< 2 Crônicas 14 >

1 E Abias dormiu com seus paes e o sepultaram na cidade de David; e Asa, seu filho, reinou em seu logar: nos seus dias esteve a terra em paz dez annos.
Naye Abiya akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake. Katika siku zake, nchi ikawa na amani kwa miaka kumi.
2 E Asa fez o que era bom e recto aos olhos do Senhor seu Deus.
Asa akatenda yaliyo mema na haki machoni pa Bwana Mungu wake.
3 Porque tirou os altares dos deuses estranhos, e os altos: e quebrou as estatuas, e cortou os bosques.
Akaziondoa madhabahu za kigeni na mahali pa juu pa kuabudia miungu, akayavunja yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Maashera.
4 E mandou a Judah que buscassem ao Senhor Deus de seus paes, e que observassem a lei e o mandamento.
Akawaamuru Yuda kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao na kutii sheria zake na amri zake.
5 Tambem tirou de todas as cidades de Judah os altos e as imagens do sol: e o reino esteve quieto diante d'elle.
Akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu za kufukizia uvumba kwenye kila mji katika Yuda, nao ufalme ulikuwa na amani katika utawala wake.
6 E edificou cidades fortes em Judah: porque a terra estava quieta, e não havia guerra contra elle n'aquelles annos; porquanto o Senhor lhe dera repouso.
Akajenga miji yenye ngome katika Yuda, wakati nchi ikiwa na amani. Hakuna mtu yeyote aliyepigana vita naye katika miaka hiyo, kwa kuwa Bwana alimstarehesha.
7 Disse pois a Judah: Edifiquemos estas cidades, e cerquemol-as de muros e torres, portas e ferrolhos, emquanto a terra ainda está quieta diante de nós, pois buscámos ao Senhor nosso Deus; buscámol-o, e deu-nos repouso em redor. Edificaram, pois, e prosperaram.
Mfalme akawaambia Yuda, “Tuijenge hii miji na tuizungushie kuta, pamoja na minara, malango na makomeo. Nchi bado ni yetu, kwa sababu tumemtafuta Bwana Mungu wetu, tulimtafuta naye ametupa raha kila upande.” Hivyo wakajenga na wakafanikiwa.
8 Tinha pois Asa um exercito de trezentos mil de Judah que traziam pavez e lança; e duzentos e oitenta mil de Benjamin, que traziam escudo e atiravam d'arco; todos estes eram varões valentes.
Asa alikuwa na jeshi la watu 300,000 kutoka Yuda, wenye ngao kubwa na mikuki na jeshi la watu 280,000 kutoka Benyamini, wenye ngao ndogo na pinde. Watu hawa wote walikuwa wapiganaji mashujaa.
9 E Zera, o ethiope, saiu contra elles, com um exercito de mil milhares, e trezentos carros, e chegou até Maresa.
Zera Mkushi akatoka kupigana dhidi yao akiwa na jeshi la watu maelfu ya maelfu na magari ya vita 300, nao wakaja mpaka Maresha.
10 Então Asa saiu contra elle: e ordenaram a batalha no valle de Zephatha, junto a Maresa.
Asa akatoka kumkabili, nao wakapanga vita katika Bonde la Sefatha karibu na Maresha.
11 E Asa clamou ao Senhor seu Deus, e disse: Senhor, nada para ti é ajudar, quer o poderoso quer o de nenhuma força; ajuda-nos, pois, Senhor nosso Deus, porque em ti confiamos, e no teu nome viemos contra esta multidão: Senhor, tu és nosso Deus, não prevaleça contra ti o homem
Kisha Asa akamlilia Bwana Mungu wake na kusema, “Ee Bwana, hakuna yeyote aliye kama wewe wa kuwasaidia wasio na nguvu dhidi ya wenye nguvu. Utusaidie, Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, kwa kuwa tunakutumainia wewe, nasi kwa jina lako tumekuja dhidi ya jeshi hili kubwa. Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, usiwaache wanadamu wakushinde wewe.”
12 E o Senhor feriu os ethiopes diante d'Asa e diante de Judah: e fugiram os ethiopes.
Bwana akawapiga Wakushi mbele ya Asa na Yuda. Wakushi wakakimbia,
13 E Asa, e o povo que estava com elle os perseguiram até Gerar, e cairam tantos dos ethiopes, que já não havia n'elles vigor algum; porque foram quebrantados diante do Senhor, e diante do seu exercito: e levaram d'ali mui grande despojo.
naye Asa na jeshi lake wakawafuatia mpaka Gerari. Idadi kubwa ya Wakushi ilianguka hata wasiweze kuinuka tena, wakapondapondwa mbele za Bwana na majeshi yake.
14 E feriram todas as cidades nos arredores de Gerar; porque o terror do Senhor estava sobre elles; e saquearam todas as cidades, porque havia n'ellas muita preza.
Watu wa Yuda wakachukua nyara nyingi sana, wakaangamiza vijiji vyote vinavyoizunguka Gerari, kwa kuwa hofu ya Bwana ilikuwa imewaangukia. Wakateka nyara vijiji hivi vyote, kwani kulikuwepo nyara nyingi huko.
15 Tambem feriram as malhadas do gado; e levaram ovelhas em abundancia, e camelos, e voltaram para Jerusalem.
Pia wakashambulia kambi za wachunga makundi ya wanyama wakachukua na kuyaswaga makundi ya kondoo, mbuzi na ngamia. Kisha wakarudi Yerusalemu.

< 2 Crônicas 14 >