< Tiago 5 >

1 Eia pois agora vós, ricos, chorae e pranteae, por vossas miserias, que sobre vós hão de vir.
Na sasa sikilizeni enyi matajiri! Lieni na kuomboleza kwa sababu ya taabu zitakazowajieni.
2 As vossas riquezas estão apodrecidas, e os vossos vestidos estão comidos da traça.
Mali zenu zimeoza, na nguo zenu zimeliwa na nondo.
3 O vosso oiro e a vossa prata se enferrujaram; e a sua ferrugem dará testemunho contra vós, e comerá como fogo a vossa carne. Enthesourastes para os ultimos dias.
Dhahabu yenu na fedha vimeota kutu, na kutu hiyo itakuwa ushahidi dhidi yenu, nayo itakula miili yenu kama vile moto. Ninyi mmejilundikia mali katika siku hizi za mwisho!
4 Eis que o jornal dos trabalhadores que ceifaram as vossas terras, e o qual por vós foi diminuido, clama; e os clamores dos que ceifaram entraram nos ouvidos do Senhor dos exercitos.
Hamkuwalipa mishahara watumishi waliofanya kazi katika mashamba yenu. Sikilizeni malalamiko yao! Kilio cha hao wanaovuna mashamba yenu kimefika masikioni mwa Bwana, Mwenye Nguvu.
5 Deliciosamente vivestes sobre a terra, e vos deleitastes: cevastes os vossos corações, como n'um dia de matança.
Mmeishi duniani maisha ya kujifurahisha na ya anasa. Mmejinenepesha tayari kwa siku ya kuchinjwa.
6 Condemnastes e matastes o justo; elle não vos resistiu.
Mmemhukumu na kumwua mtu asiye na hatia, naye hakuwapigeni.
7 Sêde pois, irmãos, pacientes até á vinda do Senhor. Eis que o lavrador espera o precioso fructo da terra, aguardando-o com paciencia, até que receba a chuva temporã e serodia.
Basi, ndugu zangu, muwe na subira mpaka Bwana atakapokuja. Tazameni mkulima anavyongoja kwa subira mimea yake itoe mavuno mazuri. Yeye hungojea kwa subira mvua za masika na za vuli.
8 Sêde vós tambem pacientes, fortalecei os vossos corações; porque já a vinda do Senhor está proxima.
Nanyi pia mnapaswa kuwa na subira; imarisheni mioyo yenu, maana siku ya kuja kwake Bwana inakaribia.
9 Irmãos, não vos queixeis uns contra os outros, para que não sejaes condemnados. Eis que o juiz está á porta.
Ndugu zangu, msinung'unikiane ninyi kwa ninyi msije mkahukumiwa na Mungu. Hakimu yu karibu, tayari kuingia.
10 Meus irmãos, tomae por exemplo de afflicção e paciencia os prophetas que fallaram em nome do Senhor.
Ndugu, mkitaka kuona mfano wa subira na uvumilivu katika mateso, fikirini juu ya manabii ambao walinena kwa jina la Bwana.
11 Eis que temos por bemaventurados os que soffrem. Ouvistes qual foi a paciencia de Job, e vistes o fim que o Senhor lhe deu; porque o Senhor é muito misericordioso e piedoso.
Tunawaita hao wenye heri kwa sababu walivumilia. Mmesikia habari za uvumilivu wa Yobu, na mnajua jinsi Bwana alivyomtendea mwishoni. Maana Bwana amejaa huruma na rehema.
12 Porém, sobretudo, meus irmãos, não jureis, nem pelo céu, nem pela terra, nem façaes qualquer outro juramento; mas que a vossa palavra seja sim, sim, e não, não; para que não caiaes em condemnação.
Zaidi ya hayo yote, ndugu zangu, msiape kwa mbingu, wala kwa dunia, wala kwa kitu kingine chochote. Semeni “Ndiyo” kama maana yenu ni ndiyo, na “La” kama maana yenu ni la, na hapo hamtahukumiwa na Mungu.
13 Está alguem entre vós afflicto? ore. Está alguem contente? psalmodie.
Je, pana mtu yeyote miongoni mwenu aliye na shida? Anapaswa kusali. Je, yuko mwenye furaha? Anapaswa kuimba nyimbo za sifa.
14 Está alguem entre vós doente? chame os anciãos da egreja, e orem sobre elle, ungindo-o com azeite em nome do Senhor;
Je, yuko mgonjwa kati yenu? Anapaswa kuwaita wazee wa kanisa, nao watamwombea na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.
15 E a oração da fé salvará o doente, e o Senhor o levantará; e, se houver commettido peccados, ser-lhe-hão perdoados.
Wakiomba kwa imani mgonjwa ataponyeshwa; Bwana atampatia nafuu, na dhambi alizotenda zitaondolewa.
16 Confessae as vossas culpas uns aos outros, e orae uns pelos outros para que sareis: a oração efficaz do justo pode muito.
Basi, ungamanianeni dhambi zenu, na ombeaneni, ili mpate kuponywa. Sala ya mtu mwema ina nguvu ya kutenda mengi.
17 Elias era homem sujeito ás mesmas paixões que nós, e, orando, pediu que não chovesse, e, por tres annos e seis mezes, não choveu sobre a terra.
Eliya alikuwa binadamu kama sisi. Aliomba kwa moyo mvua isinyeshe, nayo haikunyesha nchini kwa muda wa miaka mitatu na miezi sita.
18 E orou outra vez, e o céu deu chuva, e a terra produziu o seu fructo.
Kisha akaomba tena, mvua ikanyesha kutoka angani na nchi ikatoa mazao yake.
19 Irmãos, se algum de entre vós se tem desviado da verdade, e algum o converter,
Ndugu zangu, mmoja wenu akipotoka kuhusu ukweli, na mwingine akamrudisha,
20 Saiba que aquelle que fizer converter do erro do seu caminho um peccador salvará da morte uma alma, e cobrirá uma multidão de peccados.
fahamuni kwamba, huyo anayemrudisha mwenye dhambi kutoka njia yake ya upotovu, ataiokoa roho yake kutoka kifo, na dhambi nyingi zitaondolewa.

< Tiago 5 >