< Ezequiel 46 >
1 Assim diz o Senhor Jehovah: A porta do atrio interior, que olha para o oriente, estará fechada os seis dias que são de trabalho; porém no dia de sabbado ella se abrirá; tambem no dia da lua nova se abrirá.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Lango la ukumbi wa ndani linaloelekea upande wa mashariki litakuwa linafungwa kwa siku sita za juma, ila siku ya Sabato na siku ya Mwezi Mwandamo litafunguliwa.
2 E o principe entrará pelo caminho do vestibulo da porta, por fóra, e estará em pé na hombreira da porta; e os sacerdotes prepararão o seu holocausto, e os seus sacrificios pacificos, e elle se prostrará no umbral da porta, e sairá; porém a porta não se fechará até á tarde.
Mkuu anayetawala ataingia kupitia baraza ya njia ya lango la ukumbi na kusimama karibu na nguzo ya lango. Makuhani watatoa sadaka za mkuu anayetawala za kuteketezwa na sadaka za amani. Mkuu anayetawala atasujudu kwenye kizingiti cha njia ya lango, kisha atatoka nje, lakini lango halitafungwa mpaka jioni.
3 E o povo da terra se prostrará á entrada da mesma porta, nos sabbados e nas luas novas, diante do Senhor.
Siku za Sabato na za Mwezi mwandamo watu wote wa nchi wataabudu mbele za Bwana penye lile ingilio la ile njia.
4 E o holocausto, que o principe offerecerá ao Senhor, será, no dia de sabbado, seis cordeiros sem mancha e um carneiro sem mancha.
Sadaka ya kuteketezwa aletazo mkuu anayetawala kwa Bwana siku ya Sabato itakuwa ni wana-kondoo sita na kondoo dume mmoja, wote wasiwe na dosari.
5 E a offerta de manjares será um epha para cada carneiro; e para cada cordeiro, a offerta de manjares será um dom da sua mão; e de azeite um hin para cada epha.
Sadaka ya nafaka inayotolewa pamoja na huyo kondoo dume itakuwa efa moja na sadaka ya nafaka inayotolewa na hao wana-kondoo itakuwa kiasi apendacho mtu pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
6 Mas no dia da lua nova será um bezerro, sem mancha; e seis cordeiros e um carneiro, elles serão sem mancha.
Siku ya mwezi mwandamo atatoa fahali mchanga, wana-kondoo sita na kondoo dume, wote wasiwe na dosari.
7 E preparará por offerta de manjares um epha para o bezerro e um epha para o carneiro, mas para os cordeiros, conforme o que alcançar a sua mão; e um hin de azeite para um epha.
Atatoa kuwa sadaka ya nafaka efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja na kondoo dume mmoja na pamoja na wana-kondoo kama atakavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
8 E, quando entrar o principe, entrará pelo caminho do vestibulo da porta, e sairá pelo mesmo caminho.
Wakati mkuu anayetawala aingiapo, atapitia kwenye baraza ya njia ya lango, naye atatoka nje kwa njia hiyo hiyo.
9 Mas, quando vier o povo da terra perante a face do Senhor nas solemnidades, aquelle que entrar pelo caminho da porta do norte, para adorar, sairá pelo caminho da porta do sul; e aquelle que entrar pelo caminho da porta do sul sairá pelo caminho da porta do norte: não tornará pelo caminho da porta por onde entrou, mas sairá pela outra que está opposta.
“‘Wakati watu wa nchi wanapokuja mbele za Bwana katika sikukuu zilizoamriwa, yeyote aingiaye kwa lango la kaskazini kuabudu atatoka nje kwa lango la kusini na yeyote aingiaye kwa lango la kusini atatoka nje kwa lango la kaskazini. Hakuna mtu yeyote atakayerudi kwa kupitia lango lile aliloingilia, lakini kila mmoja atatoka nje kwa lango linalokabili lile aliloingilia.
10 E o principe no meio d'elles entrará, quando elles entrarem, e, saindo elles, sairão todos.
Mkuu anayetawala atakuwa miongoni mwao, akiingia nao ndani wanapoingia, naye atatoka nao nje wanapotoka.
11 E nas festas e nas solemnidades será a offerta de manjares um epha para o bezerro, e um epha para o carneiro, mas para os cordeiros um dom da sua mão; e de azeite um hin para um epha.
“‘Kwenye sikukuu na kwenye sikukuu zilizoamriwa, sadaka ya nafaka itakuwa efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja pamoja na kondoo dume mmoja, pamoja na idadi ya wana-kondoo kama mtu apendavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
12 E, quando o principe fizer offerta voluntaria de holocaustos, ou de sacrificios pacificos, por offerta voluntaria ao Senhor, então lhe abrirão a porta que olha para o oriente, e fará o seu holocausto e os seus sacrificios pacificos, como houver feito no dia de sabbado; e sairá, e se fechará a porta depois d'elle sair
Mkuu anayetawala anapotoa sadaka ya hiari kwa Bwana, ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani, lango linaloelekea mashariki litafunguliwa kwa ajili yake. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka yake ya amani kama afanyavyo katika siku ya Sabato. Kisha atatoka nje, naye akiisha kutoka nje, lango litafungwa.
