< 37 >

1 Sobre isto tambem treme o meu coração, e salta do seu logar.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Attentamente ouvi o movimento da sua voz, e o sonido que sae da sua bocca.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 Elle o envia por debaixo de todos os céus, e a sua luz até aos confins da terra.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 Depois d'isto brama com grande voz, troveja com a sua alta voz; e, ouvida a sua voz, não tarda com estas coisas.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 Com a sua voz troveja Deus maravilhosamente: faz grandes coisas, e nós as não comprehendemos.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 Porque á neve diz: Está sobre a terra: como tambem ao aguaceiro e á sua forte chuva.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 Elle sella as mãos de todo o homem, para que conheça todos os homens de sua obra.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 E as bestas entram nos seus esconderijos e ficam nas suas cavernas.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 Da recamara sae o pé de vento, e dos ventos dispersivos o frio.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 Pelo assopro de Deus se dá a geada, e as largas aguas se endurecem.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Tambem com a humidade carrega as grossas nuvens, e esparge a nuvem da sua luz.
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 Então ellas, segundo o seu prudente conselho, se tornam pelas espheras, para que façam tudo quanto lhes ordena sobre a superficie do mundo habitavel,
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 Seja que por vara, ou para a sua terra, ou por beneficencia as faça vir.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 A isto, ó Job, inclina os teus ouvidos: põe-te em pé, e considera as maravilhas de Deus.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Porventura sabes tu quando Deus considera n'ellas, e faz resplandecer a lua da sua nuvem?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Tens tu noticia do equilibrio das grossas nuvens e das maravilhas de aquelle que é perfeito nos conhecimentos,
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 Ou de como os teus vestidos aquecem, quando do sul ha calma sobre a terra?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 Ou estendeste com elle os céus, que estão firmes como espelho fundido?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Ensina-nos o que lhe diremos; porque nós nada poderemos pôr em boa ordem, por causa das trevas.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Ou ser-lhe-hia contado, quando eu assim fallasse? dir-lhe-ha alguem isso? pois será devorado.
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 E agora se não pode olhar para o sol, quando resplandece nos céus; passando e purificando-os o vento.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 O esplendor de oiro vem do norte: pois em Deus ha uma tremenda magestade.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 Ao Todo-poderoso não podemos alcançar; grande é em potencia; porém a ninguem opprime em juizo e grandeza de justiça.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Por isso o temem os homens: elle não respeita aos sabios de coração.
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< 37 >