< Provérbios 24 >
1 Não tenhas inveja dos homens malignos, nem desejes estar com elles,
Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
2 Porque o seu coração medita a rapina, e os seus labios fallam a malicia.
kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
3 Com a sabedoria se edifica a casa, e com a intelligencia se estabelece:
Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
4 E pelo conhecimento se encherão as camaras de todas as substancias preciosas e deleitaveis.
kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
5 E o varão sabio é forte, e o varão de conhecimento consolida a força.
Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
6 Porque com conselhos prudentes tu farás a guerra; e ha victoria na multidão dos conselheiros.
kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
7 É demasiadamente alta para o tolo toda a sabedoria; na porta não abrirá a sua bocca.
Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
8 A'quelle que cuida em fazer mal mestre de maus intentos o chamarão.
Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
9 O pensamento do tolo é peccado, e é abominavel aos homens o escarnecedor.
Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
10 Se te mostrares frouxo no dia da angustia, a tua força será estreita.
Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
11 Livra aos que estão tomados para a morte, e aos que levam para matança, se os poderes retirar.
Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
12 Se disseres: Eis que o não sabemos: porventura aquelle que pondera os corações não o entenderá? e aquelle que attenta para a tua alma não o saberá? porque pagará ao homem conforme a sua obra.
Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
13 Come mel, meu filho, porque é bom, e o favo de mel é doce ao teu paladar.
Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
14 Tal será o conhecimento da sabedoria para a tua alma: se a achares, haverá para ti galardão, e não será cortada a tua expectação.
Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
15 Não espies a habitação do justo, ó impio, nem assoles a sua camara.
Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
16 Porque sete vezes cairá o justo, e se levantará; mas os impios tropeçarão no mal
Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
17 Quando cair o teu inimigo, não te alegres, nem quando tropeçar se regozije o teu coração.
Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
18 Para que o Senhor o não veja, e seja mau aos seus olhos, e desvie d'elle a sua ira.
Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
19 Não te indignes ácerca dos malfeitores, nem tenhas inveja dos impios,
Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
20 Porque o maligno não terá galardão, e a lampada dos impios se apagará.
kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
21 Teme ao Senhor, filho meu, e ao rei, e não te entremettas com os que buscam mudança.
Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
22 Porque de repente se levantará a sua perdição, e a ruina d'elles ambos quem a sabe?
kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
23 Tambem estes são proverbios dos sabios: Ter respeito a pessoas no juizo não é bom.
Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
24 O que disser ao impio: Justo és: os povos o amaldiçoarão, as nações o detestarão.
Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
25 Mas para os que o reprehenderem haverá delicias, e sobre elles virá a benção do bem
Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
26 Beijados serão os labios do que responde com palavras rectas.
Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
27 Prepara de fóra a tua obra, e apparelha-a no campo, e então edifica a tua casa.
Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
28 Não sejas testemunha sem causa contra o teu proximo; porque enganarias com os teus beiços?
Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
29 Não digas: Como elle me fez a mim, assim o farei eu a elle: pagarei a cada um segundo a sua obra.
Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
30 Passei pelo campo do preguiçoso, e junto á vinha do homem falto de entendimento;
Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
31 E eis que toda estava cheia de cardos, e a sua superficie coberta d'ortigas, e a sua parede de pedra estava derribada.
miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
32 O que tendo eu visto, o tomei no coração, e, vendo-o, recebi instrucção.
Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
33 Um pouco de somno, adormecendo um pouco; encruzando as mãos outro pouco, para estar deitado.
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
34 Assim te sobrevirá a tua pobreza como um caminhante, e a tua necessidade como um homem armado.
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.