< Salmos 57 >
1 Tem misericordia de mim, ó Deus, tem misericordia de mim, porque a minha alma confia em ti; e na sombra das tuas azas me abrigo, até que passem as calamidades.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
2 Clamarei ao Deus altissimo, ao Deus que por mim tudo executa.
Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
3 Elle enviará desde os céus, e me salvará do desprezo d'aquelle que procurava devorar-me (Selah) Deus enviará a sua misericordia e a sua verdade.
Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
4 A minha alma está entre leões, e eu estou entre aquelles que estão abrazados, filhos dos homens, cujos dentes são lanças e frechas, e a sua lingua espada afiada.
Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
5 Sê exaltado, ó Deus, sobre os céus; seja a tua gloria sobre toda a terra.
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 Armaram uma rede aos meus passos; a minha alma está abatida; cavaram uma cova diante de mim, porém elles mesmos cairam no meio d'ella (Selah)
Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
7 Preparado está o meu coração, ó Deus, preparado está o meu coração; cantarei, e direi psalmos.
Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
8 Desperta, gloria minha, desperta, alaude e harpa; eu mesmo despertarei ao romper da alva.
Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
9 Louvar-te-hei, Senhor, entre os povos; eu te cantarei entre as nações.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
10 Pois a tua misericordia é grande até aos céus, e a tua verdade até ás nuvens.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
11 Sê exaltado, ó Deus, sobre os céus; e seja a tua gloria sobre toda a terra.
Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.