< Levítico 6 >

1 Fallou mais o Senhor a Moysés, dizendo:
Bwana akamwambia Mose:
2 Quando alguma pessoa peccar, e trespassar contra o Senhor, e negar ao seu proximo o que se lhe deu em guarda, ou o que depoz na sua mão, ou o roubo, ou o que retem violentamente ao seu proximo,
“Kama mtu yeyote akitenda dhambi, naye si mwaminifu kwa Bwana kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa, au kimeachwa chini ya utunzaji wake, au kimeibwa, au kama akimdanganya,
3 Ou que achou o perdido, e o negar com falso juramento, ou fizer alguma outra coisa de todas em que o homem costuma peccar;
au akiokota mali iliyopotea na akadanganya, au kuapa kwa uongo, au kama akitenda dhambi yoyote ambayo watu waweza kuitenda;
4 Será pois que, porquanto peccou e ficou culpado, restituirá o roubo que roubou, ou o retido que retem violentamente, ou o deposito que lhe foi dado em guarda, ou o perdido que achou,
wakati akitenda dhambi hizo na kuwa mwenye hatia, ni lazima arudishe kile alichokuwa amekiiba au amekichukua kwa dhuluma, au alichokuwa amekabidhiwa, au mali iliyokuwa imepotea akaipata,
5 Ou tudo aquillo sobre que jurou falsamente; e o restituirá no seu cabedal, e ainda sobre isso accrescentará o quinto; áquelle de quem é o dará no dia de sua expiação.
au chochote alichokuwa amekiapia kwa uongo. Lazima akirudishe kikamilifu, na aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, vyote ampe mwenye mali siku ile anapeleka sadaka yake ya hatia.
6 E a sua expiação trará ao Senhor: um carneiro sem mancha do rebanho, conforme á tua estimação, para expiação da culpa, trará ao sacerdote:
Kisha kama adhabu lazima amletee kuhani, yaani kwa Bwana, kama sadaka yake ya hatia, kondoo dume asiye na dosari na mwenye thamani kamili kutoka kundi lake.
7 E o sacerdote fará expiação por ella diante do Senhor, e será perdoada de qualquer de todas as coisas que fez, sendo culpada n'ellas.
Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa kwa kosa lolote katika mambo hayo aliyoyatenda yaliyomfanya kuwa na hatia.”
8 Fallou mais o Senhor a Moysés, dizendo:
Bwana akamwambia Mose:
9 Dá ordem a Aarão e a seus filhos, dizendo: Esta é a lei do holocausto; o holocausto será queimado sobre o altar toda a noite até á manhã, e o fogo do altar arderá n'elle.
“Mpe Aroni na wanawe agizo hili: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa itabaki kwenye moto juu ya madhabahu usiku kucha, mpaka asubuhi, nao moto lazima uwe unaendelea kuwaka juu ya madhabahu.
10 E o sacerdote vestirá a sua veste de linho, e vestirá as calças de linho sobre a sua carne, e levantará a cinza, quando o fogo houver consumido o holocausto sobre o altar, e a porá junto ao altar.
Kisha kuhani atavaa mavazi yake ya kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani mwilini wake, na aondoe majivu ya sadaka ya kuteketezwa ambayo moto umeteketeza juu ya madhabahu, na kuyaweka kando ya madhabahu.
11 Depois despirá as suas vestes, e vestirá outras vestes: e levará a cinza fóra do arraial para um logar limpo.
Kisha atayavua mavazi haya na kuvaa mengine, naye achukue yale majivu nje ya kambi na kuyapeleka mahali palipo safi kwa kawaida ya ibada.
12 O fogo pois sobre o altar arderá n'elle, não se apagará; mas o sacerdote accenderá lenha n'elle cada manhã, e sobre elle porá em ordem o holocausto, e sobre elle queimará a gordura das offertas pacificas.
Moto ulio juu ya madhabahu lazima uwe unaendelea kuwaka, kamwe usizimike. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni na kupanga sadaka ya kuteketezwa juu ya moto, na kuteketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake.
13 O fogo arderá continuamente sobre o altar; não se apagará.
Moto lazima uendelee kuwaka juu ya madhabahu mfululizo, kamwe usizimike.
14 E esta é a lei da offerta de manjares: um dos filhos de Aarão a offerecerá perante o Senhor diante do altar,
“‘Haya ndiyo masharti ya sadaka ya nafaka: Wana wa Aroni wataileta mbele za Bwana, mbele za madhabahu.
15 E d'ella tomará o seu punho cheio da flôr de farinha da offerta e do seu azeite, e todo o incenso que estiver sobre a offerta de manjares: então o accenderá sobre o altar, cheiro suave é isso, por ser memorial ao Senhor.
