< Salmos 76 >

1 Conhecido é Deus em Judah: grande é o seu nome em Israel.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
2 E em Salem está o seu tabernaculo, e a sua morada em Sião.
Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
3 Ali quebrou as frechas do arco; o escudo, e a espada e a guerra (Selah)
Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
4 Tu és mais illustre, ó glorioso, do que os montes de preza.
Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
5 Os que são ousados de coração são despojados; dormiram o seu somno, e nenhum dos homens de força achou as suas mãos
Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
6 Á tua reprehensão, ó Deus de Jacob, carros e cavallos são lançados n'um somno profundo.
Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
7 Tu, tu és terrivel; e quem subsistirá á tua vista, uma vez que te irares?
Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
8 Desde os céus fizeste ouvir o teu juizo; a terra tremeu e se aquietou,
Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
9 Quando Deus se levantou para fazer juizo, para livrar a todos os mansos da terra (Selah)
wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
10 Porque a colera do homem redundará em teu louvor; o restante da colera tu o restringirás.
Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
11 Fazei votos, e pagae ao Senhor, vosso Deus: tragam presentes, os que estão em redor d'elle, áquelle que é tremendo.
Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
12 Elle ceifará o espirito dos principes: é tremendo para com os reis da terra.
Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.

< Salmos 76 >