< Salmos 36 >
1 A prevaricação do impio diz no intimo do seu coração: Não ha temor de Deus perante os seus olhos.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
2 Porque em seus olhos se lisongeia, até que a sua iniquidade se descubra ser detestavel.
Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
3 As palavras da sua bocca são malicia e engano: deixou de entender e de fazer o bem.
Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
4 Projecta a malicia na sua cama; põe-se no caminho que não é bom: não aborrece o mal
Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
5 A tua misericordia, Senhor, está nos céus, e a tua fidelidade chega até ás mais excelsas nuvens.
Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
6 A tua justiça é como as grandes montanhas; os teus juizos são um grande abysmo; Senhor, tu conservas os homens e os animaes.
Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
7 Quão preciosa é, ó Deus, a tua benignidade, pelo que os filhos dos homens se abrigam á sombra das tuas azas.
Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
8 Elles se fartarão da gordura da tua casa, e os farás beber da corrente das tuas delicias;
Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
9 Porque em ti está o manancial da vida; na tua luz veremos a luz.
Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
10 Estende a tua benignidade sobre os que te conhecem, e a tua justiça sobre os rectos de coração.
Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
11 Não venha sobre mim o pé dos soberbos, e não me mova a mão dos impios.
Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
12 Ali caem os que obram a iniquidade; cairão, e não se poderão levantar.
Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!