< Salmos 22 >
1 Meu Deus, meu Deus, porque me desamparaste? porque te alongas do meu auxilio e das palavras do meu bramido?
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
2 Meu Deus, eu clamo de dia, e tu não me ouves; de noite, e não tenho socego.
Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
3 Porém tu és Sancto, o que habitas entre os louvores d'Israel.
Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
4 Em ti confiaram nossos paes; confiaram, e tu os livraste.
Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
5 A ti clamaram e escaparam; em ti confiaram, e não foram confundidos.
Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
6 Mas eu sou verme, e não homem, opprobrio dos homens e desprezado do povo.
Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
7 Todos os que vêem zombam de mim, arreganham os beiços e meneiam a cabeça, dizendo:
Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
8 Confiou no Senhor, que o livre; livre-o, pois n'elle tem prazer.
Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
9 Mas tu és o que me tiraste do ventre: fizeste-me esperar, estando aos peitos de minha mãe.
Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
10 Sobre ti fui lançado desde a madre; tu és o meu Deus desde o ventre de minha mãe.
Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
11 Não te alongues de mim, pois a angustia está perto, e não ha quem ajude.
Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
12 Muitos toiros me cercaram; fortes toiros de Bazan me rodearam.
Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
13 Abriram contra mim suas boccas, como um leão que despedaça e que ruge.
Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
14 Como agua me derramei, e todos os meus ossos se desconjuntaram: o meu coração é como cera, derreteu-se no meio das minhas entranhas.
Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
15 A minha força se seccou como um caco, e a lingua se me pega ao paladar: e me pozeste no pó da morte.
Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
16 Pois me rodearam cães: o ajuntamento de malfeitores me cercou, traspassaram-me as mãos e os pés.
Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
17 Poderia contar todos os meus ossos: elles o vêem e me contemplam.
Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
18 Repartem entre si os meus vestidos, e lançam sortes sobre a minha tunica.
Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
19 Mas tu, Senhor, não te alongues de mim: força minha, apressa-te em soccorrer-me.
Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
20 Livra-me a minha alma da espada, e a minha predilecta da força do cão.
Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
21 Salva-me da bocca do leão, sim, ouviste-me, desde as pontas dos unicornios.
Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
22 Então declararei o teu nome aos meus irmãos: louvar-te-hei no meio da congregação.
Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
23 Vós, que temeis ao Senhor, louvae-o; todos vós, semente de Jacob, glorificae-o; e temei-o todos vós, semente d'Israel.
Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
24 Porque não desprezou nem abominou a afflicção do afflicto, nem escondeu d'elle o seu rosto; antes, quando elle clamou, o ouviu.
Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
25 O meu louvor virá de ti na grande congregação: pagarei os meus votos perante os que o temem.
Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
26 Os mansos comerão e se fartarão; louvarão ao Senhor os que o buscam: o vosso coração viverá eternamente.
Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
27 Todos os limites da terra se lembrarão, e se converterão ao Senhor: e todas as gerações das nações adorarão perante a tua face.
Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
28 Porque o reino é do Senhor, e elle domina entre as nações.
kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
29 Todos os que na terra são gordos comerão e adorarão, e todos os que descem ao pó se prostrarão perante elle: e ninguem poderá reter viva a sua alma.
Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
30 Uma semente o servirá: será contada ao Senhor de geração em geração.
Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
31 Chegarão e annunciarão a sua justiça ao povo que nascer, porquanto elle o fez.
Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.