< Tiago 2 >

1 Meus irmãos, não tenhaes a fé de nosso Senhor Jesus Christo, Senhor da gloria, em accepção de pessoas.
Ndugu zangu, mkiwa mnamwamini Bwana Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwabague watu kamwe.
2 Porque, se no vosso ajuntamento entrar algum homem com annel de oiro no dedo, com vestidos preciosos, e entrar tambem algum pobre com vestido sordido,
Tuseme mtu mmoja ambaye amevaa pete ya dhahabu na mavazi nadhifu anaingia katika mkutano wenu, na papo hapo akaingia mtu maskini aliyevaa mavazi machafu.
3 E attentardes para o que traz o vestido precioso, e lhe disserdes: Assenta-te tu aqui n'um logar de honra; e disserdes ao pobre: Tu, fica ahi em pé, ou assenta-te abaixo do meu estrado;
Ikiwa mtamstahi zaidi yule aliyevaa mavazi ya kuvutia na kumwambia: “Keti hapa mahali pazuri,” na kumwambia yule maskini: “Wewe, simama huko,” au “Keti hapa sakafuni miguuni pangu,”
4 Porventura não fizestes differença dentro de vós mesmos, e não vos fizestes juizes de maus pensamentos?
je, huo si ubaguzi kati yenu? Je, na huo uamuzi wenu haujatokana na fikira mbaya?
5 Ouvi, meus amados irmãos: Porventura não escolheu Deus aos pobres d'este mundo para serem ricos na fé, e herdeiros do reino que promette aos que o amam?
Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni! Mungu amechagua watu ambao ni maskini katika ulimwengu huu ili wapate kuwa matajiri katika imani na kupokea Utawala aliowaahidia wale wanaompenda.
6 Porém vós deshonrastes o pobre. Porventura não vos opprimem os ricos, e não vos arrastam aos tribunaes?
Lakini ninyi mnawadharau watu maskini! Je, matajiri si ndio wanaowakandamizeni na kuwapeleka mahakamani?
7 Porventura não blasphemam elles o bom nome que sobre vós foi invocado?
Je, si haohao wanaolitukana hilo jina lenu zuri mlilopewa?
8 Todavia, se cumprirdes, conforme a Escriptura, a lei real: Amarás a teu proximo como a ti mesmo, bem fazeis.
Kama mnaitimiza ile sheria ya Utawala kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Mpende binadamu mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe”, mtakuwa mnafanya vema kabisa.
9 Porém, se fazeis accepção de pessoas, commetteis peccado, e sois redarguidos pela lei como transgressores.
Lakini mkiwabagua watu, basi, mwatenda dhambi, nayo Sheria inawahukumu ninyi kuwa mna hatia.
10 Porque qualquer que guardar toda a lei, e deslisar em um só ponto, é culpado de todos.
Anayevunja amri mojawapo ya Sheria, atakuwa na hatia ya kuivunja Sheria yote.
11 Porque aquelle que disse: Não commetterás adulterio, tambem disse: Não matarás. Se tu pois não commetteres adulterio, porém matares, estás feito transgressor da lei
Maana yuleyule aliyesema: “Usizini,” alisema pia “Usiue”. Kwa hiyo, hata ikiwa hukuzini lakini umeua, wewe umeivunja Sheria.
12 Assim fallae, e assim obrae, como devendo ser julgados pela lei da liberdade.
Basi, semeni na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria iletayo uhuru.
13 Porque o juizo virá sem misericordia sobre aquelle que não fez misericordia; e a misericordia gloría-se contra o juizo.
Maana, Mungu hatakuwa na huruma atakapomhukumu mtu asiyekuwa na huruma. Lakini huruma hushinda hukumu.
14 Meus irmãos, que aproveita se alguem disser que tem fé, e não tiver as obras? Porventura a fé pode salval-o?
Ndugu zangu, kuna faida gani mtu kusema ana imani, lakini haonyeshi kwa vitendo? Je, hiyo imani yawezaje kumwokoa?
15 E, se o irmão ou a irmã estiverem nús, e tiverem falta de mantimento quotidiano,
Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula.
16 E algum de vós lhe disser: Ide em paz, aquentae-vos, e fartae-vos; e lhe não derdes as coisas necessarias para o corpo, que proveito virá d'ahi?
Yafaa kitu gani ninyi kuwaambia hao: “Nendeni salama mkaote moto na kushiba,” bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?
17 Assim tambem a fé, se não tiver as obras, está morta em si mesma.
Vivyo hivyo, imani peke yake bila matendo imekufa.
18 Porém dirá alguem: Tu tens a fé, e eu tenho as obras: mostra-me a tua fé pelas tuas obras, e eu te mostrarei a minha fé pelas minhas obras.
Lakini mtu anaweza kusema: “Wewe unayo imani, mimi ninayo matendo!” Haya! Nionyeshe jinsi mtu anavyoweza kuwa na imani bila matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.
19 Tu crês que ha um só Deus: fazes bem; tambem os demonios o crêem, e estremecem.
Je, wewe unaamini kwamba yuko Mungu mmoja? Sawa! Lakini hata pepo huamini hilo, na hutetemeka kwa hofu.
20 Mas, ó homem vão, queres tu saber que a fé sem as obras está morta?
Mpumbavu wee! Je, wataka kuonyeshwa kwamba imani bila matendo imekufa?
21 Porventura o nosso pae Abrahão não foi justificado pelas obras, quando offereceu sobre o altar o seu filho Isaac?
Je, Abrahamu baba yetu alipataje kukubalika mbele yake Mungu? Kwa matendo yake, wakati alipomtoa mwanae Isaka sadaka juu ya madhabahu.
22 Bem vês que a fé cooperou com as suas obras, e que a fé foi aperfeiçoada pelas obras.
Waona basi, kwamba imani yake iliandamana na matendo yake; imani yake ilikamilishwa kwa matendo yake.
23 E cumpriu-se a Escriptura, que diz: E creu Abrahão em Deus, e foi-lhe isso imputado a justiça, e foi chamado o amigo de Deus.
Hivyo yakatimia yale Maandiko Matakatifu yasemayo: “Abrahamu alimwamini Mungu na kwa imani yake akakubaliwa kuwa mtu mwadilifu; na hivyo Abrahamu akaitwa rafiki wa Mungu.”
24 Vedes então que o homem é justificado pelas obras, e não sómente pela fé.
Mnaona basi, kwamba mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa matendo yake na si kwa imani peke yake.
25 E de egual modo Rahab, a meretriz, não foi tambem justificada pelas obras, quando recolheu os emissarios, e os despediu por outro caminho?
Ilikuwa vivyo hivyo kuhusu yule malaya Rahabu; yeye alikubaliwa kuwa mwadilifu kwa sababu aliwapokea wale wapelelezi na kuwasaidia waende zao kwa kupitia njia nyingine.
26 Porque, assim como o corpo sem o espirito está morto, assim tambem a fé sem as obras está morta.
Basi, kama vile mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo imani bila matendo imekufa.

< Tiago 2 >