< Isaías 10 >

1 Ai dos que ordenam ordenanças injustas, e dos que prescrevem trabalho aos escrivães.
Ole wao wawekao sheria zisizo za haki, kwa wale watoao amri za kuonea,
2 Para desviarem aos pobres do seu direito, e para arrebatarem o direito dos afflictos do meu povo, para despojarem as viuvas e para roubarem os orphãos!
kuwanyima maskini haki zao na kuzuilia haki za watu wangu walioonewa, kuwafanya wajane mawindo yao na kuwanyangʼanya yatima.
3 Mas que fareis vós-outros no dia da visitação, e da assolação, que ha de vir de longe? a quem vos refugiareis para obter soccorro, e onde deixareis a vossa gloria?
Mtafanya nini siku ya kutoa hesabu, wakati maafa yatakapokuja kutoka mbali? Mtamkimbilia nani awape msaada? Mtaacha wapi mali zenu?
4 Sem que cada um se abata entre as prezas, e caia entre os mortos? Com tudo isto a sua ira se não apartou, mas ainda está estendida a sua mão.
Hakutasalia kitu chochote, isipokuwa kujikunyata miongoni mwa mateka, au kuanguka miongoni mwa waliouawa. Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali, mkono wake bado umeinuliwa juu.
5 Ai da Assyria! a vara da minha ira: porque a minha indignação é o bordão nas suas mãos.
“Ole kwa Ashuru, fimbo ya hasira yangu, ambaye mkononi mwake ana rungu ya ghadhabu yangu!
6 Envial-o-hei contra uma nação hypocrita, e contra o povo do meu furor lhe darei ordem, para que lhe roube o roubo, e lhe despoje o despojo, e o ponha para ser pisado aos pés, como a lama das ruas:
Ninamtuma dhidi ya taifa lisilomjua Mungu, ninamtuma dhidi ya taifa linalonikasirisha, kukamata mateka na kunyakua nyara, pia kuwakanyaga chini kama matope ya barabarani.
7 Ainda que elle não cuide assim, nem o seu coração assim o imagine: antes no seu coração intentará destruir e desarraigar nações não poucas.
Lakini hili silo analokusudia, hili silo alilo nalo akilini; kusudi lake ni kuangamiza, kuyakomesha mataifa mengi.
8 Porque diz: Porventura todos os meus principes não são elles reis?
Maana asema, ‘Je, wafalme wote si majemadari wangu?
9 Não é Calno como Carchemis? não é Hamath como Arphad? e Samaria como Damasco?
Je, Kalno hakutendwa kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi, nayo Samaria si kama Dameski?
10 Como a minha mão achou os reinos dos idolos, ainda que as suas imagens de vulto fossem melhores do que as de Jerusalem e de que as de Samaria.
Kama vile mkono wangu ulivyotwaa falme za sanamu, falme ambazo vinyago vyao vilizidi vile vya Yerusalemu na Samaria:
11 Porventura como fiz a Samaria e aos seus idolos, não faria eu tambem assim a Jerusalem e aos seus idolos?
je, nisiishughulikie Yerusalemu na sanamu zake kama nilivyoshughulikia Samaria na vinyago vyake?’”
12 Porque acontecerá que, havendo o Senhor acabado toda a sua obra no monte de Sião e em Jerusalem, então visitarei o fructo da arrogante grandeza do coração do rei da Assyria e a pompa da altivez dos seus olhos.
Bwana atakapokuwa amemaliza kazi yake yote dhidi ya Mlima Sayuni na Yerusalemu, atasema, “Nitamwadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya majivuno ya ukaidi wa moyo wake na kutazama kwa macho yenye dharau.”
13 Porquanto disse: Com a força da minha mão o fiz, e com a minha sabedoria, porque sou entendido: e terei os limites dos povos, e roubei a sua provisão, e como valente abati aos moradores.
Kwa kuwa anasema: “‘Kwa nguvu za mkono wangu nimefanya hili, kwa hekima yangu, kwa sababu nina ufahamu. Niliondoa mipaka ya mataifa, niliteka nyara hazina zao, kama yeye aliye shujaa niliwatiisha wafalme wao.
14 E achou a minha mão as riquezas dos povos como a um ninho, e como se ajuntam os ovos deixados, assim eu ajuntei a toda a terra, e não houve quem movesse a aza, ou abrisse a bocca, ou chilrasse.
Kama mtu atiavyo mkono kwenye kiota, ndivyo mkono wangu ulivyochukua utajiri wa mataifa; kama watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya nchi zote; wala hakuna hata mmoja aliyepiga bawa au kufungua kinywa chake kutoa mlio.’”
15 Porventura gloriar-se-ha o machado contra o que corta com elle? ou presumirá a serra contra o que puxa por ella? como se o bordão movesse aos que o levantam, ou a vara se levantasse como não sendo pau?