Kuhani atachukua konzi ya unga laini na mafuta, pamoja na uvumba wote ulioko juu ya sadaka ya nafaka, ateketeze sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
16 E o restante d'ella comerão Aarão e seus filhos: asmo se comerá no logar sancto, no pateo da tenda da congregação o comerão.
Aroni na wanawe watakula sehemu iliyobaki, lakini italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu, nao wataila kwenye ua wa Hema la Kukutania.
17 Levedado não se cozerá: sua porção é que lhes dei das minhas offertas queimadas: coisa sanctissima é, como a expiação do peccado e como a expiação da culpa.
Kamwe haitaokwa na chachu; nimewapa kama fungu lao la sadaka iliyotolewa kwangu kwa moto. Ni takatifu sana, kama vile ilivyo sadaka ya dhambi na ya hatia.
18 Todo o macho entre os filhos d'Aarão comerá d'ella: estatuto perpetuo será para as vossas gerações das offertas queimadas do Senhor; tudo o que tocar n'ellas será sancto.
Kila mwanaume mzao wa Aroni aweza kuila. Ni fungu lake la kawaida la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto kwa vizazi vijavyo. Chochote kinachozigusa kitakuwa kitakatifu.’”
19 Fallou mais o Senhor a Moysés, dizendo:
Tena Bwana akamwambia Mose,
20 Esta é a offerta d'Aarão e de seus filhos, que offerecerão ao Senhor no dia em que fôr ungido: a decima parte d'um epha de flôr de farinha pela offerta de manjares continua; a metade d'ella pela manhã, e a outra metade d'ella á tarde.
“Hii ni sadaka ambayo Aroni na wanawe wanapaswa kuleta kwa Bwana siku atakapotiwa mafuta: sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kama sadaka ya kawaida ya nafaka. Nusu yake ataitoa asubuhi na nusu nyingine jioni.
21 N'uma caçoila se fará com azeite; cosida a trarás; e os pedaços cosidos da offerta offerecerás em cheiro suave ao Senhor.
Iandae kwa mafuta kwenye kikaango; ilete ikiwa imechanganywa vizuri, na utoe hiyo sadaka ya nafaka ikiwa imevunjwa vipande vipande kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
22 Tambem o sacerdote, que de entre seus filhos fôr ungido em seu logar, fará o mesmo; por estatuto perpetuo seja, toda será queimada ao Senhor.
Mwanawe atakayeingia mahali pake kama kuhani aliyetiwa mafuta ndiye atakayeiandaa. Ni fungu la kawaida la Bwana, nalo litateketezwa kabisa.
23 Assim toda a offerta do sacerdote totalmente será queimada; não se comerá.
Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itateketezwa kabisa; kamwe haitaliwa.”
24 Fallou mais o Senhor a Moysés, dizendo:
Bwana akamwambia Mose,
25 Falla a Aarão e a seus filhos, dizendo: Esta é a lei da expiação do peccado: no logar onde se degola o holocausto se degolará a expiação do peccado perante o Senhor; coisa sanctissima é.
“Mwambie Aroni na wanawe: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi itachinjiwa mbele za Bwana mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, ni takatifu sana.
26 O sacerdote que a offerecer pelo peccado a comerá: no logar sancto se comerá, no pateo da tenda da congregação.
Kuhani anayeitoa ndiye atakayeikula; itakuliwa katika mahali patakatifu, katika ua wa Hema la Kukutania.
27 Tudo o que tocar a sua carne será sancto: se espargir alguem do seu sangue sobre o seu vestido, lavarás aquillo sobre o que caiu n'um logar sancto.
Chochote kitakachogusa nyama yoyote ya hiyo sadaka kitakuwa kitakatifu, na kama hiyo damu itadondokea juu ya vazi, lazima uifulie mahali patakatifu.
28 E o vaso de barro em que fôr cosida será quebrado; porém, se fôr cosida n'um vaso de cobre, esfregar-se-ha e lavar-se-ha na agua.
Chungu cha udongo kitakachopikiwa nyama lazima kivunjwe, lakini kama imepikiwa kwenye chombo cha shaba, chombo hicho kitasuguliwa na kusuuzwa kwa maji.
29 Todo o macho entre os sacerdotes a comerá: coisa sanctissima é.
Kila mwanaume katika familia ya kuhani aweza kula nyama hiyo; ni takatifu sana.
30 Porém nenhuma expiação de peccado, cujo sangue se traz á tenda da congregação, para expiar no sanctuario, se comerá: no fogo será queimada.
Lakini kila sadaka ya dhambi ambayo damu yake imeletwa ndani ya Hema la Kukutania kufanya upatanisho katika Mahali Patakatifu kamwe haitaliwa; lazima iteketezwe.

< Levítico 6 >