< Provérbios 27 >

1 Não presumas do dia d'ámanhã, porque não sabes o que parirá o dia.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
2 Louve-te o estranho, e não a tua bocca, o estrangeiro e não os teus labios.
Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
3 Pesada é a pedra, e a areia é carregada; porém a ira do insensato é mais pesada do que ellas ambas.
Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
4 Cruel é o furor e a impetuosa ira, mas quem parará perante a inveja?
Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
5 Melhor é a reprehensão aberta do que o amor encoberto.
Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
6 Fieis são as feridas feitas pelo que ama, mas os beijos do que aborrece são enganosos.
Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
7 A alma farta piza o favo de mel, mas á alma faminta todo o amargo é doce.
Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
8 Qual é a ave que vagueia do seu ninho, tal é o homem que anda vagueando do seu logar.
Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
9 O oleo e o perfume alegram o coração: assim a doença do amigo d'alguem com o conselho cordial.
Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
10 Não deixes a teu amigo, nem ao amigo de teu pae, nem entres na casa de teu irmão no dia da tua adversidade: melhor é o visinho de perto do que o irmão ao longe.
Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
11 Sê sabio, filho meu, e alegra o meu coração; para que tenha alguma coisa que responder áquelle que me desprezar.
Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
12 O avisado vê o mal, e esconde-se; mas os simples passam e pagam a pena.
Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
13 Quando alguem fica por fiador do estranho, toma-lhe tu a sua roupa; e o penhora pela estranha.
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
14 O que bemdiz ao seu amigo em alta voz, madrugando pela manhã, por maldição se lhe contará.
Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
15 O gotejar continuo no dia de grande chuva, e a mulher contenciosa, uma e outra são similhantes.
Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
16 Todos os que a esconderem esconderão o vento: e o oleo da sua dextra clama.
Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
17 Como o ferro com o ferro se aguça, assim o homem aguça o rosto do seu amigo.
Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
18 O que guarda a figueira comerá do seu fructo; e o que attenta para seu senhor, será honrado.
Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
19 Como na agua o rosto corresponde ao rosto, assim o coração do homem ao homem.
Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
20 Como o inferno e a perdição nunca se fartam, assim os olhos do homem nunca se fartam. (Sheol h7585)
Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol h7585)
21 Como o crisol é para a prata, e o forno para o oiro, assim se prova o homem pelos louvores.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
22 Ainda quando pizares o tolo com uma mão de gral entre grãos de cevada pilada, não se irá d'elle a sua estulticia.
Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
23 Procura conhecer o estado das tuas ovelhas: põe o teu coração sobre o gado.
Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
24 Porque o thesouro não dura para sempre: ou durará a corôa de geração em geração?
Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
25 Quando se mostrar a herva, e apparecerem os renovos, então ajunta as hervas dos montes.
Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
26 Os cordeiros serão para te vestires, e os bodes para o preço do campo.
wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
27 E a abastança do leite das cabras para o teu sustento, para sustento da tua casa, e para sustento das tuas creadas.
Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.

< Provérbios 27 >