13 E prepararás um cordeiro d'um anno sem mancha, em holocausto ao Senhor, cada dia: todas as manhãs o prepararás.
“‘Kila siku utamtoa mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiyekuwa na dosari kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, utaitoa kila siku asubuhi.
14 E, por offerta de manjares farás juntamente com elle, todas as manhãs, a sexta parte d'um epha, e de azeite a terça parte d'um hin, para sovar a flor de farinha; por offerta de manjares para o Senhor, em estatutos perpetuos e continuos.
Pia kila siku asubuhi pamoja na hiyo sadaka utatoa sadaka ya nafaka, ikiwa na sehemu ya sita ya efa pamoja na theluthi moja ya hini ya mafuta ya kuchanganya na ule unga. Utoaji wa sadaka hii ya nafaka kwa Bwana ni amri ya daima.
15 Assim prepararão o cordeiro, e a offerta de manjares, e o azeite, todas as manhãs, em holocausto continuo.
Kwa hiyo mwana-kondoo na sadaka ya nafaka na mafuta vitatolewa kila siku asubuhi kwa ajili ya sadaka ya daima ya kuteketezwa.
16 Assim diz o Senhor Jehovah: Quando o principe der um presente da sua herança a algum de seus filhos, isto será para seus filhos: será possessão d'elles por herança.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ikiwa mkuu atawalaye atatoa zawadi kutoka kwenye urithi wake na kumpa mmoja wa wanawe, hiyo zawadi itakuwa pia kwa wazao wake, itakuwa mali yao kwa urithi.
17 Porém, dando elle um presente da sua herança a algum dos seus servos, será d'este até ao anno da liberdade; então tornará para o principe, porque herança d'elle é; seus filhos, elles a herdarão.
Hata hivyo, kama atatoa zawadi kutoka urithi wake na kumpa mmoja wa watumishi wake, mtumishi anaweza kuiweka mpaka mwaka wa uhuru, kisha itarudishwa kwa mkuu anayetawala. Urithi wake ni wa wanawe peke yao, ni mali yao.
18 E o principe não tomará nada da herança do povo, para os defraudar da sua possessão: da sua possessão deixará herança a seus filhos, para que o meu povo não seja espalhado, cada um da sua possessão.
Mkuu anayetawala hana ruhusa kuchukua urithi wowote wa watu na kuwaondoa kwenye mali zao. Mkuu atawalaye atawapa wanawe urithi wao, kutoka kwenye mali zake mwenyewe, ili kwamba pasiwe na mtu wangu yeyote atakayetengwa na urithi wake.’”
19 Depois d'isto me trouxe pela entrada que estava ao lado da porta, ás camaras sanctas dos sacerdotes, que olhavam para o norte; e eis que ali estava um logar em ambos os lados, para a banda do occidente.
Kisha mtu yule akanileta kwa kupitia kwenye ingilio lililokuwa kando ya lango mpaka kwenye vyumba vitakatifu vinavyoelekea kaskazini, ambavyo ni vya makuhani, naye akanionyesha mahali fulani upande wa mwisho wa magharibi.
20 E elle me disse: Este é o logar onde os sacerdotes cozerão o sacrificio pela culpa, e o sacrificio pelo peccado, e onde cozerão a offerta de manjares, para que a não tragam ao atrio exterior para sanctificarem o povo.
Akaniambia, “Mahali hapa ndipo makuhani watakapotokosea sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi na kuoka sadaka ya nafaka, kuepuka kuzileta katika ukumbi wa nje na kushirikisha utakatifu kwa watu.”
21 Então me levou para fóra, para o atrio exterior, e me fez passar ás quatro esquinas do atrio: e eis que em cada esquina do atrio havia outro atrio.
Baada ya hapo akanileta kwenye ukumbi wa nje na kunizungusha kwenye pembe zake nne, nami nikaona katika kila pembe ya huo ukumbi kulikuwa na ukumbi mwingine.
22 Nas quatro esquinas do atrio havia outros atrios com chaminés de quarenta covados de comprimento e de trinta de largura: estas quatro esquinas tinham uma mesma medida.
Katika pembe nne za huo ukumbi wa nje kulikuwa na kumbi nyingine, zenye urefu wa dhiraa arobaini na upana wake dhiraa thelathini, ambapo hizo kumbi kwenye hizo pembe nne zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
23 E um muro havia ao redor d'ellas, ao redor das quatro: e havia cozinhas feitas por baixo dos muros ao redor.
Mzunguko wa ndani wa hizo kumbi nne ulikuwa na ukingo wa jiwe, zikiwa na sehemu zilizojengwa kwa ajili ya moto kuzunguka chini ya huo ukingo.
24 E me disse: Estas são as casas dos cozinheiros, onde os ministros da casa cozerão o sacrificio do povo.
Akaniambia, “Hizi ndizo sehemu za kupikia ambazo wale wanaohudumu kwenye Hekalu watatokosea dhabihu za watu.”