< Salmos 17 >
1 Ouve, Senhor, a justiça, attende ao meu clamor; dá ouvidos á minha oração, que não é feita com labios enganosos.
Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
2 Saia o meu juizo de diante do teu rosto; attendam os teus olhos á razão.
Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
3 Provaste o meu coração; visitaste-me de noite; examinaste-me, e nada achaste; propuz que a minha bocca não transgredirá.
Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
4 Quanto ao trato dos homens, pela palavra dos teus labios me guardei das veredas do destruidor.
Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
5 Dirige os meus passos nos teus caminhos, para que as minhas pégadas não vacillem.
Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
6 Eu te invoquei, ó Deus, pois me queres ouvir; inclina para mim os teus ouvidos, e escuta as minhas palavras.
Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
7 Faze maravilhosas as tuas beneficencias, ó tu que livras aquelles que em ti confiam dos que se levantam contra a tua mão direita.
Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
8 Guarda-me como á menina do olho, esconde-me debaixo da sombra das tuas azas,
Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
9 Dos impios que me opprimem, dos meus inimigos mortaes que me andam cercando.
kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
10 Na sua gordura se encerram, com a bocca fallam soberbamente.
Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
11 Teem-nos cercado agora nossos passos; e abaixaram os seus olhos para a terra;
Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
12 Parecem-se com o leão que deseja arrebatar a sua preza, e com o leãosinho que se põe em esconderijos.
Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
13 Levanta-te, Senhor, detem-n'a, derriba-o, livra a minha alma do impio, com a espada tua,
Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
14 Dos homens que são a tua mão, Senhor, dos homens do mundo, cuja porção está n'esta vida, e cujo ventre enches do teu thesouro occulto: estão fartos de filhos e dão os seus sobejos ás suas creanças.
Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
15 Emquanto a mim, contemplarei a tua face na justiça; satisfazer-me-hei da tua similhança quando acordar.
Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.