< 40 >

1 Respondeu mais o Senhor a Job e disse:
Bwana akamwambia Ayubu:
2 Porventura o contender contra o Todo-poderoso é ensinar? quem quer reprehender a Deus, responda a estas coisas.
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Então Job respondeu ao Senhor, e disse:
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 Eis que sou vil; que te responderia eu? a minha mão ponho na minha bocca.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 Já uma vez tenho fallado, porém mais não responderei: ou ainda duas vezes, porém não proseguirei.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Então o Senhor respondeu a Job desde a tempestade, e disse:
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 Ora, pois, cinge os teus lombos como varão; eu te perguntarei a ti, e tu ensina-me.
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 Porventura tambem farás tu vão o meu juizo? ou tu me condemnarás, para te justificares?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Ou tens braço como Deus? ou podes trovejar com voz como a sua?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Orna-te pois com excellencia e alteza; e veste-te de magestade e de gloria.
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Derrama os furores da tua ira, e attenta para todo o soberbo, e abate-o.
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Olha para todo o soberbo, e humilha-o, e atropella os impios no seu logar.
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Esconde-os juntamente no pó: ata-lhes os rostos em occulto.
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Então tambem eu a ti confessarei que a tua mão direita te haverá livrado.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Vês aqui a Behemoth, que eu fiz comtigo, que come a herva como o boi.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 Eis que a sua força está nos seus lombos, e o seu poder no umbigo do seu ventre.
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 Quando quer, move a sua cauda como cedro: os nervos das suas coxas estão entretecidos.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 Os seus ossos são como coxas de bronze: a sua ossada é como barras de ferro.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 Elle é obra prima dos caminhos de Deus: o que o fez lhe apegou a sua espada.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 Em verdade os montes lhe produzem pasto, onde todos os animaes do campo folgam.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 Deita-se debaixo das arvores sombrias, no esconderijo das canas e da lama.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 As arvores sombrias o cobrem, com sua sombra: os salgueiros do ribeiro o cercam.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 Eis que um rio trasborda, e elle não se apressa, confiando que o Jordão possa entrar na sua bocca.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 Podel-o-hiam porventura caçar á vista de seus olhos? ou com laços lhe furar os narizes?
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

< 40 >