< Provérbios 21 >

1 Como ribeiros d'aguas, assim é o coração do rei na mão do Senhor; a tudo quanto quer o inclina.
Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
2 Todo o caminho do homem é recto aos seus olhos, mas o Senhor pondera os corações.
Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
3 Fazer justiça e juizo é mais acceito ao Senhor do que lhe offerecer sacrificio.
Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
4 Altivez dos olhos, e inchação de coração, e a lavoura dos impios é peccado.
Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
5 Os pensamentos do diligente tendem só á abundancia, porém os de todo o apressado tão sómente á pobreza.
Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
6 Trabalhar por ajuntar thesouro com lingua falsa é uma vaidade impellida d'aquelles que buscam a morte.
Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
7 As rapinas dos impios os virão a destruir, porquanto recusam fazer a justiça.
Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
8 O caminho do homem é todo perverso e estranho, porém a obra do puro é recta.
Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
9 Melhor é morar n'um canto do terraço, do que com a mulher contenciosa, e isso em casa em que mais companhia haja.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
10 A alma do impio deseja o mal: o seu proximo lhe não agrada aos seus olhos.
Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
11 Castigado o escarnecedor, o simples se torna sabio; e, ensinado o sabio, recebe o conhecimento.
Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
12 Prudentemente considera o justo a casa do impio, quando Deus transtorna os impios para o mal.
Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
13 O que tapa o seu ouvido ao clamor do pobre elle tambem clamará e não será ouvido.
Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
14 O presente que se dá em segredo abate a ira, e a dadiva no seio a grande indignação.
Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
15 O fazer justiça é alegria para o justo, mas espanto para os que obram a iniquidade.
Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
16 O homem, que anda errado do caminho do entendimento, na congregação dos mortos repousará.
Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
17 Necessidade padecerá o que ama a galhofa: o que ama o vinho e o azeite nunca enriquecerá.
Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
18 O resgate do justo é o impio; o do recto o iniquo.
Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
19 Melhor é morar n'uma terra deserta do que com a mulher contenciosa e iracunda.
Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
20 Thesouro desejavel e azeite ha na casa do sabio, mas o homem insensato o devora.
Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
21 O que segue a justiça e a beneficencia achará a vida, a justiça e a honra.
Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
22 Á cidade dos fortes sobe o sabio, e derruba a força da sua confiança.
Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
23 O que guarda a sua bocca e a sua lingua, guarda das angustias a sua alma.
Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
24 O soberbo e presumido, zombador é seu nome: trata com indignação e soberba.
Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
25 O desejo do preguiçoso o mata, porque as suas mãos recusam trabalhar.
Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
26 Todo o dia deseja coisas de cubiçar, mas o justo dá, e nada retem.
Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
27 O sacrificio dos impios é abominação: quanto mais offerecendo-o com intenção maligna?
Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
28 A testemunha mentirosa perecerá, porém o homem que ouve com constancia fallará.
Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
29 O homem impio endurece o seu rosto, mas o recto considera o seu caminho.
Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
30 Não ha sabedoria, nem intelligencia, nem conselho contra o Senhor.
Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
31 O cavallo prepara-se para o dia da batalha, porém do Senhor vem a victoria.
Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.

< Provérbios 21 >