Je, shoka laweza kujigamba kuwa na nguvu zaidi kuliko yule anayelitumia, au msumeno kujisifu dhidi ya yule anayeutumia? Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua yeye aichukuaye, au mkongojo ungemwinua mwenye kuutumia!
16 Pelo que o Senhor, o Senhor dos Exercitos, enviará magreza entre os seus gordos, e debaixo da sua gloria accenderá incendio, como incendio de fogo.
Kwa hiyo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatuma ugonjwa wa kudhoofisha kwa askari wake walio hodari, katika fahari yake moto utawaka kama mwali wa moto.
17 Porque a Luz d'Israel virá a ser por fogo e o seu Sancto por labareda, que abraze e consuma os seus espinheiros e as suas sarças n'um dia.
Nuru ya Israeli itakuwa moto, Aliye Mtakatifu wao mwali wa moto; katika siku moja utaunguza na kuteketeza miiba na michongoma yake.
18 Tambem consumirá a gloria da sua brenha, e do seu campo fertil, desde a alma até á carne, e será como quando o porta-bandeira se desmaia.
Fahari ya misitu yake na mashamba yenye rutuba utateketeza kabisa, kama vile mtu mgonjwa adhoofikavyo.
19 E o resto das arvores da sua brenha será tão pouco em numero, que um menino as possa escrever.
Nayo miti inayobaki katika misitu yake itakuwa michache sana hata mtoto mdogo angeweza kuihesabu.
20 E acontecerá n'aquelle dia que os residuos d'Israel, e os escapados da casa de Jacob, nunca mais se estribarão sobre o que os feriu: antes se estribarão verdadeiramente sobre o Senhor, o Sancto d'Israel.
Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Bwana Aliye Mtakatifu wa Israeli.
21 Os residuos se converterão, os residuos, digo, de Jacob, ao Deus forte.
Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu.
22 Porque ainda que o teu povo, ó Israel, seja como a areia do mar, todavia só um resto d'elle se converterá: já a destruição está determinada, trasbordando em justiça.
Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki.
23 Porque determinada já a destruição, o Senhor Jehovah dos Exercitos a executará no meio de toda esta terra.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote.
24 Pelo que assim diz o Senhor Jehovah dos Exercitos: Não temas, povo meu, que habitas em Sião, á Assyria, quando te ferir com a vara, e contra ti levantar o seu bordão ao modo dos egypcios,
Kwa hiyo, hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Enyi watu wangu mkaao Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya.
25 Porque d'aqui a bem pouco se cumprirão a minha indignação e a minha ira, para os consumir.
Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”
26 Porque o Senhor dos Exercitos levantará um açoite contra elle, qual a matança de Midian junto á rocha d'Oreb, e qual a sua vara sobre o mar, que levantará ao modo dos egypcios.
Bwana Mwenye Nguvu Zote atawachapa kwa mjeledi, kama alivyowapiga Wamidiani katika mwamba wa Orebu, naye atainua fimbo yake juu ya maji, kama alivyofanya huko Misri.
27 E acontecerá, no mesmo dia, que tirará a sua carga do teu hombro, e o seu jugo do teu pescoço: e o jugo será despedaçado por amor do ungido.
Katika siku hiyo mzigo wao utainuliwa kutoka mabegani mwenu, na nira yao kutoka shingoni mwenu; nira itavunjwa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
28 Já vem chegando a Aiath, já vae passando por Migron, e em Michmas lança a sua bagagem.
Wanaingia Ayathi, wanapita katikati ya Migroni, wanahifadhi mahitaji huko Mikmashi.
29 Já vão passando o vau, já se alojam em Geba: já Rama treme, e Gibeah de Saul vae fugindo.
Wanavuka kivukoni, nao wanasema, “Tutapiga kambi huko Geba usiku kucha.” Rama inatetemeka; Gibea ya Sauli inakimbia.
30 Grita altamente com a tua voz, ó filha de Gallim! ouve ó Lais! ó tu pobre Anathoth.
Piga kelele, ee Binti Galimu! Sikiliza, ee Laisha! Maskini Anathothi!
31 Já Madmena se foi, os moradores de Gebim vão fugindo em bandos.
Madmena inakimbia; watu wa Gebimu wanajificha.
32 Ainda um dia parará em Nob: moverá a sua mão contra o monte da filha de Sião, o outeiro de Jerusalem.
Siku hii ya leo watasimama Nobu; watatikisa ngumi zao kwa mlima wa Binti Sayuni, kwa kilima cha Yerusalemu.
33 Porém eis-que o Senhor Jehovah dos Exercitos decotará os ramos com violencia, e os de alta estatura serão cortados, e os altivos serão abatidos.
Tazama, Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.
34 E cortará com o ferro a espessura da brenha, e o Libano cairá á mão de um poderoso.
Atakata vichaka vya msitu kwa shoka; Lebanoni itaanguka mbele zake yeye Mwenye Nguvu.

< Isaías 10 >