara katikati ya lile shamba, nao wakalishindania na wakawaua Wafilisti. Naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
15 E três dos trinta chefes desceram à penha, a David, na caverna de Adullam: e o arraial dos philisteus estava acampado no vale de Rephaim.
Wakuu watatu miongoni mwa wale thelathini, walimwendea Daudi katika mwamba huko kwenye pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
16 E David estava então no lugar forte: e o alojamento dos philisteus estava então em Beth-lehem.
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
17 E desejou David, e disse: Quem me dará a beber da água do poço de Beth-lehem, que está junto à porta?
Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilichoko karibu na lango la Bethlehemu!”
18 Então aqueles três romperam pelo arraial dos philisteus, e tiraram água do poço de Beth-lehem, que estava à porta, e tomaram dela, e a trouxeram a David; porém David não a quis beber, mas a derramou ao Senhor,
Kwa hivyo wale watatu, wakapita katikati ya safu za Wafilisti, wakachota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
19 E disse: Nunca meu Deus permita que faça tal! beberia eu o sangue destes varões com as suas vidas? Pois com perigo das suas vidas a trouxeram. E ele não a quis beber: isto fizeram aqueles três varões.
Akasema, “Mungu apishie mbali kwamba nifanye hivi! Je kweli, niinywe damu ya watu hawa waliohatarisha maisha yao?” Kwa sababu walihatarisha maisha yao kuyaleta yale maji, Daudi hakukubali kuyanywa. Huo ndio uliokuwa ujasiri wa wale mashujaa watatu.
20 E também Abisai, irmão de Joab, foi chefe de três, o qual, brandindo a sua lança contra trezentos, os feriu: e teve nome entre os três.
Abishai, ndugu yake Yoabu ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300, ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
21 Dos três foi mais ilustre do que os outros dois, pelo que foi chefe deles; porém não chegou aos primeiros três.
Alitunukiwa heshima maradufu ya wale Watatu, akawa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
22 Também Benaias, filho de Joiada filho de um valente varão, grande em obras, de Kabseel: ele feriu a dois fortes leões de Moab; e também desceu, e feriu um leão dentro de uma cova, no tempo da neve.
Benaya, mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
23 Também feriu ele a um homem egípcio, homem de grande altura, de cinco côvados: e trazia o egípcio uma lança na mão, como o órgão do tecelão; mas desceu contra ele com uma vara, e arrancou a lança da mão do egípcio, e o matou com a sua própria lança
Alimuua Mmisri aliyekuwa na urefu kama dhiraa tano. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi mwake, Benaya alimwendea na rungu. Akamnyangʼanya Mmisri mkuki wake na kumuua nao.
24 Estas coisas fez Benaias, filho de Joiada; pelo que teve nome entre aqueles três varões.
Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
25 Eis que dos trinta foi ele o mais ilustre; contudo não chegou aos três: e David o pôs sobre os da sua guarda.
Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu: Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
26 E foram os varões dos exércitos: Asael, irmão de Joab, Elhanan, filho de Dodo, de Beth-lehem,
Wale watu mashujaa walikuwa: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
27 Sammoth, o harodita, Heles, o pelonita,
Shamothi Mharori, Helesi Mpeloni,
28 Ira, filho de Ikkes, o tekoita, Abiezer, o anathothita,
Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, Abiezeri kutoka Anathothi,
29 Sibbechai, o husathita, Ilai, o ahohita,
Sibekai Mhushathi, Ilai Mwahohi,
30 Maharai, o netophathita, Heled, filho de Baena, o netophathita,
Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi,
31 Ithai, filho de Ribai, de Gibeah, dos filhos de Benjamin, Benaias, o pirathonita,
Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini, Benaya Mpirathoni,
32 Hurai, do ribeiro de Gaas, Abiel, o arbathita,
Hurai kutoka mabonde ya Gaashi, Abieli Mwaribathi,
33 Asmaveth, o baharumita, Eliahba, o saalbonita.
Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
34 Dos filhos de Hasem, o gizonita: Jonathan, filho de Sage, o hararita,
wana wa Hashemu Mgiloni, Yonathani mwana wa Shagee Mharari,
35 Ahiam, filho de Sachar, o hararita, Eliphal, filho de Ur,
Ahiamu mwana wa Sakari Mharari, Elifale mwana wa Uru,
36 Hepher, o mecheratita, Ahias, o pelonita,
Heferi Mmekerathi, Ahiya Mpeloni,
37 Hesro, o carmelita, Naari, filho d'Esbai,
Hezro Mkarmeli, Naarai mwana wa Ezbai,
38 Joel, irmão de Nathan, Mibhar, filho de Geri,
Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri,
39 Zelek, o amonita, Nahrai, o berothita, escudeiro de Joab, filho de Zeruia,
Seleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
40 Ira, o ithrita, Gareb, o ithrita,
Ira Mwithiri, Garebu Mwithiri,
41 Urias, o hethita, Zabad, filho de Ahlai,
Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai,
42 Adina, filho de Siza, o rubenita, chefe dos rubenitas; todavia sobre ele havia trinta;
Adina mwana wa Shiza Mreubeni, ambaye alikuwa mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini,
43 Hanam, filho de Maacha, e Josaphat, o mithnita,
Hanani mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni,
44 Uzias, o astharathita, Sama e Jeiel, filhos de Hotham, o aroerita,
Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri,
45 Jediael, filho de Simri, e Joha, seu irmão, o tisita,
Yediaeli mwana wa Shimri, nduguye Yoha Mtizi,
46 Eliel, o mahavita, e Jeribai, e Joshavias, filhos d'Elnaam, e Ithma, o moabita,
Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu, Ithma Mmoabu,
47 Eliel, e Obed, e Jaasiel, e Mesobaia.
Elieli, na Obedi na Yaasieli Mmesobai.