< Provérbios 23 >

1 Quando te assentares a comer com um governador, attenta bem para o que se te poz diante,
Unapoketi kula pamoja na mtawala, angalia kwa uangalifu kilichopo mbele yako,
2 E põe uma faca á tua garganta, se és homem de grande appetite.
na kama ni mtu unayependa kula chakula sana weka kisu kooni.
3 Não cubices os seus manjares gostosos, porque são pão de mentiras.
Usitamani vinono vyake maana ni chakula cha uongo.
4 Não te cances para enriqueceres; dá de mão á tua prudencia.
Usifanye kazi sana ili kupata mali; uwe na busara ya kutosha ili ujue wakati wa kuacha.
5 Porventura fitarás os teus olhos n'aquillo que não é nada? porque certamente se fará azas e voará ao céu como a aguia
Je utaruhusu macho yako yaangaze juu yake? Itaondoka, maana itawaa mabawa kama tai na kuruka angani.
6 Não comas o pão d'aquelle que tem o olho maligno, nem cubices os seus manjares gostosos.
Usile chakula cha yule mwenye jicho baya- na usiwe na shauku ya vinono vyake,
7 Porque, como imaginou na sua alma, te dirá: Come e bebe; porém o seu coração não estará comtigo.
maana ni mtu mwenye kuhesabu gharama ya chakula. “Kula na kunywa!” anakuambia, lakini moyo wake haupo pamoja nawe.
8 Vomitarias o bocado que comeste, e perderias as tuas suaves palavras.
Utatapika kiasi kidogo ulichokula na utakuwa umepoteza sifa zako njema.
9 Não falles aos ouvidos do tolo, porque desprezará a sabedoria das tuas palavras.
Usiongee katika usikivu wa mpumbavu, maana atadharau hekima ya maneno yako.
10 Não removas os limites antigos, nem entres nas herdades dos orphãos,
Usihamishe jiwe la mpaka wa kale au kunyang'anya mashamba ya yatima,
11 Porque o seu redemptor é o Forte, que pleiteará a sua causa contra ti.
maana Mkombozi wao ni imara na atatetea kesi yao dhidi yako.
12 Applica á disciplina o teu coração, e os teus ouvidos ás palavras do conhecimento.
Elekeza moyo wako katika mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
13 Não retires a disciplina da creança, quando a fustigares com a vara; nem por isso morrerá.
Usizuie kuadilisha mtoto, maana ukimchapa kwa fimbo, hatakufa.
14 Tu a fustigarás com a vara, e livrarás a sua alma do inferno. (Sheol h7585)
Ni wewe unayepaswa kumchapa kwa fimbo na kuikoa nafsi yake kuzimu. (Sheol h7585)
15 Filho meu, se o teu coração fôr sabio, alegrar-se-ha o meu coração, sim, o meu proprio,
Mwanangu, kama moyo wako una busara, basi moyo wangu utafurahi pia;
16 E exultarão os meus rins, quando os teus labios fallarem coisas rectas.
sehemu zangu ndani kabisa zitafurahi sana midomo yako inaponena haki.
17 Não inveje aos peccadores o teu coração; antes sê no temor do Senhor todo o dia
Usiruhusu moyo wako kuwahusudu wenye dhambi, lakini endelea kumcha Yehova siku zote.
18 Porque devéras ha um bom fim: não será cortada a tua expectação.
Hakika tumaini lako halitaondolewa na siku zako za hapo baadaye.
19 Ouve tu, filho meu, e sê sabio, e dirige no caminho o teu coração.
Sikia- wewe! - mwanangu, na uwe mwenye busara na uelekeze moyo wako katika njia.
20 Não estejas entre os beberrões de vinho, nem entre os comilões de carne.
Usishirikiane pamoja na walevi, au pamoja na walaji wa nyama walafi,
21 Porque o beberrão e o comilão empobrecerão; e a somnolencia faz trazer os vestidos rotos.
maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
22 Ouve a teu pae, que te gerou, e não desprezes a tua mãe, quando vier a envelhecer.
Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
23 Compra a verdade, e não a vendas: a sabedoria, e a disciplina, e a prudencia.
Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.
24 Grandemente se regozijará o pae do justo, e o que gerar a um sabio se alegrará n'elle.
Baba yake mwenye haki atafurahia sana, na yule amzaaye mtoto mwenye busara atamfurahia.
25 Alegrem-se teu pae e tua mãe, e regozije-se a que te gerou.
Mfurahishe baba yako na mama yako na yule aliyekuzaa afurahie.
26 Dá-me, filho meu, o teu coração, e os teus olhos observem os meus caminhos.
Mwanangu, nipe moyo wako na macho yako yachunguze njia zangu.
27 Porque cova profunda é a prostituta, e poço estreito a estranha.
Maana malaya ni shimo refu, na mke wa mume mwingine ni kisima chembamba.
28 Tambem ella, como um salteador, se põe a espreitar, e multiplica entre os homens os iniquos.
Anavizia kama mnyang'anyi na huongeza idadi ya wadanganyifu miongoni mwa wanadamu.
29 Para quem são os ais? para quem os pezares? para quem as pelejas? para quem as queixas? para quem as feridas sem causa? e para quem os olhos vermelhos?
Nani mwenye taabu? Nani mwenye huzuni? Nani mwenye mapigano? Nani mwenye malalamiko? Nani mwenye majeraha bila sababu? Nani mwenye macho mekundu?
30 Para os que se demoram perto do vinho, para os que andam buscando bebida misturada.
Ni wale ambao huzengea kwenye mvinyo, wale wanaojaribu kuchanganya mvinyo.
31 Não olhes para o vinho quando se mostra vermelho, quando resplandece no copo e se escoa suavemente.
Usiutazame mvinyo ukiwa mwekundu, wakati unametameta kwenye kikombe na kutelemka kwa uraini.
32 No seu fim morderá como a cobra, e como o basilisco picará.
Mwisho wake unauma kama nyoka na sumu yake kama kifutu.
33 Os teus olhos olharão para as mulheres estranhas, e o teu coração fallará perversidades.
Macho yako yataona vitu vigeni na moyo wako utatamka vitu vya ukaidi.
34 E serás como o que dorme no meio do mar, e como o que dorme no topo do mastro.
Utakuwa kama anayelala kwenye bahari au anayelala juu ya mlingoti. “
35 E dirás: Espancaram-me, e não me doeu; maçaram-me, e não o senti; quando virei a despertar? ainda tornarei a buscal-a outra vez
Wamenipiga,” utasema, “lakini sikuumia. Wamenichapa, lakini sikuwa na hisia. Nitaamka lini? Nitatafuta kinywaji kingine.”

< Provérbios 23 >