< Salmos 104 >

1 Bemdize, ó alma minha, ao Senhor: Senhor Deus meu, tu és magnificentissimo, estás vestido de gloria e de magestade.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 Elle se cobre de luz como de um vestido, estende os céus como uma cortina.
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 Põe nas aguas as vigas das suas camaras; faz das nuvens o seu carro, anda sobre as azas do vento.
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 Faz dos seus anjos espiritos, dos seus ministros um fogo abrazador.
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 Lançou os fundamentos da terra, para que não vacille em tempo algum.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 Tu a cobres com o abysmo, como com um vestido: as aguas estavam sobre os montes.
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 Á tua reprehensão fugiram: á voz do teu trovão se apressaram.
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 Sobem aos montes, descem aos valles, até ao logar que para ellas fundaste.
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 Termo lhes pozeste, que não ultrapassarão, para que não tornem mais a cobrir a terra.
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 Tu, que fazes sair as fontes nos valles, as quaes correm entre os montes.
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 Dão de beber a todo o animal do campo; os jumentos montezes matam a sua sêde.
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 Junto d'ellas as aves do céu terão a sua habitação, cantando entre os ramos.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 Elle rega os montes desde as suas camaras: a terra se farta do fructo das suas obras.
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 Faz crescer a herva para as bestas, e a verdura para o serviço do homem, para fazer sair da terra o pão,
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 E o vinho que alegra o coração do homem, e o azeite que faz reluzir o seu rosto, e o pão que fortalece o coração do homem.
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 As arvores do Senhor fartam-se de seiva, os cedros do Libano que elle plantou,
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 Onde as aves se aninham: emquanto á cegonha, a sua casa é nas faias.
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 Os altos montes são um refugio para as cabras montezes, e as rochas para os coelhos.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 Designou a lua para as estações: o sol conhece o seu occaso.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 Ordenas a escuridão, e faz-se noite, na qual saem todos os animaes da selva.
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 Os leõesinhos bramam pela preza, e de Deus buscam o seu sustento.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 Nasce o sol e logo se acolhem, e se deitam nos seus covis.
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 Então sae o homem á sua obra e ao seu trabalho, até á tarde.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 Ó Senhor, quão variadas são as tuas obras! todas as coisas fizeste com sabedoria; cheia está a terra das tuas riquezas.
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 Assim é este mar grande e muito espaçoso, onde ha reptis sem numero, animaes pequenos e grandes.
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 Ali andam os navios; e o leviathan que formaste para n'elle folgar.
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 Todos esperam de ti, que lhes dês o seu sustento em tempo opportuno.
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 Dando-lh'o tu, elles o recolhem; abres a tua mão, e se enchem de bens.
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 Escondes o teu rosto, e ficam perturbados: se lhes tiras o folego, morrem, e voltam para o seu pó.
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 Envias o teu Espirito, e são creados, e assim renovas a face da terra.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 A gloria do Senhor durará para sempre: o Senhor se alegrará nas suas obras.
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 Olhando elle para a terra, ella treme; tocando nos montes, logo fumegam.
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 Cantarei ao Senhor emquanto eu viver; cantarei louvores ao meu Deus, emquanto eu tiver existencia.
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 A minha meditação ácerca d'elle será suave: eu me alegrarei no Senhor.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 Desçam da terra os peccadores, e os impios não sejam mais. Bemdize, ó alma minha, ao Senhor. Louvae ao Senhor.
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.

< Salmos 104 >