< 5 >

1 Chama agora; ha alguem que te responda? e para qual dos sanctos te virarás?
“Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
2 Porque a ira destroe o louco; e o zelo mata o tolo.
Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
3 Bem vi eu o louco lançar raizes; porém logo amaldiçoei a sua habitação.
Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
4 Seus filhos estão longe da salvação; e são despedaçados ás portas, e não ha quem os livre.
Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
5 A sua sega a devora o faminto, e até d'entre os espinhos a tira; e o salteador traga a sua fazenda.
Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
6 Porque do pó não procede a afflicção, nem da terra brota o trabalho.
Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
7 Mas o homem nasce para o trabalho, como as faiscas das brazas se levantam para voarem.
Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
8 Porém eu buscaria a Deus; e a Elle dirigiria a minha falla.
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
9 Elle faz coisas tão grandiosas, que se não podem esquadrinhar; e tantas maravilhas, que se não podem contar.
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10 Que dá a chuva sobre a terra, e envia aguas sobre os campos,
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11 Para pôr aos abatidos n'um logar alto: e para que os enlutados se exaltem na salvação.
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
12 Elle aniquila as imaginações dos astutos, para que as suas mãos não possam levar coisa alguma a effeito.
Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
13 Elle apanha os sabios na sua propria astucia; e o conselho dos perversos se precipita.
Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
14 Elles de dia encontrem as trevas; e ao meio dia andem como de noite, ás apalpadelas.
Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
15 Porém ao necessitado livra da espada, e da bocca d'elles, e da mão do forte.
Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
16 Assim ha esperança para o pobre; e a iniquidade tapa a sua bocca.
Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
17 Eis que bemaventurado é o homem a quem Deus castiga; pois não desprezes o castigo do Todo-poderoso.
“Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
18 Porque elle faz a chaga, e elle mesmo a liga: elle fere, e as suas mãos curam.
Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
19 Em seis angustias te livrará; e na setima o mal te não tocará.
Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
20 Na fome te livrará da morte; e na guerra da violencia da espada.
Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
21 Do açoite da lingua estarás encoberto; e não temerás a assolação, quando vier.
Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
22 Da assolação e da fome te rirás, e os animaes da terra não temerás.
Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
23 Porque até com as pedras do campo terás a tua alliança; e os animaes do campo serão pacificos comtigo.
Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
24 E saberás que a tua tenda está em paz; e visitarás a tua habitação, e não falharás.
Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
25 Tambem saberás que se multiplicará a tua semente e a tua posteridade como a herva da terra.
Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
26 Na velhice virás á sepultura, como se recolhe o feixe de trigo a seu tempo.
Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
27 Eis que isto já o havemos inquirido, e assim é; ouve-o, e medita n'isso para teu bem.
“Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”

< 5 >