< Salmos 135 >
1 Louvae ao Senhor. Louvae o nome do Senhor; louvae-o, servos do Senhor.
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 Vós que assistis na casa do Senhor, nos atrios da casa do nosso Deus.
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Louvae ao Senhor, porque o Senhor é bom: cantae louvores ao seu nome, porque é agradavel.
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 Porque o Senhor escolheu para si a Jacob, e a Israel para seu proprio thesouro.
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 Porque eu conheço que o Senhor é grande e que o nosso Deus está acima de todos os deuses.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 Tudo o que o Senhor quiz fez, nos céus e na terra, nos mares e em todos os abysmos.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 Faz subir os vapores das extremidades da terra; faz os relampagos para a chuva; produz os ventos dos seus thesouros.
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 O que feriu os primogenitos do Egypto, desde os homens até ás bestas.
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 O que enviou signaes e prodigios no meio de ti, ó Egypto, contra Pharaó e contra os seus servos.
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 O que feriu muitas nações, e matou poderosos reis;
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 A Sehon, rei dos amorrheos, e a Og, rei de Basan, e a todos os reinos de Canaan.
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 E deu a sua terra em herança, em herança a Israel, seu povo.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 O teu nome, ó Senhor, dura perpetuamente; e a tua memoria, ó Senhor, de geração em geração.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 Pois o Senhor julgará o seu povo, e se arrependerá com respeito aos seus servos.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 Os idolos das nações são prata e oiro, obra das mãos dos homens.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 Teem bocca, mas não fallam; teem olhos, e não vêem.
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 Teem ouvidos, mas não ouvem, nem ha respiro algum nas suas boccas.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Similhantes a elles se tornem os que os fazem, e todos os que confiam n'elles.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Casa d'Israel, bemdizei ao Senhor; casa d'Aarão bemdizei ao Senhor.
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Casa de Levi, bemdizei ao Senhor: vós, os que temeis ao Senhor, louvae ao Senhor.
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Bemdito seja o Senhor desde Sião, que habita em Jerusalem. Louvae ao Senhor.
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.