< Salmos 96 >
1 Cantae ao Senhor um cantico novo, cantae ao Senhor toda a terra.
Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
2 Cantae ao Senhor, bemdizei o seu nome; annunciae a sua salvação de dia em dia.
Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
3 Annunciae entre as nações a sua gloria; entre todos os povos as suas maravilhas.
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
4 Porque grande é o Senhor, e digno de louvor, mais tremendo do que todos os deuses.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
5 Porque todos os deuses dos povos são idolos, mas o Senhor fez os céus.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
6 Gloria e magestade estão ante a sua face, força e formosura no seu sanctuario.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
7 Dae ao Senhor, ó familias dos povos, dae ao Senhor gloria e força.
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
8 Dae ao Senhor a gloria devida ao seu nome: trazei offerenda, e entrae nos seus atrios.
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
9 Adorae ao Senhor na belleza da sanctidade: tremei diante d'elle toda a terra.
Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
10 Dizei entre as nações que o Senhor reina: o mundo tambem se firmará para que se não abale: julgará os povos com rectidão.
Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
11 Alegrem-se os céus, e regozije-se a terra: brama o mar e a sua plenitude.
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
12 Alegre-se o campo com tudo o que ha n'elle: então se regozijarão todas as arvores do bosque,
mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
13 Ante a face do Senhor, porque vem, porque vem a julgar a terra: julgará o mundo com justiça e os povos com a sua verdade.
itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.