< Salmos 29 >
1 Dae ao Senhor, ó filhos dos poderosos, dae ao Senhor gloria e força.
Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
2 Dae ao Senhor a gloria devida ao seu nome, adorae o Senhor na belleza da sanctidade.
Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
3 A voz do Senhor se ouve sobre as suas aguas; o Deus da gloria troveja; o Senhor está sobre as muitas aguas,
Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
4 A voz do Senhor é poderosa; a voz do Senhor é cheia de magestade.
Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
5 A voz do Senhor quebra os cedros; sim, o Senhor quebra os cedros do Libano.
Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
6 Elle os faz saltar como um bezerro; ao Libano e Sirion, como novos unicornios.
Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
7 A voz do Senhor separa as labaredas do fogo.
Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
8 A voz do Senhor faz tremer o deserto; o Senhor faz tremer o deserto de Kades.
Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
9 A voz do Senhor faz parir as cervas, e descobre as brenhas; e no seu templo cada um falla da sua gloria.
Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
10 O Senhor se assentou sobre o diluvio; o Senhor se assenta como Rei, perpetuamente.
Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
11 O Senhor dará força ao seu povo; o Senhor abençoará o seu povo com paz
Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.