< 3 >

1 Depois d'isto abriu Job a sua bocca, e amaldiçoou o seu dia.
Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
2 E Job respondeu, e disse:
Kisha akasema:
3 Pereça o dia em que nasci, e a noite em que se disse: Foi concebido um homem!
“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
4 Converta-se aquelle dia em trevas; e Deus de cima não tenha cuidado d'elle, nem resplandeça sobre elle a luz.
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
5 Contaminem-n'o as trevas e a sombra de morte; habitem sobre elle nuvens: a escuridão do dia o espante!
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
6 A escuridão tome aquella noite, e não se goze entre os dias do anno, e não entre no numero dos mezes!
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
7 Ah que solitaria seja aquella noite, e suave musica não entre n'ella!
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
8 Amaldiçoem-n'a aquelles que amaldiçoam o dia, que estão promptos para levantar o seu pranto.
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
9 Escureçam-se as estrellas do seu crepusculo; que espere a luz, e não venha: e não veja as pestanas dos olhos da alva!
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
10 Porque não fechou as portas do ventre; nem escondeu dos meus olhos a canceira?
kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
11 Porque não morri eu desde a madre? e em saindo do ventre, não expirei?
“Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
12 Porque me receberam os joelhos? e porque os peitos, para que mamasse?
Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
13 Porque já agora jazera e repousara; dormiria, e então haveria repouso para mim.
Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
14 Com os reis e conselheiros da terra, que se edificavam casas nos logares assolados,
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
15 Ou com os principes que tinham oiro, que enchiam as suas casas de prata,
pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
16 Ou como aborto occulto, não existiria: como as creanças que não viram a luz.
Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
17 Ali os maus cessam de perturbar: e ali repousam os cançados.
Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
18 Ali os presos juntamente repousam, e não ouvem a voz do exactor:
Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
19 Ali está o pequeno e o grande, e o servo fica livre de seu senhor.
Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
20 Porque se dá luz ao miseravel, e vida aos amargosos d'animo?
“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
21 Que esperam a morte, e não se acha: e cavam em busca d'ella mais do que de thesouros occultos:
wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
22 Que d'alegria saltam, e exultam, achando a sepultura:
ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
23 Ao homem, cujo caminho é occulto, e a quem Deus o encobriu?
Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
24 Porque antes do meu pão vem o meu suspiro: e os meus gemidos se derramam como agua.
Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
25 Porque o temor que temo me veiu: e o que receiava me aconteceu.
Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
26 Nunca estive descançado, nem soceguei, nem repousei, mas veiu sobre mim a perturbação.
Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”

< 3 >